Namna ya kuondoa harufu mbaya mdomoni kwa kutumia baking soda - Tofauti

Namna ya kuondoa harufu mbaya mdomoni kwa kutumia baking soda - Tofauti

Ok mkuu mi nilijua Ni kusukutua kumbe Hadi kumeza ruksa
nishaelewa kinachokuchanganya, ni kwamba mimi nimepost kuhusu kuondoa harufu ya mdomo, na kuna mtu akareply kuhusu kutibu UTI. nnachotaka uelewe ni kwamba kwenye kutibu UTI ndo unatakiwa umeze lakini kwa harufu ya mdomo unaswakia tu
 
Daah asantee...thats why nikiwa na safari ndefu hasa mkoani nahakikishaga bus haina ac ndo nikate tiket maana kufungua kioo kunarubusu mzunguko mkubwa wa hewa nisimkere jirani!!!
 
Ni kitu kigumu sana watu kukwambia kwamba una kikwapa au unatoa harufu mbaya mdomoni
Njia rahisi ya kujua harufu mbaya ya mdomoni ni kuramba nyuma ya kiganja cha mkono halafu nusa sehemu uliyoiramba
Aidha sidhani kama tatizo la harufu mbaya mdomoni linaanzia kinywani tuu bali wakati mwingine huanzia kwenye utumbo hivyo basi pamoja na dawa kama baking soda ambazo zitatumika kinywani tu si vibaya tukasistiza unywaji wa maji mengi ya uvuguvugu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu hii dawa si ni kali sana kuiweka kinywani haiwezi kuleta madhara ya kiafya kweli???
 
Naomba kuuliza juu ya afya nzuri ya fizi za meno ni ipi, je ni fizi zenye rangi nyeusi au za rangi ya kawaida km rangi ya ulimi
 
Ni kwamba nina imani kwamba watu wengi wanaifaham Baking soda vizuri na nimekuta huku huku JF wakielezea matumizi ya baking Soda inavyosatumika kama vile kusafishia masinki ya vyoo, na pia kuondolea harufu kwenye friji, kwenye nyama na hata nguo mpya

Lakini cha zaidi ambacho mimi ninataka kuwahabarisha ni jinsi ambavyo baking soda inaweza kuondoa harufu mbaya mdomoni, maana katika jambo linalowasumbua watu ni hilo hapo na unakosa amani kabisa.

Mimi naona tu niwaambie kwamba baking soda inatumika kutoa harufu mbaya mdomoni na kuna njia tatu za kuitumia ili uondoe harufu mdomoni

1. Ni kwamba unatakiwa utumie baking soda na kwa kuchanganya na maji (unaweza tumia maji ya baridi au ya moto ila ya moto ni mazuri zaidi)

2. Ni kuitumia kwa kuiweka kwenye mswaki na kuswaki nayo kama vile dawa ya meno

3. kuchanganya na maji ya malimao na kuswaki.
Somo murua kabisa
 
Back
Top Bottom