Namna ya kupika sambusa

Manda ya kuanda mwenyewe ni nzuri zaidi kuliko ya Azam... kanda unga kama wa chapati, kata vidonge vya wastani, sukuma kidonge kimoja kama mala mbili, paka mafuta ya kutosha .. pandishia kidonge kingine sukuma kwa pamoja cha chini kinakuwa kipana.. ikishapanuka weka kikaango kipana ktk moto bila mafuta kikishapata moto weka manda kwa muda kidogo kisha geuza ikiwa tayari banduazinatoka kama chapati laini sana na nyembamba..hifadhi zisikauke, kata kama msalaba tayari kwa kufunga sambusa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…