fakalava
JF-Expert Member
- Jul 16, 2015
- 4,459
- 6,027
Ni kweli hii biashara ina changamoto nyingi, inahitaji ujasiri mkubwa usiogope mambo ya Polisi wala Mahakama maana hivi vyombo ni Kwa ajiri ya watu/mtu na mtu mwenyewe ndiyo wewe.Hiyo mkaa ni dili nilishagalitolea macho. Ilikua nichome kwa gharama ya 13.000 then nikauze kwa 40.000 duh ila nilivoenda ofisi ya maliasili vitu wslivyoorodhesha nikashangaa faida ya mkaa iko Wapi..nikagundua ili ufaidike inabidi uifanye kwa dili. Nilipotaka kujaribu kupiga dili Kesho yake tu jamaa akakamatwa na semi trailer imejaa mkaa tegeta. Kwamba ni kesi inayohusu wizi wa nyara za serikali nikaona duh hii sasa hii kivumbi hii na mie navoogopaga jela dah nikaahirisha hiyo biashara. Ilikua nichomee moro huko then nishike masoko ya kufa m2 Dar. Dah nilishaseti kila kitu mara kesho yake nasoma mwananchi roli limekamatwa na mkaa tegeta tena ikaongelewa kama kosa kubwa sana nikapiga picha ya harufu ya jela nikaona isiwe tabu maana nshawahi kuswekwa rumande siku moja asubuhi hadi jioni kasheshe ya mazingira ya rumande ni kivumbi kuna nuka afu kunguni wanangata kinoma dah nikajiuliza sasa hii siku moja tu hivi je ukipewa miaka kadhaa jela inakuaje. Kwakweli fursa za biashara ziko nyingi ambazo ukizipiga unakua tajiri fasta ila sasa biashara za kukufanya utajirike fasta from nowhere nazo zinaambatana sana mambo ya jela hapo ndo tabu inapokuja.
Mkuu, usiogope habari unazoziona au kuzisikia, fikiria hiyo siku limekamatwa gari 1 je, mangapi yalisafirisha mkaa mpaka town.
Change your thinking man.