Nampongeza sana Mohamed Said : Nawalaumu Watanzania

Nampongeza sana Mohamed Said : Nawalaumu Watanzania

Huyu mzee wa historia ni mtu asiyekata tamaa. Naangalia Jukwaa la Historia kwa siku sikosi kuona threads zake mpaka mbili au tatu.

Pamoja na vijana wengi kwa ujivuni wao wanaonekana kutochangia mada zake badala yake wanaenda kujazana mwenye jukwaa la MMU Mzee hajakata tamaa.

Nampongeza kwa kuwa pamoja na kubezwa wakati mwingine huwa hajazibiki badala yake huendelea kushuka mistari tu.huyu ni nyani mzee amekwepa mishale mingi.

Utakuta mzee wa watu kashuka madini ila walio comment 3. This isnt fair.watanzania acheni unafiki. Mnataka akifa ndo mje mseme alikuwa anatia madini sana.

Yaani uzi wa Zero Q unapata comments za kumwaga mpaka pages 200 au ile ya Kula tunda kimasikhara inafika pages 1000+ ila harakati za Mzee wangu said nobody gives a shit.

Mods muwe mnalazimisha watu wachangie mada zake.
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
Walazimishwe,watake wasitake.
 
Tatizo maudhui ya kidin din na kuponda serikal na kuiita ya mfumo wa din flan kisha kuonyesha din flan ndio ilipigania uhuru wa nchi hii..hii nadhan ni kero watu wasiopenda.
Au namchanganya huyu bwana?
Siyo kidini Sana
Tatizo wasomi wetu na viongozi wetu wote wakisema historia wanaanzia kwa nyerere na kuoshia kwa nyerere hiyo ndio tatizo Kama vile yeye ndie wakwanza kuanzisha harakati za uhuru
 
Siyo kidini Sana
Tatizo wasomi wetu na viongozi wetu wote wakisema historia wanaanzia kwa nyerere na kuoshia kwa nyerere hiyo ndio tatizo Kama vile yeye ndie wakwanza kuanzisha harakati za uhuru
Hapo ndo wanapofanya makosa ..nyerere alipokea kijiti kutoka kwa watangulizi wke kwnn hatutaki kuthamini mchango wao?
 
Chizi Maarifa nadhani una lako jambo , ha ha ha

Katika mjadala wa miezi 6 mfululizo tulionyesha matundu ya historia ya Mohamed kwa nia njema tu.
Aliposhindwa kuyatetea akatujuza kwa lugha nzuri '' Ninaandika historia ya Wazee wangu wa kidongo chekundu''

Tulimwambia , alaa ! kama ni hilo hakuna shida. Kuwakumbuka wazee ni jambo lenye tija na lina hekma zake.

Nikupe mfano, juzi kaleta uzi unaoongelea alipokuwa na Hamza Aziz wakila futari.
Sasa hapo tutachangia nini?
Mzee kaeleza futari na yaliyojiri, unakubali au unakanusha nini.!!! Kama kulikuwa hakuna makaimati!

Siku iliyofuata kaeleza kuhusu mtaa za Sheikh Bad na Yusuf Chembera. Kawaeleza wazee wake.
Hapo unakataa nini mtu kuwaandika wazee wake?

Kuna siku anatueleza kuhusu Bi Mluguru, sasa hapo unakanusha au unachangia nini. Hatukuwepo kichangani au kidongo chekundu , yajuzu nini kuleta indhara kwa yeye anayewaeleza wazee wake!

Ni hayo tu, masalam
 
Nguruvi3 isauti ya nguruvi. Nmekuelewa. Kama alisema anazungumzia HISTORIA YA WAZEE WAKE HAPO KWA KWELI TUTAKOSA LA KUSEMA. NI SAWA NAMI NIJE NISEME NAZUNGUMZIA HISTORIA YA FAMILIA AU JAMAA ZANGU

Akianza kuzungumzia HISTORIA YA TAIFA BASI tusimtupe mkono....angalau tuchangie changie kitu. Maana haileti picha nzuri nyuzi zake mnazipita tu utadhani ni za matangazo yà kuuza shombo ya samaki.


Chizi Maarifa nadhani una lako jambo , ha ha ha

Katika mjadala wa miezi 6 mfululizo tulionyesha matundu ya historia ya Mohamed kwa nia njema tu.
Aliposhindwa kuyatetea akatujuza kwa lugha nzuri '' Ninaandika historia ya Wazee wangu wa kidongo chekundu''

Tulimwambia , alaa ! kama ni hilo hakuna shida. Kuwakumbuka wazee ni jambo lenye tija na lina hekma zake.

Nikupe mfano, juzi kaleta uzi unaoongelea alipokuwa na Hamza Aziz wakila futari.
Sasa hapo tutachangia nini?
Mzee kaeleza futari na yaliyojiri, unakubali au unakanusha nini.!!! Kama kulikuwa hakuna makaimati!

Siku iliyofuata kaeleza kuhusu mtaa za Sheikh Bad na Yusuf Chembera. Kawaeleza wazee wake.
Hapo unakataa nini mtu kuwaandika wazee wake?

Kuna siku anatueleza kuhusu Bi Mluguru, sasa hapo unakanusha au unachangia nini. Hatukuwepo kichangani au kidongo chekundu , yajuzu nini kuleta indhara kwa yeye anayewaeleza wazee wake!

Ni hayo tu, masalam
 
Chizi...
Haya mambo yanataka subra.

Nilipoanza kuandika kurekebisha historia ya TANU kwanza nilikutana na ghadhabu za wasomaji na vitisho.

Mijadala ikawa inajaza na kuna mjadala ulivunja rekodi kwa kuenda miezi sita bila kusimama.

Mimi nikiwa peke yangu na watu wengine wachache.

Taratibu wasomaji wakatambua kuwa ninayoandika ndiyo ukweli wenyewe.

Mmoja mmoja wakakimbia ulingoni wakaniacha kwani hawana la kusema kwa kuwa kwenye ukweli uongo hujitenga.

JF ni moja ya sehemu moja katika nyingi zinapokwenda makala zangu kwa hiyo nina wasomaji wengi kiasi wanaponiandikia naelemewa.

Pili JF ndipo ilipo maktaba yangu kuu ukitoa blog yangu: mohamedsaidsalum.blogspot.com.

Hapa ndipo ninapochomoa link kwa ajili ya rejea na makala zinarudi miaka 10 nyuma.

Nakushukuru sana kwa kujali.
kile kitabu chako cha historia ya uhuru nakipata wapi?
 
Chizi Maarifa nadhani una lako jambo , ha ha ha

Katika mjadala wa miezi 6 mfululizo tulionyesha matundu ya historia ya Mohamed kwa nia njema tu.
Aliposhindwa kuyatetea akatujuza kwa lugha nzuri '' Ninaandika historia ya Wazee wangu wa kidongo chekundu''

Tulimwambia , alaa ! kama ni hilo hakuna shida. Kuwakumbuka wazee ni jambo lenye tija na lina hekma zake.

Nikupe mfano, juzi kaleta uzi unaoongelea alipokuwa na Hamza Aziz wakila futari.
Sasa hapo tutachangia nini?
Mzee kaeleza futari na yaliyojiri, unakubali au unakanusha nini.!!! Kama kulikuwa hakuna makaimati!

Siku iliyofuata kaeleza kuhusu mtaa za Sheikh Bad na Yusuf Chembera. Kawaeleza wazee wake.
Hapo unakataa nini mtu kuwaandika wazee wake?

Kuna siku anatueleza kuhusu Bi Mluguru, sasa hapo unakanusha au unachangia nini. Hatukuwepo kichangani au kidongo chekundu , yajuzu nini kuleta indhara kwa yeye anayewaeleza wazee wake!

Ni hayo tu, masalam
Nguruvi3,
Tatizo linalokuhangaisha ni kuwa historia ya wazee wangu isingepata umaarufu huu ambao ndiyo unaokuhangaisha ila imemgusa Julius Kambarage Nyerere.

Historia iliyokuwa ikisomeshwa hadi Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam ni ile ya Nyerere kaunda TANU.

Mimi nikaja na historia hii ya wazee wangu.

Nikasema haiwezekani iwe TANU iundwe na Nyerere na hapo nikauliza vipi kuhusu Abdul Sykes.

Abdul ndiye aliyempokea Nyerere na akaishi na yeye nyumbani kwake na Nyerere mipango ya TANU kaikuta pale mwaka wa 1952.

Kadi ya TANU ya Ally Sykes no. 2 baada ya Nyerere no. 1 Abdul kadi no. 3, Dossa Aziz no. 4, Dennis Phombeah no. 5 Mnyasa kutoka Nyasaland, no. 6 Dome Okochi Budohi Mkenya.

Ulikuwa unayajua haya?

Hapo ndipo mjadala ukaanza nikaeleza mengi sana.

Ikiwa nyie mna historia yenu nyingine ya TANU iliyo kamili na mnaiona hii ya Abdul Sykes ina matundu mimi sina tatizo na hilo.

Uamuzi uko kwa wasomaji.
 
Nguruvi3 isauti ya nguruvi. Nmekuelewa. Kama alisema anazungumzia HISTORIA YA WAZEE WAKE HAPO KWA KWELI TUTAKOSA LA KUSEMA. NI SAWA NAMI NIJE NISEME NAZUNGUMZIA HISTORIA YA FAMILIA AU JAMAA ZANGU

Akianza kuzungumzia HISTORIA YA TAIFA BASI tusimtupe mkono....angalau tuchangie changie kitu. Maana haileti picha nzuri nyuzi zake mnazipita tu utadhani ni za matangazo yà kuuza shombo ya samaki.
Chizi...
Hii ni moja ya historia nyingi za wazee wangu wakati wakipigania uhuru wa Tanganyika:

"Dunia ni ndogo sana.

Siku ya Jumanne nilikuwa kwenye foleni benki Mlimani City na jirani yangu alikuwa amekaa binti mdogo na katika vitu alivyokuwanavyo ni kitabu, ''Vuta, Nkuvute,'' cha Adam Shafi.

Kitabu hiki ni toleo jipya hivyo ikanivutua ''cover,'' yake nikamuomba huyu binti nikiangalie kile kitabu na hapo ndipo mazungumzo yalipoanza.

Kama nilivyotangulia kusema, dunia ni ndogo sana.

Yule binti akaniambia kuwa yeye ni mjukuu wa Mzee Omari Londo.

Kwa wasiomjua Omar Londo huyu ni mmoja wa wanachama wa mwanzo wa TANU aliyekuwa akiishi Mtaa wa Somali, Gerezani.

Hivi sasa mtaa huo umebadilishwa jina na unaitwa Mtaa wa Omari Londo kwa heshima ya mzalendo huyu.

Nikamwambia kuwa namfahamu vyema babu yake.

Akanifamisha pia kuwa yeye ni kitukuu cha Bi. Tatu binti Mzee.

Kwa wasiomfahamu Bi. Tatu binti Mzee ni kuwa Bi. Tatu binti Mzee ndiye chanzo cha Bi. Titi kuingia TANU na kuwa kiongozi mkubwa aliyeongoza wanawake katika kuijenga TANU na kupandisha haiba ya Mwalimu Nyerere wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.

Hiki kitukuu cha Bi. Tatu bint Mzee ni muhitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na akanitajia jina lake kuwa ni Hawa binti Ali.

Hawa akanieleza kuwa ilikuwa wakati wa kupigania uhuru ndipo Bi. Tatu bint Mzee alipomtoa mwanae aolewe na Omari Londo na hivyo mama yake kuzaliwa lakini sasa ni marehemu.

Hawa alifahamisha kuwa amesikia mengi katika kupigania uhuru wa Tanganyika nyumbani kwao akitajwa babu yake na wazee wengine lakini kilichomstaajabisha ni kuwa historia hii hajaweza kuisoma popote.

Hapo ndipo nilipojitambulisha na nikamuahidi kumrushia picha ya bibi mkuu wake akimsindikiza Mwalimu Nyerere Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam safari ya kwanza anakwenda UNO, New York mwaka wa 1955 akiwa na Bi. Titi Mohamed, Bi. Chiku Kikusa na akina mama wengine.

Nikamweleza kuwa nimezaliwa Kipata na wazee wangu wameishi mitaa kadhaa ya Gerezani katika 1920s hadi kufikia 1960s pamoja na Mtaa wa Somali jirani na kwa babu yake.

Bahati mbaya sikuweza kumkumbuka marehemu mama yake.

Hii picha hapo chini nilipewa na Abdulrahman Ali Msham mtoto wa Ali Msham mmoja wa wazalendo walioingia TANU mapema sana kupigania uhuru.

Sikiweza kumtambua Bi. Tatu binti Mzee hadi jana Hawa baada ya kumpelekea picha hii aliponirudishia majibu na kunambia kuwa Bi. Tatu binti Mzee ni huyo wa pili kulia waliokaa na wa nne ni Bi. Titi Mohamed.

Ali Msham ni wa pili kushoto waliosimama.
Hili ni tawi la kwanza la TANU Magomeni."

2018
 
Chizi...
Hii ni moja ya historia nyingi za wazee wangu wakati wakipigania uhuru wa Tanganyika:

"Dunia ni ndogo sana.

Siku ya Jumanne nilikuwa kwenye foleni benki Mlimani City na jirani yangu alikuwa amekaa binti mdogo na katika vitu alivyokuwanavyo ni kitabu, ''Vuta, Nkuvute,'' cha Adam Shafi.

Kitabu hiki ni toleo jipya hivyo ikanivutua ''cover,'' yake nikamuomba huyu binti nikiangalie kile kitabu na hapo ndipo mazungumzo yalipoanza.

Kama nilivyotangulia kusema, dunia ni ndogo sana.

Yule binti akaniambia kuwa yeye ni mjukuu wa Mzee Omari Londo.

Kwa wasiomjua Omar Londo huyu ni mmoja wa wanachama wa mwanzo wa TANU aliyekuwa akiishi Mtaa wa Somali, Gerezani.

Hivi sasa mtaa huo umebadilishwa jina na unaitwa Mtaa wa Omari Londo kwa heshima ya mzalendo huyu.

Nikamwambia kuwa namfahamu vyema babu yake.

Akanifamisha pia kuwa yeye ni kitukuu cha Bi. Tatu binti Mzee.

Kwa wasiomfahamu Bi. Tatu binti Mzee ni kuwa Bi. Tatu binti Mzee ndiye chanzo cha Bi. Titi kuingia TANU na kuwa kiongozi mkubwa aliyeongoza wanawake katika kuijenga TANU na kupandisha haiba ya Mwalimu Nyerere wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.

Hiki kitukuu cha Bi. Tatu bint Mzee ni muhitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na akanitajia jina lake kuwa ni Hawa binti Ali.

Hawa akanieleza kuwa ilikuwa wakati wa kupigania uhuru ndipo Bi. Tatu bint Mzee alipomtoa mwanae aolewe na Omari Londo na hivyo mama yake kuzaliwa lakini sasa ni marehemu.

Hawa alifahamisha kuwa amesikia mengi katika kupigania uhuru wa Tanganyika nyumbani kwao akitajwa babu yake na wazee wengine lakini kilichomstaajabisha ni kuwa historia hii hajaweza kuisoma popote.

Hapo ndipo nilipojitambulisha na nikamuahidi kumrushia picha ya bibi mkuu wake akimsindikiza Mwalimu Nyerere Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam safari ya kwanza anakwenda UNO, New York mwaka wa 1955 akiwa na Bi. Titi Mohamed, Bi. Chiku Kikusa na akina mama wengine.

Nikamweleza kuwa nimezaliwa Kipata na wazee wangu wameishi mitaa kadhaa ya Gerezani katika 1920s hadi kufikia 1960s pamoja na Mtaa wa Somali jirani na kwa babu yake.

Bahati mbaya sikuweza kumkumbuka marehemu mama yake.

Hii picha hapo chini nilipewa na Abdulrahman Ali Msham mtoto wa Ali Msham mmoja wa wazalendo walioingia TANU mapema sana kupigania uhuru.

Sikiweza kumtambua Bi. Tatu binti Mzee hadi jana Hawa baada ya kumpelekea picha hii aliponirudishia majibu na kunambia kuwa Bi. Tatu binti Mzee ni huyo wa pili kulia waliokaa na wa nne ni Bi. Titi Mohamed.

Ali Msham ni wa pili kushoto waliosimama.
Hili ni tawi la kwanza la TANU Magomeni."

2018
Chizi,
Angalia picha hiyo hapo chini:
Screenshot_20200629-102639.jpg
 
Nguruvi3,
Tatizo linalokuhangaisha ni kuwa historia ya wazee wangu isingepata umaarufu huu ambao ndiyo unaokuhangaisha ila imemgusa Julius Kambarage Nyerere.

Historia iliyokuwa ikisomeshwa hadi Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam ni ile ya Nyerere kaunda TANU.

Mimi nikaja na historia hii ya wazee wangu.

Nikasema haiwezekani iwe TANU iundwe na Nyerere na hapo nikauliza vipi kuhusu Abdul Sykes.

Abdul ndiye aliyempokea Nyerere na akaishi na yeye nyumbani kwake na Nyerere mipango ya TANU kaikuta pale mwaka wa 1952.

Kadi ya TANU ya Ally Sykes no. 2 baada ya Nyerere no. 1 Abdul kadi no. 3, Dossa Aziz no. 4, Dennis Phombeah no. 5 Mnyasa kutoka Nyasaland, no. 6 Dome Okochi Budohi Mkenya.

Ulikuwa unayajua haya?

Hapo ndipo mjadala ukaanza nikaeleza mengi sana.

Ikiwa nyie mna historia yenu nyingine ya TANU iliyo kamili na mnaiona hii ya Abdul Sykes ina matundu mimi sina tatizo na hilo.

Uamuzi uko kwa wasomaji.
Sikiliza:
 
"Mohamed Said, post: 35857774, member: 12431"]
Nguruvi3,
Tatizo linalokuhangaisha ni kuwa historia ya wazee wangu
Mimi nikaja na historia hii ya wazee wangu.
Chizi Maarifa upo? Mwenyewe anatoa ushuhuda, anachokiandika ni habari za Wazee wake, yajuzu nini kumleta indhara ?
Nikasema haiwezekani iwe TANU iundwe na Nyerere na hapo nikauliza vipi kuhusu Abdul Sykes.
Halafu
Abdul ndiye aliyempokea Nyerere na akaishi na yeye nyumbani kwake na Nyerere mipango ya TANU kaikuta pale mwaka wa 1952.
Hapa anamaanisha TANU ilikuwepo, Nyerere akawakuta akina Abdul na wenzake wakiwa na chama chao cha TANU.
Kadi ya TANU ya Ally Sykes no. 2 baada ya Nyerere no. 1 Abdul kadi no. 3, Dossa Aziz no. 4, Dennis Phombeah no. 5 Mnyasa kutoka Nyasaland, no. 6 Dome Okochi Budohi Mkenya.
Sasa hapa Bwana Chizi ndipo tunaingia, kuna kujichanganya na kuchanganya umma. Kawakuta watu na chama chao tayari, halafu Nyerere akawa na kadi Namba 1 na mwenye chama Bw Abdul Kleist Sykes Mbuwane akawa na namba 3.
Ulikuwa unayajua haya?
Hapana , sikujua 3 inaanza halafu 1 inafuata.
Uamuzi uko kwa wasomaji.
 
Back
Top Bottom