Namuunga Mkono Mwana FA, na wasanii wengine kufanya show zao tarehe moja na show ya komando JIDE

Jospina

JF-Expert Member
Joined
Apr 19, 2013
Posts
2,421
Reaction score
1,395
watu wanataka Jide aachiwe wateja "bure bure",mi nahitaji apambane vilivyo kwani ndo biashara inavyotaka iwe...Wanamuziki wooote wafanye maonyesho yao siku hiyo it doesn't matter to me ila kwa wafuasi wa Jide wataona ameonewa.Ni muda wa kukomaa kibiashara sasa na kuacha manung'uniko,she has to earn us sio niende kwa Jide kisa kaonewa na Ruge (sympathy),NO,niende kwake kwa kuwa natarajia kitu bora.
 
kwani show ya jaydee inazuia show za wasanii wengine? hakuna ubaya kwa mwana FA kwa show lakini si kutumika.
 
MwanaFA amepewa ubalozi wa fistula kwa msaada wa hao hao mafisadi wa mziki na ni hao hao wanaoandaa show yake,unaonaje hapo???!! Fikiri nje ya box mkuu na kumbuka FA Katana nyimbo ngapi na Jide zikavuma na tuzo juu?? Kuna dhambi wakipishana???!!!
 
Mleta mada ungejaribu kutumia akili kidogo wala usingepost hayo mashudu.

Sote tunajua Lady JD yuko kwenye vita dhidi ya mnyonyaji wa wasanii yaani Clauds Entartainment(Ruge na Kusaga) sasa inakuwaje katikati ya vita hii, baadhi ya wasanii wenzake wa Bongo flavour(MwanaFA, Linah, Barnaba, Matonya, TID nk) wanajaribu kusimama kinyume naye?

Katika hili unataka tumuone mwanaFA ni mshindani wa Lady JD au sehemu ya Clauds Entartainment?

Jana alikuwa anafanyiwa Sugu, Leo anafanyiwa Lady JD, kesho nani?
 

Wasanii wenzake kivipi? Kwani walianza music siku moja . Kila mwanamuziki yuko kivyake na kaingia kwenye music kivyake. Kuhusu show hivi mbona sijawahi kusikia twanga pepeta , msondo , akudo au sikindi akilalamika mwenzake akifanya show siku moja . Si kila mtu ana wapenzi wake au
 
ewaaah swadakta bwana KUSHAGA, hii ni biashara package kazi yako vizuri watu wanunue sio kullalamika tu kwenye mitandao unaoneea huruma clouds clouds wakati kazi mbovu mwambie mmeo akutoe na TIMES FM mana alivyokuwa clouds likimaliza tu honi la jahazi unaskia live show ya Jaydee na machozi, halafu hawa wanaomtetea humu waende basi na kwenye band kule km wana uchungu kila IJumaa MACHOZI BAND jamani nendeni mana watu wanahudhuria ni wachache jama nyie waenye uchungu...acheni kubinua midomo humu ndani na kubishana hadi mnatoa povu wakati tamsha za jaydee huendi utakuwa mnafiki...
 
MwanaFA amepewa ubalozi wa fistula kwa msaada wa hao hao mafisadi wa mziki na ni hao hao wanaoandaa show yake,unaonaje hapo???!! Fikiri nje ya box mkuu na kumbuka FA Katana nyimbo ngapi na Jide zikavuma na tuzo juu?? Kuna dhambi wakipishana???!!!

Good say.
 

haya bwana
 

Sikinde na Msondovwamepiga pamoja mara kadhaa ! Hata Salma Khamis Kidogo na Hadija Kopa (Muungano v/s TOT Plus) wamepambana 'live' mara kadhaa !
Ukiwa na mtazamo wa kibiashara utaelewa lakini ukiwa na mtazamo wa 'kikupe' kama Ruge hutaelewa.
 
Mwana FA nilishamtoa kichwani baada ya kuwa kibaraka wa clouds.
 
Bongo bana wenyewe kwa wenyewe walana

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Dawa ya Ruge ni SUGU................Antivurs, VINEGA mbona walibeep tu? Sasa hivi mambo yangelikuwa Kinega !
 
Kweli wewe kupe, na fikra za kikupe kupe tu
 
Nimewahi kusikia kwamba Mwana FA ni mwanamuziki msomi-kwamba ana masters!
Kama mtu anaweza kuwa na elimu ya shahada ya pili lakini hajiamini na hawezi kujitegemea basi hata hiyo elimu aliyoipata ni bure kabisa bora asingepoteza muda kusoma.

Hawa kupe Ruge na Kusaga wamekuwa wakiwatumia wanamuziki wa bongo waziwazi bila kificho na wao wanajua lakini wamebung'aa tu kama mazuzu!
 
huyu mwana FA kweli shule aliyosoma bado haijamsaidia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…