Nani adui wa vijana katika Kujiajiri. Ni Uthubutu, Serikali, au Malezi na Mazingira?

Asante Sana mkuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi ninadhani tatizo ni kwamba vijana tuna mawazo yanayorandana, mfano ukiona flani kafanikiwa kwa kulima nawe unataka kulima. Je una passion ya kuwa mkulima?
Katika maisha nimegundua utafanikiwa zaidi hasa ukianza na kitu unachokipenda toka moyoni kikawa ndiyo chanzo cha kukufunguliwa milango mingine.
Mimi sikuwahi kuajiliwa moja kwa moja na kampuni wala taasisi yoyote. Lakini imenichukua muda kugeuza kile ninachopenda kuwa pesa kwasababu sikujua nitawezaje kumonetize ninachopenda kuwa pesa mpaka ilipofika 2018.
Nashukuru kwasasa ninaona mwanga na kwakuwa nafanya kitu ninachopenda hata nikikutana na magumu siachi na ninaona baada ya miaka kadhaa nitakuwa mbali sana.
Tatizo siyo mtaji, tatizo ni kujua wataka nini na kufuata ndoto zako...
 
kwel mkuu aslimia kubwa ndo hivo.Uvivu nishida na Tamaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna Theory nisizozipenda kama za kufanya unachipenda, ni penda unachofanya sio fanya unachopenda.
 
Kama unafanya usichokipenda kama msingi/ ngazi ya kukanyagia kuelekea kufanya unachokipenda uko sahihi

Ufanisi na ubunifu unakuwa kwa kiwango cha juu pale unapofanya unachokipenda, ni rahisi kufanikiwa sana

Hakuna Theory nisizozipenda kama za kufanya unachipenda, ni penda unachofanya sio fanya unachopenda.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…