Chaliifrancisco
JF-Expert Member
- Jan 17, 2015
- 26,021
- 79,710
- Thread starter
-
- #21
Pardon! Would you please clarify?The buck stops with her!
Kuna mwamba fulan alisema ivo.....Unamaanisha nini mkuu?
Kweli mkuu mimi ni Simba damu lakini Yanga leo wamefanya kitendo cha kiume. Tumezoea kuvunja sheria hovyo sana.Yanga chama langu na sjuti kulifahamu,wamenkosha sana,mwnaume lazma usimamie misimamo yako!
Siasa isingeingia endapo Tff wangekuwa wanauwezo wa kujisimamia.Kuchanganya siasa na mpira ndio tatizo.
Wamenikera balaahSure kabisa. Hawa jamaa sheria wanazijua wazi na wamezivunja makusudi kabisa tena bila kutoa ufafanuzi au sababu ya msingi katika barua yao.
Hapo ndipo shida inapoanziaKuchanganya siasa na mpira ndio tatizo.
Serikali sikivu ya Wanyonge[emoji724]Mods msiunge uzi🛇
Kama tunavyojua ni muda wa wiki kadhaa sasa kumekuwa na vuguvugu la pambano la mpira wa miguu kati ya watani wa jadi Simba na Yanga almaarufu kama Kariakoo Derby.
Pambano hili lililosubiriwa kwa hamu kubwa hatimae lilikuwa lifanyike leo tarehe 8 Mei saa 11:00 jioni. Lakini katika hali isiyokuwa ya kawaida muda wa mchana wa leo ikaenea taarifa kutoka TFF kuwa muda wa kuanza pambano umesogezwa mbele mpaka 1:00 usiku na kuwa hiyo imetokana na maagizo ya wizara.
Chakusikitisha zaidi barua hiyo kwa umma wa wadau wa michezo (vilabu, media, mashabiki) haikuianisha sababu za kusogezwa mbele kwa pambano hilo. Zaidi ya kusema tu ni maagizo ya wizara.
Sasa napenda kwanza kuwauliza TFF (Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania) na TPLB (bodi ya ligi) je walipopokea agizo hilo walizingatia sheria inayohusiana na jambo hilo. Je kama walizingatia waliwaeleza waliowapa agizo hilo kuhusu sheria hiyo? Je kama waliwaeleza ni majibu gani walipewa mpaka kuamua kuvunja sheria hiyo?
Tunatambua kuwa muda wa kuahirisha au kusogeza mbele muda wa pambano inaweza kufanyia chini ya masaa 24 (nikimaanisha kama ilivyofanywa leo) lakini kwa sababu maaalum. Cha ajabu ni kuwa mpaka sasa sio TFF wala Bodi ya Ligi waliotoa sababu hiyo/hizo maalumu za kusogeza mbele muda wa kuanza kwa mechi hiyo zaidi ya kusema kuwa ni agizo la wizara.
Je viongozi waliopewa dhamana ya kuongoza vyombo vyetu vihi hawana weledi juu ya sheria zinazosimamia soka letu?
Je gharama zilizotumiwa na vilabu katika kujiandaa na pambano hili zitafidiwa? Je gharama zilizotumiwa na mashabiki kusafiri kutoka mikoani au hata tarafa mbali mbali za jiji la Dar es Salaam zitafiwa na nani?
Je utaratibu utakuwa vipi kwa wale waliokuwa wamenunua tiketi kwaajili ya kutizama pambano hilo mubashara?
Je vombo vya habari vilivyotumia budget kuandaa vyombo vyao na watu wao kwaajili ya kurusha matangazo live katika channel za redio na runinga zitafidiwa na nani?
Je ni lini TFF na TPLB wataueleza umma wa Watanzania sababu za msingi za kusogezwa mbele kwa muda wa kuanza pambalo nilo na je watakapoeleza watawezaje ku justify kitendo hicho cha kutoa sababu baada ya usumbufu wote huu na sio kabla?
Haya ni maswali ambayo viongozi husika inabidi kuyajibu. Pia viongozi na mamlaka husika inabidi kuwajibika au ikibidi kuwajibishwa ili kuwa funzo siku nyingine.
Yanga wanajielewa sana aiseeh, msimamo walioonyesha walau umenipa auheniYanga chama langu na sjuti kulifahamu,wamenkosha sana,mwnaume lazma usimamie misimamo yako!
Watafuta hawa nao akili zao ni kama tff na bodi ya ligiUzi haufutwi tu bila sababu za msingi.
Yanga wamefata sheria ila hawana busara kwa maana kusogezwa masaa mbele hakuathiri kitu sana kuliko kama wangerudishwa nyuma masaa na wakasema chezeniKweli mkuu mimi ni Simba damu lakini Yanga leo wamefanya kitendo cha kiume. Tumezoea kuvunja sheria hovyo sana.
Ni sawa mkuu lakini wao wametumia kifungu cha sheria na labda wana sababu zao kwanini wamegomea mechi.Yanga wamefata sheria ila hawana busara kwa maana kusogezwa masaa mbele hakuathiri kitu sana kuliko kama wangerudishwa nyuma masaa na wakasema chezeni
Kama haijavunja terms na conditions za hapa thread haifutwi tu hovyo.Watafuta hawa nao akili zao ni kama tff na bodi ya ligi
Ngoja pakikucha tutasikia mengi.Serikali sikivu ya Wanyonge
Mimi washafuta nyuzi zangu nyingi hawa hawana maana wanataka vitu wanavyopenda waoKama haijavunja terms na conditions za hapa thread haifutwi tu hovyo.
Mwinyi kapewa Benz la kazi gani?Kawapa hasara Mpira wa leo pia kawapa hasara kwa kugawa Benz la ml450 utafikiri mwanae alishindwa kulinunua.
Bi mkubwa atutake radhi kwanza ikiwezekana ainame masaa mawili kama yule waziri wa japana sijui kuomba radhi
Mimi nawalaumu zaidi bodi ya ligi na TFF kwa kukubali kufanyiwa maamuzi na wanasiasa wakati kuna sheria zinaongoza masuala ya kimpira.
Shost we ni Simba au Yanga? Maana si kwa kukereka huko[emoji28]Wamenikera balaah