Wakuu hiki jina Taifa stars nani aliipa timu yetu yaTaifa? Linabeba ama kutangaza kitu gani kwa Nchi yetu?
Ninadhani kunapokuwa na mafanikio kwa timu ya Taifa ni fursa pia ya kutangaza alama maalumu ya Taifa ambayo bila shaka inaweza chochea pia utambulisho wetu na utalii wetu.
Mfano Uganda wanajiita the crane.
Bila shaka wakimaanisha ndege adimu wanaopatikana kwa wingi Uganda.
Wengine wanajiita "mamba weusi"
Wengine "Tai wa Jangwani"
Wengine "simba wa theranga"
Hapo jirani nadhani kwa sabbu ya machimbo ya shaba wanajiita "risasi za moto" chipolopolo.
Ama kule kusini wanajiita "Bafana bafana"
Je kwanini timu yetu ya Taifa isiwe na utambulisho maalumu wenye kuleta maana?
Mfano tukaiita timu yetu "the giraffe"..
"Tukiamini kuwa twiga ni mnyama anayekula majani ya juu ya miti."
Na anaeona Mbali zaidi adui yake kabla hajamkaribia. Pia Twiga ni kimbilio kwa wanyama wengi wasio weza kumuona adui yao kwa mbali..
Napendekeza timu yetu ya Taifa ya mpira wa Miguu iitwa "THE GIRAFFE "!