Nani alimwelewa stara thomas?

Nani alimwelewa stara thomas?

Huyu si ndo nilisikia hakupewa promo kwenye bongo fleva ndo maana hakua juu kama wanawake wenzake.... Afu kaenda kwenye INJILI ajapata tena promo kaamua kurud tena BONGO FLEVA........ INATAKIWA ATAMBUE KATIKA MUZIKI AU KUWA STAA YA KWAMBA ........SIO KILA MTU ANANYOTA YA MCHEZO ndo maana Kila Mwaka mtu kama FID Q apati tuzo sio kwamba hawez ila ananyota ya mchezo hivyo unaweza kuwa na kipaj kizur lakin watu wasikukubali sanaaa
 
tujuze hiyo ya kwenye red
japo kuna mtu kanijibia ila mimi sikuwa huko ni kwamba mama huyo hutoza pesa kubwa sana pindi mwanamziki mchanga akimuomba kushiriki uzinduzi wa nyimbo yake na hata kama ukimbembeleza yeyehushikilia msimamo huohuo kwa mana ya kwamba bwana alisema kale kwa mikono yako,so yupo kibiashara zaidi,nyingine hujiona yupo juu sana,mfano kuna askari mmoja ambaye ni rafiki wa familia aliwai kumkamata kwa makosa madogo ya barabarani akiwa na gali yake,akamjibu wewe askari unamjua unayeongea nae kwanza?askari akamjibu kwamba yeye yupo kazini mambo ya kujuana atamjulia kituoni.nyingine.....kwenye usiku wa matumaini uwanja wa taifa mwaka jana alikacha kuimba uwanjani na kuondoka licha ya gharama alizopewa na waandaajikisa eti kwa nini amewekwa na wasanii wa bongo fleva?amesahau hata hao wasanii ndo wanunuzi wa nyimbo zake na kwa mungu hakuna ubaguzi...ni mengi nimechoka kwa sasa....nampenda ila kwa hayo mambo yake kidogokidogo naanza kumsahau.....
 
jamani kama stara manyama uzembe yule sijui mr politician mtamuweka wapi?mwacheni bhana ameachia kitu shamba la matunda eee bwana eeeh!sauti kama kinanda,chezea stara weye!
 
Ni kitambo kidogo tokea mwanamama huyu alipohama fani ya bongo fleva kwenda muziki wa injili na sasa kurudi tena bongo fleva,kitu ambacho sikumwelewa ni pale kwenye kipindi cha leo tena-clouds wiki iliyopitakudai kwamba ameamua kurudi tena bongo fleva ili kujitafutia riziki,kwani mara ya kwnza alipokuwa anaenda kule gospel lidhani yale maneno ya kula madhabahuni yanawahusu hata waimbaji kumbe ni wachungaji hata alipoambiwa kwamba mbona kuna wengi waliofanikiwa kwenye injili bado alidai eti hakuna maslahi yale aliyotegemea na kule hakuna mshikamano kati ya waimbaji akimaanisha wale walio juu,sasa ambacho mimi sikumwelewaje aliokoka au alifuata maslahi?au mi ndo sikumuelewa?mana bado anadai japo karudi bonbo fleva eti ila bado kaokoka!

Haya ameyarudia alishayasema tena kwenye amplifaya ya Millard. Ushauri wangu kwa huyu mama ni nzuri akapima kwa kina anachokiongea on air. Mwisho wa siku atajivunjia heshima na kudharaulika sana na kushindwa kufanya biashara hata huko kwenye bongo flavour kinyume na yeye anavyotarajia.
 
Back
Top Bottom