Interest
JF-Expert Member
- Apr 11, 2015
- 3,434
- 7,072
Sijui ni lini tutakuwa serious kama nchi.
Mimi sifuatiliagi sana vipengele vya kisheria ila hii nimejikuta naipitia kwa sababu zangu binafsi. Nimecheka japo inakera sana.
Sheria hii ya ajabu kwanza ilitungwa kabla ya Katiba ya mwaka 1977. Yenyewe ilitungwa 1973. Nadhani ilitungwa na wakoloni. Hawa jamaa walikuwa walevi sana.
Haiwezekani sheria hii iweke ukomo wa kilevi kuwa ni 0.08g/dl aisee. Hapa ni kuruhusu madereva kuendesha roho za watu au mali wakiwa bwiii! Matokeo take ndio hizi ajali zisizoeleweka.
WHO yenyewe inaeleza kuwa dereva mwenye kiwango hicho cha ulevi anakua hatarini kupata ajali mara nne zaidi ya yule ambaye hajatumia pombe kabisa.
Bora tungefuata ushauri wa WHO kuwa ukomo wa ulevi uwe ni 0.05g/dl kwa madereva wazoefu na 0.02g/dl kwa madereva wapya wasio na uzoefu.
Pia sheria hii ni kama imewaacha salama walevi wanaotembea kwa miguu. Hawa hawana limit kabisa kisheria na wanavuka barabara. Fikiria!
Acha hilo la matingasi. Kuna wale jamaa wanaopiga misele mitaani kwa fujo. Unakuta gari imeachiwa spidi kitaa unabaki kushika mdomo. Kuna watoto wanabutuliwa kila siku.
Haya yote tunaweza kusema ni ajali na uzembe. Sawa. Adhabu zake zinatosha kukomesha? Kichekesho.
Dereva mwenye leseni faini yake haizidi laki moja kwa makosa yote ya barabarani, hata akigonga na kuua. Mlevi anayetembea kwa miguu hana faini kabisa.
Haya mapitio ya Sheria hii yaliyofanywa mwaka 2002 yalirekebisha nini sasa?
Kwangu mie nimeona hayo. Najua humu kuna wataalamu watanielekeza kisheria ni vipi tunaweza kupata marekebisho mapya yapelekwe bungeni kama mapendekezo. Angalau kupitia mtandao tutakuwa tutakuwa tumewasaidia hawa jamaa kutunga Sheria inayoeleweka.
Karibuni mawakili na wanasheria wasomi mtudadavulie!
Mimi sifuatiliagi sana vipengele vya kisheria ila hii nimejikuta naipitia kwa sababu zangu binafsi. Nimecheka japo inakera sana.
Sheria hii ya ajabu kwanza ilitungwa kabla ya Katiba ya mwaka 1977. Yenyewe ilitungwa 1973. Nadhani ilitungwa na wakoloni. Hawa jamaa walikuwa walevi sana.
Haiwezekani sheria hii iweke ukomo wa kilevi kuwa ni 0.08g/dl aisee. Hapa ni kuruhusu madereva kuendesha roho za watu au mali wakiwa bwiii! Matokeo take ndio hizi ajali zisizoeleweka.
WHO yenyewe inaeleza kuwa dereva mwenye kiwango hicho cha ulevi anakua hatarini kupata ajali mara nne zaidi ya yule ambaye hajatumia pombe kabisa.
Bora tungefuata ushauri wa WHO kuwa ukomo wa ulevi uwe ni 0.05g/dl kwa madereva wazoefu na 0.02g/dl kwa madereva wapya wasio na uzoefu.
Pia sheria hii ni kama imewaacha salama walevi wanaotembea kwa miguu. Hawa hawana limit kabisa kisheria na wanavuka barabara. Fikiria!
Acha hilo la matingasi. Kuna wale jamaa wanaopiga misele mitaani kwa fujo. Unakuta gari imeachiwa spidi kitaa unabaki kushika mdomo. Kuna watoto wanabutuliwa kila siku.
Haya yote tunaweza kusema ni ajali na uzembe. Sawa. Adhabu zake zinatosha kukomesha? Kichekesho.
Dereva mwenye leseni faini yake haizidi laki moja kwa makosa yote ya barabarani, hata akigonga na kuua. Mlevi anayetembea kwa miguu hana faini kabisa.
Haya mapitio ya Sheria hii yaliyofanywa mwaka 2002 yalirekebisha nini sasa?
Kwangu mie nimeona hayo. Najua humu kuna wataalamu watanielekeza kisheria ni vipi tunaweza kupata marekebisho mapya yapelekwe bungeni kama mapendekezo. Angalau kupitia mtandao tutakuwa tutakuwa tumewasaidia hawa jamaa kutunga Sheria inayoeleweka.
Karibuni mawakili na wanasheria wasomi mtudadavulie!