James Martin
JF-Expert Member
- Apr 2, 2016
- 1,206
- 1,509
Nafikiri mpaka sasa Watanzania wengi watakuwa wamepata habari kuhusu tukio la spika wa bunge kujiuzuru. Swali litakalofuata ni, nani anafaa kuziba pengo lake?
Mimi binafsi nafikiri Mussa Azzan Zungu ni mtu sahihi wa kujaza nafasi hiyo ya spika wa bunge.
Sababu ya kwanza ni kwamba Mh. Zungu ana uzoefu mkubwa wa kuongoza vikao vya bunge. Binafsi nimeshawahi kumuona mara kadhaa akiongoza vikao vya kamati za bunge kwa ufanisi mkubwa.
Pili, ni mtu anayekubalika na kuheshimika kwenye chama chake tawala na vyama vya upinzani.
Na mwisho, huyu mzee ni mtu mwenye busara. Kiti cha spika wa bunge kinahitaji mtu mwenye busara, hususan ukizingatia bunge ni mhimili wa malumbano hali inayopelekea wakati mwingine wabunge kupandwa na jazba. Kwahiyo, anahitajika mtu kama yeye ili kuweza kutuliza mambo.
Unakaribishwa kutoa mawazo yako. Unafikiri nani mwingine anafaa kushika nafasi ya uspika?
Mimi binafsi nafikiri Mussa Azzan Zungu ni mtu sahihi wa kujaza nafasi hiyo ya spika wa bunge.
Sababu ya kwanza ni kwamba Mh. Zungu ana uzoefu mkubwa wa kuongoza vikao vya bunge. Binafsi nimeshawahi kumuona mara kadhaa akiongoza vikao vya kamati za bunge kwa ufanisi mkubwa.
Pili, ni mtu anayekubalika na kuheshimika kwenye chama chake tawala na vyama vya upinzani.
Na mwisho, huyu mzee ni mtu mwenye busara. Kiti cha spika wa bunge kinahitaji mtu mwenye busara, hususan ukizingatia bunge ni mhimili wa malumbano hali inayopelekea wakati mwingine wabunge kupandwa na jazba. Kwahiyo, anahitajika mtu kama yeye ili kuweza kutuliza mambo.
Unakaribishwa kutoa mawazo yako. Unafikiri nani mwingine anafaa kushika nafasi ya uspika?