Nani anafaa kuwa man of the match kwenye game ya leo kati ya Tanzania na Uganda?

John Bocco alinikosha sana jana, kwa mavitu aliyokuwa anayafanya nilielewa kwanini kuna mashabiki huwa wanavamia uwanjani. Goli la 3 aliniacha mdomo wazi, aliupiga mwingi sana akamalizia na cross matata iliyozaa goli... kwakweli anastahili kuwa nyota wa mchezo.

Wengine Erasto Nyoni jamaa katulia sana, anacheza kwa kujiamini pasi zake ni za uhakika. Kelvin Yondani aliweza kuzuia mashambulizi yote yaliyoelekezwa upande wetu vyema, pamoja na Mbwana Samatta alituonesha vitu vya Ulaya jana hahaaaaa.

Na sisi mashabiki msitusahau jamani, tuliimba na kucheza dakika zote 90 bila kuchoka [emoji23][emoji23]


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Fei toto alinipigia pasi moja matata sana. Ghafla nilijikuta kama namuangali Andrea Pirlo
 
Nami nilikuona ulikua karibu na bashite hahaaa
 
Mkuu combination ya Nyoni na Yondani imetulia sana kule nyuma, yondani,Nyoni,Samata,Bocco,Msuva walikuwa vizuri,ila timu nzima sijaona wa kumkosoa
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilishauri siku za nyuma, nashukuru Mungu, Amunike amenisikia. Kombination ya Samatta-Msuva-Bocco inaweza kuipasua defence yoyote ya Africa. Hawa wote ni deadly strikers na wana vitu tofautitofauti sana. Kuna mabavu, kimo na nidhamu ya mchezo (Bocco), kasi na upambanaji (Msuva), na akili na ubunifu wa mpira (Samatta)

Man of the match, bila shaka ni John Rapahel Bocco. Michango mingine iliyotukuka kutoka kwa wachezaji wot walioanza isipokuwa Manula ambaye hakuwa na kazi sana golini. Alilindwa vizuri. Huree Tanzania
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…