Nani anafaidi utajiri huu wa Tanzania?

Nani anafaidi utajiri huu wa Tanzania?

Tanzania ni masikini kwa sababu ya UBINAFSI wa viongozi wetu wa ngazi za juu serikalini .

Reginald mengi ni tajiri mkubwa ni kiongozi wa serikali?
Bakhresa ni tajiri mkubwa mno ni kiongozi wa serikali?
Umaskini wa nchi wa kujitakia.Ukiwa mvivu wa kutumia fursa zilizopo eneo lako usitafute mchawi.
 
Kuna viongozi wachache wameilaanisha ardhi ya Tz
 
migodi ya dhahabu mingine imefungwa na mingne dhahabu ndio inaisha lkn bado hatujanufaika na hizo dhahabu.
 
This things got complicated...ngoja niendelee na kilimo changu cha miti na migomba
 
Ahsante kwa taarifa mkuu, ila kimoja kikubwa ulichosahau ni kwamba tanzania ina CCM iliyoikalia hii nchi kwa zaid ya miaka 50 bila lolote zaidi ya maneno mengi.
 
Mleta uzi huu, nakupongeza sana na aliye juu Mungu, akuzidishie hekima uliyonayo, sema Aamiiin!

Nimejikuta nikighadhabika baada tu ya kumaliza kusoma utajiri wa nchi hii, najiuliza mambo mengi mengi tu na kujijibu mwenyewe.

Na katika hali ya kawaida, bado kuna utajiri mwengine haujaufikia na upo naamini, ila kwa sababu raia sisi sio watu wa kufuatilia, wajanja wanapiga tu pesa kimya kimya.

Najiuliza, wale vijana wasio na kazi kipindi cha kampeni wanavalishwa nguo za rangi na kukesha juani masaa mengi, na wengine kutukana wenzao wa upande wa pili mitandaoni, tena kwa posho ndogo tu na wengine wanajiita wasomi, wanayajua haya? Wanafahamu wanayemnadi atafaidika vipi?! Najikuta nikisikitika tu!

Ahsante!
 
Wanasiasa kiukweli, wametufikisha hapa, nakumbuka ile misemo yao mingi mingi tu ya miaka ya nyuma, mfano VIJANA NI TAIFA LA KESHO, bila kutoa ufafanuzi wa ziada, ni kiaje awe Taifa la kesho? Ila miaka ya hivi karibuni wamebadili (si unajua kubembeleza kula), eti VIJANA NI TAIFA LA LEO, na bado hawafafanui.

Wanatoa mikopo vyuoni, japo wapo wanaoikosa, ila ukimaliza tu chuo na kuomba kazi, wanataka UZOEFU USIOZIDI MIAKA MITANO, hapo lazima ukose sifa na awekwe wa mlengo wao ili mrija uendelee kunyonywa.

Wa-Tanzania, tumekuwa (japo siyo wote), watu wa matukio sana, yaani utakuta wasomi wapo wapo tu, hawawi wabunifu, ila ni kila baada ya kazi, nani kasema nini na wapi, ndiyo habari hizo, mfano Raisi katangaza mshahara wake (inasemekana), yaani wengi wanam-support bila kujua hayo aloyoyataja mleta uzi atafaidika vipi nayo huyo kiongozi.

Tu wepesi sana kulaumu, kuliko kufanyia kazi yale yaliyo maovu. Tu wepesi pia kuwaamini wanasiasa bila kufikiri kwa msaada wa jicho la tatu.

Ahsante!
 
KWA WALE MSIOIJUA TANZANIA VIZURI SOMENI KWA MAKINI UTAJIRI WA TANZANIA HALAFU JIULIZE KWANINI NI MASIKINI WA MWISHO NA MALI ZOTE HIZI

1.Tz ilipata uhuru mwaka 1961 ina miaka 54 tangu ipate uhuru ikiwa ni ya kwanza Afrika Mashariki.

2.Tz Kwa miaka 38 imeongozwa na CCM peke yake ambayo ni zao la TANU na ASP.

3.Tz ni nchi ambayo haijawahi kupata majanga makubwa kama matetemeko ya ardhi, magonjwa ya mlipuko kama ebola, mafuriko na vimbunga au ukame.

4.Tz ni nchi ambayo imekuwa na kitu ambacho nchi za Afrika zimekikosa. Kitu hicho ni AMANI. Kwa miaka yote 54 ya uhuru haijawahi kupigana vita vya wenyewe kwa wenyewe.

5.Tz ina ukubwa wa 945,000 km za mraba yani sawa na uchukuwe Denmark, France, United Kingdom, Netherland, Ireland ujumlishe zote kwa pamoja.

6.Tz ina eneo la bahari lenye ukubwa wa 1,424 km. Bahari inaleta fursa za usafirishaji, uvuvi, utalii na nyinginezo.

7.Tz ni nchi ambayo imepakana na nchi za (Uganda, Rwanda, Burundi, Zambia, Malawi, D. R. Congo) ambazo zinategemea bahari yetu kwa usafirishaji wa mizigo na ni fursa nzuri ya kuzipelekea bidhaa za viwanda vyetu.

8. Tz ina maziwa makubwa manne na mengine madogo mengi.
Maziwa matatu makubwa yako kwenye kumi bora za ukubwa duniani na Maziwa makubwa matatu yote yapo Tanzania. Ziwa Victoria ni la tatu kwa ukubwa duniani (la kwanza Afrika) na ziwa Tanganyika ni la sita kwa ukubwa (la pili Afrika) na la kwanza kwa kuwa na kina kirefu duniani. Ziwa Nyasa ni la tisa kwa ukubwa duniani (ni la tatu Afrika).

9.Tz ina mito mikubwa kumi ambayo ni mto Kagera, mto Ruvuma, mto Rufiji, mto Wami, mto Malagarasi, mto Mara, mto Pangani, mto Ruaha, mto Gombe, mto Mweupe wa Nile na ina mito midogo mengi kama mto Kilombero, mto Mbemkuru n.k

10.Tz ndiyo nchi ya kwanza Afrika kuwa na maji mengi yasio na chumvi yaliyokuwa kwenye uso wa dunia (fresh surface water) kutokana na kuwa
na mito na maziwa mengi na kupitiwa na bonde la ufa.

11.Tz ni nchi ya nne kwa uzalishaji dhahabu Afrika baada ya Afrika Kusini, Ghana na Mali na ipo TOP 20 duniani. Kuna migodi nane inayochimbwa dhahabu na miwili imefungwa. Migodi inayochimbwa ni Buzwagi gold mine- (Shinyanga), Geita gold mine-(Geita), Golden pride gold mine-Nzega (Tabora), Bulyanhulu gold mine- (Shinyanga). New leuka Gold mine- (Mbeya),
Tulawaka gold mine-(Kagera), North mara gold mine-(Mara). Iliyofungwa ni Korandoto gold mine (Shinyanga), Senkenke gold mine-(Shinyanga???).

12.Tz ina madini ya almasi yanayopatikana Mwadui Shinyanga. Mgodi huo ulianza kuchimbwa tangu mwaku 1940. Mpaka leo bado unachimbwa, unamilikiwa na kampuni ya Waingereza.

13.Tz ni nchi ya kwanza na ni nchi pekee inayozalisha madini ya tanzanite duniani. Mkufu wa kuvaa shingoni unatengenezwa na tanzanite na almasi unauzwa hadi shilingi milioni 25 za Kitanzania.

14.Tz ina madini ya chuma yanayopatikana Mchuchuma, Ludewa- Njombe mgodi unamilikiwa na Wachina. Mgodi huo una hifadhi ya madini ya chuma tani milioni 122 ambayo yanawezwa kuchimbwa kwa zaidi ya miaka 100.

15.Tz ina madini ya makaa ya mawe (Coal) yanayochimbwa Kiwira Mbeya, Mchuchuma na Liganga Njombe. Unamilikiwa na Wachina. Pia mgodi wa Ngaka kule Mbinga-Ruvuma unamilikiwa na kampuni ya Tancoal ya Australia. Hifadhi ya madini ya makaa ya mawe iliyopo ni tani bilioni 2. Makaa ya mawe ndio chanzo cha pili cha umeme wa bei nafuu duniani baada ya maji.

16.Tz ina hifadhi ya madini ya Uranium kule Dodoma (Bahi) na ni mgodi ambao unamilikiwa na Warusi. Pia madini haya yanapatikana Namtumbo (Mkuju), Galapo, Minjingu, Mbulu, Simanjiro, Lake Natron, Manyoni, Songea, Tunduru, Madaba and Nachingwea.

17.Tz ni moja ya nchi tatu Afrika zikiwemo Zimbabwe na Madagascar kwa kuwa na madini mengi ya graphite. Madini haya yapo Tanga, Mahenge-Morogoro, Mererani- Manyara. Madini ya graphite ndiyo yanayotumika
kutengenezea betri za simu, kwenye injini na brake za magari na kwenye karamu za risasi (pencili).

18.Tz ina madini ya nickel yanayopatikana kule Kabanga Kagera, milima ya Uluguru-Morogoro, North Mara, Ngasoma-Mwanza.

19.Tz ni nchi ya tatu duniani kwa kuwa na hifadhi kubwa ya magadi soda duniani baada ya Marekani na Uturuki. Magadi soda hutumika kutengeneza vioo vya aina zote. Vioo vya nyumbani hadi magari pia kutengeneza sabuni na dawa mbalimbali za usafi.

20.Tz ina hifadhi na mgodi wa madini ya niobium uliopo Panda hill Mbeya ambao ndio utakuwa mgodi mkubwa wa kwanza Afrika na wa nne duniani. Mgodi huu unamilikiwa na kampuni ya Australia. Madini ya niobium ni magumu sana hutumika kutengeneza mabomba pamoja na madini chuma pia hutumika kutengeneza baadhi ya sehemu za injini za ndege na vyombo vinavyoenda nje ya uso wa dunia (mfano Apollo 15 CSM), vioo vya computer na lenzi za camera.

21.Tz ni nchi ya kwanza Afrika na ya pili duniani kwa kuwa na vivutio vingi vya utalii. Ya kwanza ni Brazil. Nchi zilizokuwa kwenye tano bora kwa utalii Afrika ni Tanzania, Botswana, Afrika Kusini, Kenya na Zambia.

22.Tz ina mbuga zipatazo 16 na ile mbuga maarufu kuliko zote duniani Serengeti ipo Tanzania, mbuga iliyopakana na bahari iitwayo Saadani ipo Tanzania na mlima mrefu kuliko wote Africa Kilimanjaro upo Tanzania.

24. Tz ina ardhi kubwa yenye rutuba na inayofaa kwa kilimo cha mazao mengi tofauti tofauti. Mashamba makubwa ya mpunga kwa mfano yaliyokuwa chini ya Shirika la NAFCO yalitoa mazao ya kulisha Tanzania na pia nchi nyingine.

24.Tz ina gesi ya asili ya Carbon Dioxide (CO2) inayovunwa kule Kyejo, Rungwe-Mbeya na kampuni ya TOL. Gesi ya asili ya cardon dioxide inatumika sana kutengenezea vinywaji laini kama soda, bia na pia kutengenezea madawa, makaratasi na kutibia maji (water treatment).

25.Tz ina gesi ya asili inayopatikana katika kisiwa cha Songo songo mkoa wa Lindi. Gesi hii imekuwa ikichimbwa na kusafirishwa hadi Dar es salaam tangu mwaka 2004. Inamilikiwa na kampuni ya Songas ya Uingereza.

26.Tz imengundua gesi ya asili yenye zaidi ya meta za ujazo trilioni 55.3 iliyongunguliwa katika maeneo ya bahari ya Hindi na Mtwara.

Pamoja na sifa zote hizi lakini Tz ni nchi iliyo kwenye kundi la nchi maskini duniani ambayo asilimia kubwa ya raia wake wanaishi chini ya Dola moja za Marekani na hali ya huduma za kijamii ikiwa duni.

TATIZO NI NINI? NANI ANAFAIDI HUU UTAJIRI? NANI WA KUMLAUMU? NANI NI SABABU?

KWA NINI TUNASHINDWA KUTUMIA HUU UTAJIRI?
Hapa muchawi ni nani???????????????????????????
Aise mimi nataka kulia
 
Ahsante kwa taarifa mkuu, ila kimoja kikubwa ulichosahau ni kwamba tanzania ina CCM iliyoikalia hii nchi kwa zaid ya miaka 50 bila lolote zaidi ya maneno mengi.


tatizo wale viherehere wa kuuliza na kuibua hoja zenye vithibitisho....
wengne ukutwa na mauti au kutolewa kucha na meno....
 
Ila nashauri njia pekee ya kujikwamua na ugumu huu wa maisha, ni kuanza kuzijenga akili zetu katika kujiajiri kibiashara, japo pia vikwazo vitakuwepo sana tu (Rejea wimbo wa Remmy Ongala - Marehemu-, uitwao Mama), utajisikia kama siyo kulia basi ni kuhuzunika.

Tuwaache wanasiasa wafanye siasa, japo tuwasimamie kwa utendaji wao na siyo kushabikia kila wanalosema, yaani watu inafikia hatua tunazisizisha akili zetu kisa tu mwanasiasa fulani mpendwa kasema nini na wapi, upande wa pili wa alichokisema hatujisumbua kuhoji bongo zetu kutupa tafsiri.

Nashukuru, binafsi sina ushabiki wa kisiasa hadi kuvaa sare zao, bali nina ushabiki wa maendeleo niyaonayo ya nchi, yaani upinzani ama ushabiki wangu upo kwenye damu na siyo nguo na kutusi wengine.

Naomba niishie hapa, nahisi ghadhabu kidogo imenishuka. Tufanye biashara zetu kihalali, kazi za halali, wanasiasa wasituchanganye.

Ahsante!
 
Mleta uzi huu, nakupongeza sana na aliye juu Mungu, akuzidishie hekima uliyonayo, sema Aamiiin!

Nimejikuta nikighadhabika baada tu ya kumaliza kusoma utajiri wa nchi hii, najiuliza mambo mengi mengi tu na kujijibu mwenyewe.

Na katika hali ya kawaida, bado kuna utajiri mwengine haujaufikia na upo naamini, ila kwa sababu raia sisi sio watu wa kufuatilia, wajanja wanapiga tu pesa kimya kimya.

Najiuliza, wale vijana wasio na kazi kipindi cha kampeni wanavalishwa nguo za rangi na kukesha juani masaa mengi, na wengine kutukana wenzao wa upande wa pili mitandaoni, tena kwa posho ndogo tu na wengine wanajiita wasomi, wanayajua haya? Wanafahamu wanayemnadi atafaidika vipi?! Najikuta nikisikitika tu!

Ahsante!
Mkuu wa tz sisi hasa vijana ndo tatizo tukipewa buku mbili tunaanza kushikana miguu
 
KWA NINI TUNASHINDWA KUTUMIA HUU UTAJIRI?

Mkuu hii mada yako nimewapa wanachuo waijadili hili ndio jibu wametoa.
Mmoja anasema jina la mleta maana ni la kihehe ambalo ni la pale Iringa.Akasema iringa ya wahehe ina fursa nyingi mno lakini wahehe ni maskini wa kutupwa.Matajiri wakubwa wa Iringa ya wahehe ni wafuatao ambao waliona kuna fursa Iringa ya Wahehe wakaona wazitumie.Matajiri wa Iringa ya wahehe ni wafuatao
1.Waarabu akina ASAS &CO
2.Wakinga
3.wachaga
4.wabena
Hata mashamba makubwa ya miti yanamilikiwa na watu toka mikoa mingine.

Akasema wahehe ni wavivu kutumia fursa zilizopo mkoani kwao.

Mleta maada labda utueleze tu huo utajiri na raslimali za huko kwenu kwa nini hamtaki kuzitumia hadi uje kuuliza nani anafaidi humu jamii forums ilitakiwa ufanye utafiti kwenu kwanza.
 
Mkuu wa tz sisi hasa vijana ndo tatizo tukipewa buku mbili tunaanza kushikana miguu


tatizo sio chama wala siasa, tatizo ni wale watawala au viongozi wanaopewa dhamana na wananchi lkn wao wanageuka kuwa mawakala wa wawekezaji nakusahau uzalendo.
 
Reginald mengi ni tajiri mkubwa ni kiongozi wa serikali?
Bakhresa ni tajiri mkubwa mno ni kiongozi wa serikali?
Umaskini wa nchi wa kujitakia.Ukiwa mvivu wa kutumia fursa zilizopo eneo lako usitafute mchawi.
Soma posts vizuri na kuzielewa kabla ya kutokwa povu, hapa.
Hao uliowataja wameingiaje kwenye uzi huu?
Kuna fursa gani Nyamongo kwa wazawa wakati watu wanaangamia kwa maji yenye sumu toka migodini?
Wengine wameuawa kwa kusingiziwa kuwa ni wezi.
Viongozi wanakwenda kuongea na wawekezaji badala ya wananchi, halafu kimyaaaa
Tanzania ni miongoni mwa nchi maskini ingawa ina utajiri wote huo ulioko mikononi mwa wageni.
 
KWA WALE MSIOIJUA TANZANIA VIZURI SOMENI KWA MAKINI UTAJIRI WA TANZANIA HALAFU JIULIZE KWANINI NI MASIKINI WA MWISHO NA MALI ZOTE HIZI

1.Tz ilipata uhuru mwaka 1961 ina miaka 54 tangu ipate uhuru ikiwa ni ya kwanza Afrika Mashariki.

2.Tz Kwa miaka 38 imeongozwa na CCM peke yake ambayo ni zao la TANU na ASP.

3.Tz ni nchi ambayo haijawahi kupata majanga makubwa kama matetemeko ya ardhi, magonjwa ya mlipuko kama ebola, mafuriko na vimbunga au ukame.

4.Tz ni nchi ambayo imekuwa na kitu ambacho nchi za Afrika zimekikosa. Kitu hicho ni AMANI. Kwa miaka yote 54 ya uhuru haijawahi kupigana vita vya wenyewe kwa wenyewe.

5.Tz ina ukubwa wa 945,000 km za mraba yani sawa na uchukuwe Denmark, France, United Kingdom, Netherland, Ireland ujumlishe zote kwa pamoja.

6.Tz ina eneo la bahari lenye ukubwa wa 1,424 km. Bahari inaleta fursa za usafirishaji, uvuvi, utalii na nyinginezo.

7.Tz ni nchi ambayo imepakana na nchi za (Uganda, Rwanda, Burundi, Zambia, Malawi, D. R. Congo) ambazo zinategemea bahari yetu kwa usafirishaji wa mizigo na ni fursa nzuri ya kuzipelekea bidhaa za viwanda vyetu.

8. Tz ina maziwa makubwa manne na mengine madogo mengi.
Maziwa matatu makubwa yako kwenye kumi bora za ukubwa duniani na Maziwa makubwa matatu yote yapo Tanzania. Ziwa Victoria ni la tatu kwa ukubwa duniani (la kwanza Afrika) na ziwa Tanganyika ni la sita kwa ukubwa (la pili Afrika) na la kwanza kwa kuwa na kina kirefu duniani. Ziwa Nyasa ni la tisa kwa ukubwa duniani (ni la tatu Afrika).

9.Tz ina mito mikubwa kumi ambayo ni mto Kagera, mto Ruvuma, mto Rufiji, mto Wami, mto Malagarasi, mto Mara, mto Pangani, mto Ruaha, mto Gombe, mto Mweupe wa Nile na ina mito midogo mengi kama mto Kilombero, mto Mbemkuru n.k

10.Tz ndiyo nchi ya kwanza Afrika kuwa na maji mengi yasio na chumvi yaliyokuwa kwenye uso wa dunia (fresh surface water) kutokana na kuwa
na mito na maziwa mengi na kupitiwa na bonde la ufa.

11.Tz ni nchi ya nne kwa uzalishaji dhahabu Afrika baada ya Afrika Kusini, Ghana na Mali na ipo TOP 20 duniani. Kuna migodi nane inayochimbwa dhahabu na miwili imefungwa. Migodi inayochimbwa ni Buzwagi gold mine- (Shinyanga), Geita gold mine-(Geita), Golden pride gold mine-Nzega (Tabora), Bulyanhulu gold mine- (Shinyanga). New leuka Gold mine- (Mbeya),
Tulawaka gold mine-(Kagera), North mara gold mine-(Mara). Iliyofungwa ni Korandoto gold mine (Shinyanga), Senkenke gold mine-(Shinyanga???).

12.Tz ina madini ya almasi yanayopatikana Mwadui Shinyanga. Mgodi huo ulianza kuchimbwa tangu mwaku 1940. Mpaka leo bado unachimbwa, unamilikiwa na kampuni ya Waingereza.

13.Tz ni nchi ya kwanza na ni nchi pekee inayozalisha madini ya tanzanite duniani. Mkufu wa kuvaa shingoni unatengenezwa na tanzanite na almasi unauzwa hadi shilingi milioni 25 za Kitanzania.

14.Tz ina madini ya chuma yanayopatikana Mchuchuma, Ludewa- Njombe mgodi unamilikiwa na Wachina. Mgodi huo una hifadhi ya madini ya chuma tani milioni 122 ambayo yanawezwa kuchimbwa kwa zaidi ya miaka 100.

15.Tz ina madini ya makaa ya mawe (Coal) yanayochimbwa Kiwira Mbeya, Mchuchuma na Liganga Njombe. Unamilikiwa na Wachina. Pia mgodi wa Ngaka kule Mbinga-Ruvuma unamilikiwa na kampuni ya Tancoal ya Australia. Hifadhi ya madini ya makaa ya mawe iliyopo ni tani bilioni 2. Makaa ya mawe ndio chanzo cha pili cha umeme wa bei nafuu duniani baada ya maji.

16.Tz ina hifadhi ya madini ya Uranium kule Dodoma (Bahi) na ni mgodi ambao unamilikiwa na Warusi. Pia madini haya yanapatikana Namtumbo (Mkuju), Galapo, Minjingu, Mbulu, Simanjiro, Lake Natron, Manyoni, Songea, Tunduru, Madaba and Nachingwea.

17.Tz ni moja ya nchi tatu Afrika zikiwemo Zimbabwe na Madagascar kwa kuwa na madini mengi ya graphite. Madini haya yapo Tanga, Mahenge-Morogoro, Mererani- Manyara. Madini ya graphite ndiyo yanayotumika
kutengenezea betri za simu, kwenye injini na brake za magari na kwenye karamu za risasi (pencili).

18.Tz ina madini ya nickel yanayopatikana kule Kabanga Kagera, milima ya Uluguru-Morogoro, North Mara, Ngasoma-Mwanza.

19.Tz ni nchi ya tatu duniani kwa kuwa na hifadhi kubwa ya magadi soda duniani baada ya Marekani na Uturuki. Magadi soda hutumika kutengeneza vioo vya aina zote. Vioo vya nyumbani hadi magari pia kutengeneza sabuni na dawa mbalimbali za usafi.

20.Tz ina hifadhi na mgodi wa madini ya niobium uliopo Panda hill Mbeya ambao ndio utakuwa mgodi mkubwa wa kwanza Afrika na wa nne duniani. Mgodi huu unamilikiwa na kampuni ya Australia. Madini ya niobium ni magumu sana hutumika kutengeneza mabomba pamoja na madini chuma pia hutumika kutengeneza baadhi ya sehemu za injini za ndege na vyombo vinavyoenda nje ya uso wa dunia (mfano Apollo 15 CSM), vioo vya computer na lenzi za camera.

21.Tz ni nchi ya kwanza Afrika na ya pili duniani kwa kuwa na vivutio vingi vya utalii. Ya kwanza ni Brazil. Nchi zilizokuwa kwenye tano bora kwa utalii Afrika ni Tanzania, Botswana, Afrika Kusini, Kenya na Zambia.

22.Tz ina mbuga zipatazo 16 na ile mbuga maarufu kuliko zote duniani Serengeti ipo Tanzania, mbuga iliyopakana na bahari iitwayo Saadani ipo Tanzania na mlima mrefu kuliko wote Africa Kilimanjaro upo Tanzania.

24. Tz ina ardhi kubwa yenye rutuba na inayofaa kwa kilimo cha mazao mengi tofauti tofauti. Mashamba makubwa ya mpunga kwa mfano yaliyokuwa chini ya Shirika la NAFCO yalitoa mazao ya kulisha Tanzania na pia nchi nyingine.

24.Tz ina gesi ya asili ya Carbon Dioxide (CO2) inayovunwa kule Kyejo, Rungwe-Mbeya na kampuni ya TOL. Gesi ya asili ya cardon dioxide inatumika sana kutengenezea vinywaji laini kama soda, bia na pia kutengenezea madawa, makaratasi na kutibia maji (water treatment).

25.Tz ina gesi ya asili inayopatikana katika kisiwa cha Songo songo mkoa wa Lindi. Gesi hii imekuwa ikichimbwa na kusafirishwa hadi Dar es salaam tangu mwaka 2004. Inamilikiwa na kampuni ya Songas ya Uingereza.

26.Tz imengundua gesi ya asili yenye zaidi ya meta za ujazo trilioni 55.3 iliyongunguliwa katika maeneo ya bahari ya Hindi na Mtwara.

Pamoja na sifa zote hizi lakini Tz ni nchi iliyo kwenye kundi la nchi maskini duniani ambayo asilimia kubwa ya raia wake wanaishi chini ya Dola moja za Marekani na hali ya huduma za kijamii ikiwa duni.

TATIZO NI NINI? NANI ANAFAIDI HUU UTAJIRI? NANI WA KUMLAUMU? NANI NI SABABU?

KWA NINI TUNASHINDWA KUTUMIA HUU UTAJIRI?
Mkuu nimesoma uzi wako hadi chozi limenitoka.nafikir vigogo wa awamu ya tatu na nne na familia zao.
 
mimi sitailaumu serikali pekee katika hili, bali pia watanzania wengi ni wavivu, hawapendi kujifunza na kujituma, ni watu wa kulalamika kila mara japokua pia serikali inazo lawama, pia sisi hatujaweza kufanya part yetu kama wananchi wazalendo
 
Back
Top Bottom