#COVID19 Nani anapaswa kupata chanjo ya COVID-19?

#COVID19 Nani anapaswa kupata chanjo ya COVID-19?

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
ChanjoWHO.png


Chanjo za COVID-19 ziko salama kwa watu wengi wenye umri wa miaka 18 na zaidi, na hata wale wenye changamoto za kiafya kama vile shinikizo la damu, ugonjwa wa kisukari, pumu, magonjwa ya mapafu, ini figo pamoja na mengineyo.

Inashauriwa kuwa endapo kuna ufinyu wa chanjo katika eneo lako, ni vema kujadili hali yako na mtoa huduma ikiwa:
  • Una kinga ya mwili iliyoathirika/dhoofika
  • Una ujamzito (ikiwa unanyonyesha, unapaswa kuendelea baada ya chanjo)
  • Una historia ya mzio (allergy), hasa kwa chanjo au viambatanishi vyake
  • Unajijua kuwa ni dhaifu sana
Watoto na vijana huwa na magonjwa ambayo si mazito na makubwa ikilinganishwa na ya watu wazima. Hivyo basi, vijana na watoto wasipokuwa sehemu ya kundi lililo katika hatari kubwa ya kupata COVID-19, hakuna uharaka sana wa kuwapa chanjo kama ilivyo kwa watu wazee, wenye matatizo sugu ya kiafya pamoja na wahudumu wa afya.

Kikundi cha Ushauri cha Wataalam wa Kimkakati (SAGE) cha Shirika la Afya duniani (WHO) kimehitimisha kuwa chanjo ya Pfizer / BionTech inafaa kutumiwa na watu wenye umri wa miaka 12 na zaidi. Watoto wenye umri kati ya miaka 12 na 15 walio katika hatari kubwa wanaweza kupewa chanjo hii pamoja na makundi mengine yanayopaswa kupewa kipaumbele kwenye chanjo.

Hata hivyo, Majaribio ya chanjo kwa watoto yanaendelea na WHO itasasisha mapendekezo yake.

Chanzo: WHO
 
WHO na chanjo za COVID 19 Mtanziko kwa walimwengu kuchanja au kutochanja
 
Back
Top Bottom