GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 7,189
- 10,375
Mwaka 2010, nilienda na rafiki yangu nyumbani kwao Usukumani. Nilishangaa nilipoamkiwa "shikamoo" na dada yake ambaye alionekana wazi anaweza akawa mkubwa kwangu. Ndivyo alivyoniamkia na ndivyo alivyomsalimia pia rafiki yangu ambaye ni ndugu yake wa damu.
Japo niliitikia, lakini ilikuwa kwa shingo upande. Sikuwa na uhakika kama nilistahili au la. Nilifikiri kakosea. Lakini siku chache baadaye, nilikuja kugundua kuwa hakusalimia kimakosa. Alijua alichokiwa anakifanya.
Alikuwa ni mkubwa kiumri kwa rafiki yangu ambaye ni ndugu yake, na alijua hilo lakini bado alimwamkia. Nilikuja kubaini kuwa kwa utamaduni wao, mwanaume ni mkubwa kwa mwanamke hata kama ni mdogo kiumri. Kwa hiyo ni kawaida kwa dada mtu kumwamkia "shikamoo" mdogo wake wa kiume.
Kwetu sisi, mkubwa ndiye anayeamkiwa hivyo.
Sijawahi kukutana na changamoto ninayotaka kushirikisha, lakini natamani kufahamu.
Inajulikana kuwa kwa tamaduni za baadhi ya makabila, ni kawaida kwa baadhi ya wazee kuoa wake zaidi ya mmoja, na wakati mwingi anaweza akaoa mwanamke anayelingana na mtoto wake wa kumzaa na hata mdogo zaidi.
Sasa chukulia, kwa mfano, baba mtu kaoa binti aliyesoma darasa moja na mtoto wake! Huyo mtoto atamsalimiaje mke mdogo wa baba yake?
Ikumbukwe kuwa mke wa baba mtu ni "mama" mtu pia.
1. Atamwita mama hata kama walikuwa marafiki shuleni na wanalingana umri?
2. Atamsalimia "shikamoo mama"?
Japo niliitikia, lakini ilikuwa kwa shingo upande. Sikuwa na uhakika kama nilistahili au la. Nilifikiri kakosea. Lakini siku chache baadaye, nilikuja kugundua kuwa hakusalimia kimakosa. Alijua alichokiwa anakifanya.
Alikuwa ni mkubwa kiumri kwa rafiki yangu ambaye ni ndugu yake, na alijua hilo lakini bado alimwamkia. Nilikuja kubaini kuwa kwa utamaduni wao, mwanaume ni mkubwa kwa mwanamke hata kama ni mdogo kiumri. Kwa hiyo ni kawaida kwa dada mtu kumwamkia "shikamoo" mdogo wake wa kiume.
Kwetu sisi, mkubwa ndiye anayeamkiwa hivyo.
Sijawahi kukutana na changamoto ninayotaka kushirikisha, lakini natamani kufahamu.
Inajulikana kuwa kwa tamaduni za baadhi ya makabila, ni kawaida kwa baadhi ya wazee kuoa wake zaidi ya mmoja, na wakati mwingi anaweza akaoa mwanamke anayelingana na mtoto wake wa kumzaa na hata mdogo zaidi.
Sasa chukulia, kwa mfano, baba mtu kaoa binti aliyesoma darasa moja na mtoto wake! Huyo mtoto atamsalimiaje mke mdogo wa baba yake?
Ikumbukwe kuwa mke wa baba mtu ni "mama" mtu pia.
1. Atamwita mama hata kama walikuwa marafiki shuleni na wanalingana umri?
2. Atamsalimia "shikamoo mama"?