Nani anayekagua na kudhibiti ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG)?

Duh, aisee, umegonga Ikulu, kwa kweli natamani hii iende hewani magazetini, kuna suala la Kikatiba hapa...nami nakupongeza sana sana
 
nadhani ulikuwa unahitaji jibu hili-ofisi yake huwa inakaguliwa na PWC.

sasa mbona matokeo ya ukaguzi ktk ofisi yake hayatolewi publicaly, nahakika hata ktk ofisi yake madudu yapo ila hatupati fursa ya kuyajua
 

Imetulia na majibu yanajitosheleza vizuri.

Naomba kuongezea kuwa ripoti zile zilikuwa zinapitia ukiritimba mwingi ili ku-neutralize sumu yake. Sina shaka uwepo wa wapinzani makini ktk hizo Kamati za kudumu za bunge umesaidia sana mabadiliko ya uwasilishaji wa ripoti za CAG.
 
Kwa wenye kujua naombeni msaada wenu. Hivi sasa anakagua 'madudu' ya akina Mhando wa TANESCO.Yeye anakaguliwa na nani? Isije ikawa yeye ndiye fisadi nambari wani...
 
Kubenea tafadhali pitia huko utupatie data kwani huenda jamaa huyu anajikagua.
 
Kwa wenye kujua naombeni msaada wenu. Hivi sasa anakagua 'madudu' ya akina Mhando wa TANESCO.Yeye anakaguliwa na nani? Isije ikawa yeye ndiye fisadi nambari wani...

Hilo nalo swali zuri si yeye tu je na makampuni mengine ya ukaguzi yanakaguliwa na nani?????
 
mkuu umenena jamaa namfahamu fisadi tu tangu kitambo hana lolote
 
Nimemwona akijigamba kwenda kukagua TANESCO - kilichotokea kwenye issue ya Jairo siwezi kumwani Utouh, wala ofisi ya CAG mpaka huyu bwana aondoke.
 
Hivi mmepata kujiuliza kwanini Blandina Nyoni wakati wake akiwa CAG ufisadi haukuwepo? wadau mnasemaje, huyu mama.... mhhh
 
nyie vipi mbona mapolisi wanajichunguza wenyewe hawaundi tume huru...na yeye ana haki ya kujikagua mwenyewe
 
Sawa na Ikerege wa TBS, kutoa vibali vya ubora lakini hakuna ofisi wala kibanda cha kukagulia.
 
nimesahau section ila CAG anatakiwa kukaguliwa kama ilivyoelezwa kwenye Public Audit Act 2008 na kwa sasa ofisi ya CAG inakaguliwa na TAC ASSOCIATES
 
Hivi mmepata kujiuliza kwanini Blandina Nyoni wakati wake akiwa CAG ufisadi haukuwepo? wadau mnasemaje, huyu mama.... mhhh
duh we mkali! Blandina Nyoni HAJAWAHI kuwa CAG...kwa mujibu wa katiba ukiwa CAG huruhusiwi kufanya kazi nyingine yeyote serikalini
 
Blandina Nyoni hakuwa Mhasibu Mkuu wa Serikali?
 
Hivi mmepata kujiuliza kwanini Blandina Nyoni wakati wake akiwa CAG ufisadi haukuwepo? wadau mnasemaje, huyu mama.... mhhh
Usichanganye mambo Nyoni hajawahi kuwa CAG. Alikuwa Accountant General. Maana yake ni Mhasibu Mkuu wa serikali.
 
Hivi mmepata kujiuliza kwanini Blandina Nyoni wakati wake akiwa CAG ufisadi haukuwepo? wadau mnasemaje, huyu mama.... mhhh
RUTAJUMBUKIRWA kwa taarifa Blandina Nyoni hakuwahi kuwa CAG; yeye alikuwa Accountant General. Swala kwamba kabla ya Uttoh hakukuwa na ufisadi si kweli tofauti iliyopo ni kuimarika kwa uhuru wa vyombo vya habari tofauti na kipindi cha Mkapa. Tofauti na huko nyuma, siku hizi taarifa ya CAG huwekwa hadharani na hata kamati za kudumu za hesabu za Serikali Kuu, Serikali za mitaa na Mashirika ya umma zimeanza kuongozwa na wapinzani awamu hii ya Kikwete (Kazi nzuri ya Hon. Samweli Sitta) hivyo kupunguza uoga uliokuwepo wa kuhoji matumizi ya serikali na taasisi zake.
 
Last edited by a moderator:
Hilo nalo swali zuri si yeye tu je na makampuni mengine ya ukaguzi yanakaguliwa na nani?????
Lu-ma-ga kampuni za ukaguzi zinawajibika kuwasilisha hesabu zilizokaguliwa TRA kwa mujibu wa Sheria ya Mapato ya mwaka 2004 kama mapato yanazidi 20 million. Vile vile zinawajibika kujiwekea utaratibu wa kupitia ubora wa kazi zao (Cold review) na vile vile kukaguliwa na "regulator" kwa kile kinachoitwa Audit Quality Review (AQR). Kwa maana ingine kazi ya ukaguzi inayofanywa na kampuni ya ukaguzi inaweza kupitiwa na mtu mwingine katika zoezi la Audit Quality Review.
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…