Nani aniuzie simu kwa bei ya jumla

Nani aniuzie simu kwa bei ya jumla

Joel360

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2013
Posts
986
Reaction score
657
Habari zenu wana jukwaa la Biashara.

Nasafiri naenda Mbeya. Wilaya ninayokwenda hakuna maduka makubwa ya simu kama Kariakoo, ila watu wanapenda sana hizi smartphone.

Sasa natafuta muuzaji wa simu ambae ataniuzia simu kwa bei nafuu (bei ya jumla). Nataka ninunue simu mbili tu kabla sijasafiri ili nikauze kule. Na kama nikipata wateja haraka basi nitamtuma binamu yangu (yupo Kigogo) anunue nyingine mbili kutoka kwa huyo muuzaji kisha anitumie kupitia basi.

Kama utanitajia namba yako au utanitajia simu ulizonazo au utanitajia page yako ya mitandao ya kijamii ili nikazione itakuwa vizuri. Ila tu bei yako ikiwa nzuri itakuwa vizuri ili nami nikapate hela ya chai na sukari huko nnakoenda.
 
Njoo WhatsApp
0766473551
IMG-20220215-WA0065.jpg
IMG-20220215-WA0068.jpg
 
Back
Top Bottom