Nani awe kiongozi wa wanawake, Halima bint Khamis au Titi Mohamed?

Nani awe kiongozi wa wanawake, Halima bint Khamis au Titi Mohamed?

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
KHALIMA BINT KHAMISI MMOJA WA WANAWAKE MSTARI WA MBELE KATIKA KUPIGANIA UHURU WA TANGANYIKA 1954

Kumbukumbu za wazalendo mfano wa Bi. Halima bint Khamis hazipo popote hata ukienda ofisi ya CCM Lumumba Avenue hutaona picha yake katika kuta wala hutaona picha ya yeyote katika wale waliopigania uhuru wa Tanganyika.

Bi. Halima Khamis kwao ni Bagamoyo na kabila yake Mmanyema. Halima Khamis ni mmoja kati ya wengi wazalendo waliofukiwa na historia.

Nimehudhuria shughuli za wanawake kwa kualikwa kama mzungumzaji nimekuta picha zilizowekwa kupamba ukumbi ni za akina mama wengine wengi tu.

Napitia picha moja baada ya nyingine kwa kutegemea labda nitaona picha ya Halima Khamis, Tatu bint Mzee, Hawa bint Maftah, Zarula bint Abdulrahman, Shariffa bint Mzee, Fatma bint Matola, Nyange bint Chande, Amina, Kinabo, Mama bint Mwalimu, Halima Selengia...

Anaeoneka katika picha hizi ni Bibi Titi Mohamed peke yake. Kuta zote zimejaa wazalendo akina mama wapya wa leo.

Kwa nini iwe hivi?
Hiyo picha hapo juu ni Bi. Halima Khamis akisalimiana na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mbele ya Ukumbi wa Diamond.

Bi. Halima na Mwalimu Nyerere walikuwa hawajaonana kwa miaka mingi sana. Wanasema ile nafasi ya Bibi Titi ilikuwa ama achukue Bibi Titi au Halima Khamis kwani vipaji vyao vikilingana kwa karibu sana.

Bahati ilimwangukia Bibi Titi.

Wakati ule wa harakati miaka ya 1950 Halima Khamisi alikuwa msichana mdogo chini ya miaka 30 akisomesha watoto Qur'an kwenye madrasa yake mwenyewe Mtaa wa Kariakoo na Livingstone si mbali na ofisi ya TANU Mtaa wa New Street na Kariakoo.

Hawa ndiyo wale akina mama wa mabaibui waliotajwa na Mama Maria Nyerere waliopigania uhuru wa Tanganyika.

1718426380064.png

Bi Halima Khamis
1718426487531.png

Bibi Titi Mohamed
 
Fikiria unaingia ofisi ya CCM Lumumba Avenue na unaona picha hizo hapo chini kwenye kuta zake.

Fikiria unaingia kwenye ukumbi wa shughuli yoyote ile ya akina mama na unakuta picha kama hizi zimewekwa.
 
Fikiria unaingia ofisi ya CCM Lumumba Avenue na unaona picha hizo hapo chini kwenye kuta zake.

Fikiria unaingia kwenye ukumbi wa shughuli yoyote ile ya akina mama na unakuta picha kama hizi zimewekwa.
Halima Khamisi alikuwa msichana mdogo chini ya miaka 30 akisomesha watoto Qur'an kwenye madrasa yake mwenyewe🤣😂😆
 
Halima Khamisi alikuwa msichana mdogo chini ya miaka 30 akisomesha watoto Qur'an kwenye madrasa yake mwenyewe🤣😂😆
Salari...
Hakika Halima Khamis hiyo ni moja ya sifa zake.
Mwalimu wa madrasa.

Akienda kuhudhuria mikutano ya TANU amevaa baibui.

Hii ndiyo historia yetu.
Angalia picha hizo hapo chini:

1718445048273.jpeg

Mkutano wa TANU 1950s
Angalia kushoto kwenye picha kuna sehemu kuwa weusi mtupu.
Hiyo ilikuwa sehemu wanakokaa wanawake katika mikutano ya TANU Mnazi Mmoja na huo weusi ni mabaibui.​

1718444587018.png

Salari,
Ikiwa wewe historia hii inakutaabisha hiyo ni bahati mbaya sana kwako.
Mimi hii ni historia ya bibi, mama na shangazi zangu.

Najua mchango wao katika kupigania uhuru wa Tanganyika na naiandika na shingo nimetoa kwa kuwa ni historia ambayo mimi najivunia kwayo.

Historia hii haikuwapo.
Nimeirejesha na ndiyo hii leo inasomwa hapa JF Jukwaa la Historia.
 
Dini dini dini dini
Kaa...
Naam.
Uislam, Uislam, Uislam na Uislam.
Huwezi kuuweka mbali na harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Mikutano ya mwanzo ya TANU Mnazi Mmoja ikifunguliwa kwa dua.
Baada ya harakati kuanza kila tatizo lililojitokeza TANU ilifanya dua.

Dua ya kwanza ilikuwa ya kumuoombea Rashid Ali Meli.
Rashid Ali Meli alitoa fedha za serikali akampa Idd Faiz Mafungo Mweka Hazina wa TANU atie kwenye mfuko wa safari ya Nyerere UNO 1955 awahi kikao na haraka fedha arejeshewe 1955.

Rashid Ali Meli alikuwa Bwana Fedha, Dar es Salaam Municipal Council.

Dua ya pili alifanyiwa Abdulwahid Sykes yeye alikutwa na Town Clerk Mzungu akiwa na kadi za TANU akiuza Kariakoo Market 1955.

Abdul Sykes alikuwa Market Master.
Ilihofiwa Abdul Sykes atafukuzwa kazi.

Dua ya tatu alisomewa Nyerere Lindi nyumbani kwa Suleiman Masudi Mnonji muasisi wa TANU Southern Province mwaka wa 1955.

Dua ya kumuombea Nyerere na TANU salama.

Dua ya nne nyumbani kwa Jumbe Tambaza, Upanga kumuombea Nyerere ashinde njama za Gavana Edward Francis Twining.

Dua ya tano Mnyanjani.

Dua ya kuiombea TANU na Nyerere ushindi katika sakata la Kura Tatu chama kilipokuwa kinakabiliwa na hatari ya kusambaratika kuhusu kukubaliana na masharti ya upigaji kura na kugombea nafasi 1958.

Hii ndiyo historia yetu.
Uislam, Uislam Uislam, Uislam wewe unaita udini, udini, udini, udin.

Sasa ndugu yangu tufanyeje?
Tupeleke mswada wa sheria Bungeni kupiga marufuku historia hii?

Fikiria unaingia ofisi ya CCM Lumumba Avenue na unaona picha za wazalendo hawa kwenye kuta zake.

Angalia video hiyo hapo chini:

 
Hua wanaweka picha za akina nani?
Mpaji...
Kulia wa kwanza ni Chiku bint Said Kisusa, Bibi Titi Mohamed.

Kushoto wa kwanza ni Tatu bint Mzee na huyo katikati ni Julius Nyerere wanamsindikiza Uwaja wa Ndege Dar es Salaam safari ya kwanza UNO 1955.
 
Back
Top Bottom