Nani kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar baada ya kifo cha Maalim Seif Sharif Hamad?

hivyo ndivo ilivyo, Hussein Mwinyi kwa njia alizoanza nazo kujaribu kuenda na siasa za usawa ni wazi kuwa asingeweza kushinda uchaguzi ujao bila ya kupata support ya ACT kimakubaliano, bila ya hivo atalazimika kurejesha vurugu za nyuma.
 
Jussa nadhani bilashaka.. Kama hakulainika na kipondo kile, huu ni wakati wake kujipambanua.

BACK TANGANYIKA
 
ukisoma comment za wachangiaji juu ya maalim na uamuzi wake halafu ukaamua kufanya ziara ndogo mitaani unakutana na dunia tofauti...

Hao waliokua wakipiga kelele maalim kasaliti ni wahuni wa JF na twitter, wafuasi wa Maalim hawajawahi kutetereka.
 
huyo Hamad Masoud hafai mkuu, Na siamini kama anaweza kuwemo hata katika watakaopendekezwa.
Juma Duni Haji nadhani experience na age,vitam favour achaguliwe, Mansour anapendwa ila Mwinyi hawezi kumuweka kijana mwenzie kwenye ile position kwa sababu anahitaji mtu wa makamo kuliko yeye na mwenye uzoefu mkubwa wa siasa.
 

Anayefaa kuchukua nafasi ya Maalim ni Mhe Juma Duni Haji, no hullabaloo!
 
Jussa anafaa zaidi ili kuleta mawazo mbadala chanya kulingana na mahitaji ya kizazi cha sasa. Hata Maalim Seif(RIP) alianza kuaminiwa akiwa bado kijana ndio maana ameweza kuhimili mikikimikiki ya siasa kwa weledi mkubwa. Hivyo ikiwapendeza wana ACT na Mh. Rais wanaweza kupata mchango mkubwa wa mawazo na fikra pevu mbadala kwa maendeleo ya Wazanzibari wote.
 
A person needed is from PEMBA unless otherwise
 
Nadhani hauko sawa. Katiba yao inatambua nafasi ya makamu wa kwanza wa Raisi na kwamba atatoka kwenye chama kilichopata angalau asilimia kumi ya kura kwenye uchaguzi mkuu. Na chama kilichopata ushindi kina nafasi ya kutoa makamu wa pili wa Rais.

Kwa mantiki hii, ACT Wazalendo ndicho chama kilichokidhi hili takwa la kikatiba, kilipata zaidi ya asilimia kumi, na ndiyo maana kilipewa nafasi ya kupendekeza jina la Makamu wa kwanza wa Rais, na Maalim Seif (RIP) akapendekezwa na chama chake, na hatimaye kuapishwa na kuwa makamu wa kwanza wa Raisi wa SMZ.

Nafasi hii ni yao (ACT), kwa vile Maalimu Seif katutoka, ACT watapeleka jina la mwanachama mwingine - Mzanzibari kujaza nafasi ya Maalim baada ya muda utakaporuhusu kikatiba, na si vinginevyo. Hivyo ndo ninavyojua mimi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…