Nani mbabe: Black Mamba vs King Cobra

Nani mbabe: Black Mamba vs King Cobra

mwambie huyo anayeongoza ni kifutu ( puffer adder)

Sababu wanapatika maeneo mengi

Wanakaga kimpya.

Nirahisi kuchangamana na watu.
Kifutu mstaarabu sana.. mpaka umchokoze ndio anakushambulia, anaweza kaa pembeni yako hata saa zima na usijue kama yupo ila usijitingishe ukamgusa
 
Hebu tujaribu kidogo kuwachambua hawa wababe wawili kisha tujue ikiwa watakutana nani atakuwa zaidi??

Black mamba na King cobra ni moja ya jamii hatari zaidi za nyoka duniani na maarufu hata kimuonekano kutokana na upekee wa maumbo yao.

BLACK MAMBA: Nyoka anaejulikana kwa kuua sana duniani na mwenye kasi zaidi kuliko nyoka wote ardhini.

  • Makabila mbalimbali ya kiafrika yanatumia utambulisho wake kama alama zao na wengine kumuabudu kama mlinzi na mungu wao katika maeneo yao.
  • Ameripotiwa kusababisa vifo vya maelfu ya watu kila mwaka.
  • Wakorofi na wako tayari kung'ata mara nyingi iwezekanavyo pale inapombidi kufanya hivyo kutokana na tishio la adui.
  • Kwa sababu hii wanahesabika kama TOP KILLER kati ya nyoka wote wanaotambaa ardhini. Karibia watu 20,000 kila mwaka wanakufa kwa kugongwa na nyoka huyu.
  • Wanapatikana zaidi hasa Afrika maeneo ya central na east Afrika.
UREFU
-Kwa black mamba aliyekuwa na kukomaa anaweza fikia urefu wa 6.6 - 8.2 feet (2 - 2.5m)

-Urefu wa meno ni 0.25 inches (6.5mm)

SPEED/KASI

-12.5 m/h (20km/h). Mara nyingi hutumia kasi yake kukimbia hatari kuliko kuwindia.

UZITO

-1.6 Kg

MUONEKANO NA RANGI

Black mamba huwa warefu pia wembamba. Wanapatikana kwa rangi ya kijivu au brown mbichi (light brown)

CHAKULA/DIET

• Wanyama wadogo na ndege.
*Imewahi kulipotiwa kukutwa kasuku wazima na hata Cobra wakubwa kwenye tumbo la Black mamba.

ATTACK NA UWINDAJI

- Wanapopata windo husubiri kwanza windo lake kuparalyze au kufa kutokana na sumu aliyowatia kupitia meno yake, ndipo huwa muda mahususi kwa kumla.
-Kawaida huchukua muda mchache sana kwa windo lake kufa baada ya kung'atwa na humeza windo lake kama lilivyo.
- Wana taya laini kujitegua ili kufit chakula mdomoni hata mara 4 ya saizi ya kichwa chake.

TABIA

• Ni wakazi wa eneo moja. Wanatoka asubuhi na baadae tena jioni kwa ajili ya kuwinda ama kupumzika nje kisha kurudi eneo lao.
• Ni waoga lakini hurudisha attack pale inapowalazimu na kukimbilia katika kichaka au shimo .


KING COBRA: Ni kati ya nyoka wakubwa na hatari zaidi duniani. King cobra hupatikana hasa Southeast Asia na India

  • Anapokutana na tishio hutumia ngozi yake karibu na kichwa kuitanua ili kuinekana hatari. Alama nyeusi nyeusi zilizopo katika hood yake hutishia baadhi ya wanyama wakali wanapokuwa karibu nae.
• Anauwezo wa kunyanyua 3/4 ya mwili wake toka ardhini huku kumfuata adui yake kwa lengo moja tu ( kuattack).

UREFU

-10 to 12 feet (3.3m) lakini wengine wanaweza kufikia mpaka 5.4 m.

UZITO

- 6Kg.

RANGI NA MUONEKANO

-King cobra waliokomaa wapo wa rangi nyeusi, light yellow, kijani na brown. King cobra ni mnene kidogo kuliko black mamba.

CHAKULA/DIET

-King cobra wanajulikana kama '' OPHIOPHAGONS" yaani snake eater. Anauwezo wa kula hata nyoka wenzake wenye sumu.
- Mlo pendwa ni pamoja na jamii za panya, mijusi, ndege na hata nyoka wengine kama chatu, cobra, jamii za vipers n.k.
-Mlo unapopatikana vizuri anaweza kukaa hata mwezi kutokana na mmeng'enyo chakula wake wa taratibu.

ATTACK NA UWINDAJI

-Anawinda kwa kutumia kemikali inayogundua haruru ya windo lilipo hata zaidi ya umbali wa mita 100 toka alipo.
- Sumu yake hatari inaweza kumpa paralyze na kumuua kabisa tembo ndani ya masaa 3 tu toka amng'ate iwe mguuni au kwenye mkonga.

TABIA

- Hawana eneo maalumu kuishi.
-King cobra hukutana pale tu wanapotaka ku-mate na jinsia nyingine.
-Wako active muda wote wa siku.
-Hupendelea kukimbia hatari au kuattack anapomlazimika.

====> Nini tofauti yao kubwa endapo mmoja wao atakutana na mwingine?

BLACK MAMBA


A)Hatari ila anatabirika. Yupo tayari kupigana au akimbie kujiokoa
B) Kwa kila ng'ato humuachia adui kiasi cha 55 mg za sumu mwilini.

KING COBRA

A)Hatari na hatabiriki, anajiamini na kuattack kwa mahesabu.
B)Anaacha kiasi kikubwa cha sumu 420 mg; mwilini kwa adui kwa mng'ato mmoja.
C) Imethibitishwa kuwa king cobra ndie nyoka anaetumia akili sana kabla ya kuattack.

HITIMISHO:
~Black mamba akikutana na king cobra; ajitahidi kupigana ashinde au akimbie.

~King cobra akikutana na black mamba; kwanza kakutana na chakula au apigwe na afe.

MSHINDI: King cobra[emoji1628]
Mkuu.. kuwa na heshima na koboko aisee.. na kuna sifa yake moja umeisahau, anapenda bangi kupita maelezo
 
Mbona kuna sifa za Koboko umehamishia kwa Cobra. Jaribu kuhariri andiko lako.!
Watafiti mbalimbali wanasema bora ukutane na Simba porini na sio Black Mamba.! Unajua ‘Kiss of Death’?!
Usiombe kujaribu.
Analeta utani na koboko.. kile kiumbe [emoji119]
 
Hii tabia na michezo ya nyoka huwa zinatokea wapi jamani
 
Black mamba ni habari nyingine yanii.. huyo nyoka sio wa utani wengine mpaka uwachokoze ndo wanakudhuru huyu vita ni vita yanii akikuona tu unalooo... 🤣 🤣 🤣 🤣 anakufata hadi kwako yanii
 
Kwa nyama tamu Black Mamba ana nyama tamu zaidi na laini..mimi hupenda hii ya Black Mamba. Na supu yake ni nzuri kwa kuongezea ngumu za kiume. Unachemsha na tangawizi unakunywa kijiko kimoja kwa gram 50 za nyama chemsha na maji nusu lita na kipande cha tangawizi kilichosagwa kijiko kidogo. Utanambia.

Tahadhali : usinywe kama huna uhakika wa kupata mademu wasiopungua watatu siku husika.
 
Jf ni jukwaa Huru!
Hivyo kila mtu ana uhuru wa Kuchangia...

Ila sio kwa uchangiaji huu,Mambo mengine tujaribu kuwa watu wazima kidogo.

Mada inamaanisha nini,vipi na wewe unamaanisha nini sasa.
ili nibidi nicheke tu maana hamna namna
 
Hebu tujaribu kidogo kuwachambua hawa wababe wawili kisha tujue ikiwa watakutana nani atakuwa zaidi??

Black mamba na King cobra ni moja ya jamii hatari zaidi za nyoka duniani na maarufu hata kimuonekano kutokana na upekee wa maumbo yao.

BLACK MAMBA: Nyoka anaejulikana kwa kuua sana duniani na mwenye kasi zaidi kuliko nyoka wote ardhini.

  • Makabila mbalimbali ya kiafrika yanatumia utambulisho wake kama alama zao na wengine kumuabudu kama mlinzi na mungu wao katika maeneo yao.
  • Ameripotiwa kusababisa vifo vya maelfu ya watu kila mwaka.
  • Wakorofi na wako tayari kung'ata mara nyingi iwezekanavyo pale inapombidi kufanya hivyo kutokana na tishio la adui.
  • Kwa sababu hii wanahesabika kama TOP KILLER kati ya nyoka wote wanaotambaa ardhini. Karibia watu 20,000 kila mwaka wanakufa kwa kugongwa na nyoka huyu.
  • Wanapatikana zaidi hasa Afrika maeneo ya central na east Afrika.
UREFU
-Kwa black mamba aliyekuwa na kukomaa anaweza fikia urefu wa 6.6 - 8.2 feet (2 - 2.5m)

-Urefu wa meno ni 0.25 inches (6.5mm)

SPEED/KASI

-12.5 m/h (20km/h). Mara nyingi hutumia kasi yake kukimbia hatari kuliko kuwindia.

UZITO

-1.6 Kg

MUONEKANO NA RANGI

Black mamba huwa warefu pia wembamba. Wanapatikana kwa rangi ya kijivu au brown mbichi (light brown)

CHAKULA/DIET

• Wanyama wadogo na ndege.
*Imewahi kulipotiwa kukutwa kasuku wazima na hata Cobra wakubwa kwenye tumbo la Black mamba.

ATTACK NA UWINDAJI

- Wanapopata windo husubiri kwanza windo lake kuparalyze au kufa kutokana na sumu aliyowatia kupitia meno yake, ndipo huwa muda mahususi kwa kumla.
-Kawaida huchukua muda mchache sana kwa windo lake kufa baada ya kung'atwa na humeza windo lake kama lilivyo.
- Wana taya laini kujitegua ili kufit chakula mdomoni hata mara 4 ya saizi ya kichwa chake.

TABIA

• Ni wakazi wa eneo moja. Wanatoka asubuhi na baadae tena jioni kwa ajili ya kuwinda ama kupumzika nje kisha kurudi eneo lao.
• Ni waoga lakini hurudisha attack pale inapowalazimu na kukimbilia katika kichaka au shimo .


KING COBRA: Ni kati ya nyoka wakubwa na hatari zaidi duniani. King cobra hupatikana hasa Southeast Asia na India

  • Anapokutana na tishio hutumia ngozi yake karibu na kichwa kuitanua ili kuinekana hatari. Alama nyeusi nyeusi zilizopo katika hood yake hutishia baadhi ya wanyama wakali wanapokuwa karibu nae.
• Anauwezo wa kunyanyua 3/4 ya mwili wake toka ardhini huku kumfuata adui yake kwa lengo moja tu ( kuattack).

UREFU

-10 to 12 feet (3.3m) lakini wengine wanaweza kufikia mpaka 5.4 m.

UZITO

- 6Kg.

RANGI NA MUONEKANO

-King cobra waliokomaa wapo wa rangi nyeusi, light yellow, kijani na brown. King cobra ni mnene kidogo kuliko black mamba.

CHAKULA/DIET

-King cobra wanajulikana kama '' OPHIOPHAGONS" yaani snake eater. Anauwezo wa kula hata nyoka wenzake wenye sumu.
- Mlo pendwa ni pamoja na jamii za panya, mijusi, ndege na hata nyoka wengine kama chatu, cobra, jamii za vipers n.k.
-Mlo unapopatikana vizuri anaweza kukaa hata mwezi kutokana na mmeng'enyo chakula wake wa taratibu.

ATTACK NA UWINDAJI

-Anawinda kwa kutumia kemikali inayogundua haruru ya windo lilipo hata zaidi ya umbali wa mita 100 toka alipo.
- Sumu yake hatari inaweza kumpa paralyze na kumuua kabisa tembo ndani ya masaa 3 tu toka amng'ate iwe mguuni au kwenye mkonga.

TABIA

- Hawana eneo maalumu kuishi.
-King cobra hukutana pale tu wanapotaka ku-mate na jinsia nyingine.
-Wako active muda wote wa siku.
-Hupendelea kukimbia hatari au kuattack anapomlazimika.

====> Nini tofauti yao kubwa endapo mmoja wao atakutana na mwingine?

BLACK MAMBA


A)Hatari ila anatabirika. Yupo tayari kupigana au akimbie kujiokoa
B) Kwa kila ng'ato humuachia adui kiasi cha 55 mg za sumu mwilini.

KING COBRA

A)Hatari na hatabiriki, anajiamini na kuattack kwa mahesabu.
B)Anaacha kiasi kikubwa cha sumu 420 mg; mwilini kwa adui kwa mng'ato mmoja.
C) Imethibitishwa kuwa king cobra ndie nyoka anaetumia akili sana kabla ya kuattack.

HITIMISHO:
~Black mamba akikutana na king cobra; ajitahidi kupigana ashinde au akimbie.

~King cobra akikutana na black mamba; kwanza kakutana na chakula au apigwe na afe.

MSHINDI: King cobra🥇
Mbona unakuwa kama msomali wa Tanzania football failure.ushindanishe wewe na utoe ubingwa wewe
 
Mtoa mada nakusahihisha kidogo,nyoka anaeongoza kuua watu wengi si black mamba,sababu nyoka huyo mara nyingi hukimbia watu.
Nyoka anaeongoza kwa kuua watu wengi ni nyoka anaeitwa saw scaled viper,jina lake maarufu jingine ni carpet viper jina la kisayansi anaitwa echis carinatus. Kwa mujibu wa tovuti ya britannica.com,nyoka huyo ameua idadi kubwa ya watu ambayo inafidia ukijumlisha idadi ya watu waliouwawa na aina nyingine zote za nyoka.
Huyo carpet viper ni noma,naomba kama kuna mtu anlijua jina lake kwa kiswahili atuambie.
 
Mkuu usije ukajichanganya na black mamba. Hawa sumu yao ni deadly sana! Be careful. Cobra most of the time anatema mate, na mate yake ni hatari zaidi yakikufikia machoni. Ukiwahi kunawa kwa maji mengi na sabuni asilimia za kupona ni kubwa na hautapofuka. Black mamba akikugonga usikawie zaidi ya nusu saa (nadhani ni dakika 20) bila kufika hospitali UTAKUFA! Usione hizo mils 55 ukazidharau, ni hatari sana kuliko 400 za cobra

Nimekuonya!
Unamuongelea swira mkuu
 


mada ni wakikutana yupi atasanda??

black mamba ni nyoka hatari sana kwa viumbe wengine,ila sio huyo mwenzao wa kuitwa king cobra.
king cobra ndiye nyoka anayekamata na kumeza nyoka wengine.
kwa aina hiyo ya maisha ni dhahiri amepewa kinga ya sumu kama alivyo nyegere,nguchiro na kenge wanaokula nyoka pia.
 
King Mufasa Mbona kuna sifa za Koboko umehamishia kwa Cobra. Jaribu kuhariri andiko lako.!
Watafiti mbalimbali wanasema bora ukutane na Simba porini na sio Black Mamba.! Unajua ‘Kiss of Death’?!
Usiombe kujaribu.
Nilivyoelewa ni kwamba Hii Jamaa imejikita kupambanisha wao kwa wao na si wao against sisi binadamu

Ila ukiwapambanisha na binadamu ni bora mara 10 ukutane na Black mamba kuliko Cobra.
 
Kuna tofauti kati ya swila na black mamba/Green mamba mkuu?
Swila anavimba kama cobra ila sio cobra yeye siraha yake ni mate , king cobra muache kabisa kwanza mwili wake unazalisha kinga dhidi ya sumu zote nyoka including cobra themselves
Wakipigana cobra na koboko koboko analiwa alfajiri tu ila wewe kama wewe ukiambiwa ukutanishwe na mmoja wao chagua kukutana na kobra sio koboko, koboko ni hatari na hana mpinzani kwa hio tasnia
 
Kuna kipindi flani kinaoneshwaga Nat Geography mwamba akienda kutoa nyoka akimkuta black mamba yaani anakuwa seriously mpk jasho linamtoka ila Cobra sio kivile
Simon Keys Na mkewe Siouxie hahahaaa
 
Black mamba vs king cobra apa kombe tunampa king cobra... lakini wote wawili wakipambana na viumbe wengine aiseee black mamba sio wa mchezo mchezo kabisa
 
Black Mamba ni hatari zaidi
Hatari akikabiliana na Nani? King Cobra au Binadamu

Vs Binadamu mbona Koboko/Black Mamba mbona hana noma ni mpaka umchokoze ndio anakuwa hatari.....

Lkn Usiombe Ukutane Na King Cobra uyu kwanza by nature tu ni Mbabe na ni Mkorofi atakushambulia bila hata kuanza kumchokoza
 
Back
Top Bottom