Nani Mkubwa kati ya Mkuu wa Majeshi na Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa?

Mmoja anaitwa Mkurugenzi wa usalama mwingine anaitwa mkuu wa vikosi vya ulinzi na usalama.

Unafikiri Nani mkubwa? Uliwahi kuona Rais akimbatana DGIS kwenye hafla yeyote rasmi mfano ukaguzi wa gwaride.... Na mengine.

Bettle na Scania yote ni magari Yana kazi tofauti lakini mmoja linawwza kumbeba mwingine Ila mbebwaji hawezi kumbeba mwengine
 
Kiseniority utaratibu ni kuwa

Jeshi
POlisi
USalama
Na majeshi mengine yanakuja chini.

Mkuu wa majeshi ndio mkuu wao.

Kikubwa ni kuwa usalama wameata ile mamlaka ya kuwa karibu na raisi kuliko polisi au jeshi.

Kama ambavyo polisi wamepewa mamlaka ya kukagua vyombo na kushtaki dhidi ya vyombo vingine,mamlaka ya kushughulikia shida za wananchi katika kesi zao kinyume na jeshi n.k

Hivyo kuna mgawanyiko wa madaraka na majukumu kwa vyombo vya usalama.
 
Mbona Mara nyingi meko alikuwa anasafiri na Diwani

Sent from my TECNO B1f using JamiiForums mobile app
 
Sio kweli, mmoja Ni Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa na mwingine Ni Mkuu wa majeshi ya Ulinzi.
Vyombo vya Usalama vina wakuu wao lakini ukifuata Protocol hao wengine hawana cheo Cha General ndio maana wengine Ni makamishina huku Ni mabrigedia nk.
Hivyo inapelekea yeye kuwa wakwanza kimadaraka lakini sio kwamba anawaongoza kimajukumu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…