Uchaguzi 2020 Nani mkweli kati ya hawa watu? Spika, NEC au CHADEMA?

Sidhani kama ni sahihi kuwaweka Chadema kwenye kundi moja na hizo taasisi 2 ulizozitaja.

Chadema washatoa ushahidi kuwa hawakupeleka majina na kama yamepelekwa ni kwa njia ya jinai. Wanataka jinai ichunguzwe na vyombo husika. Vyombo vimepiga kimya.
Chadema wamesha play part yao. The ball is out of their court.

NEC na Bunge wanahitajika sasa ku authenticate maamuzi yao. Bado hawajafanya hivyo.
The ball is now in these 2 institutions' courts.
 
NEC hawana haja ya kufanya anything
Nyie ubunge hamuutaki na wakina Mdee mmshawafukuza Sasa mnatumia nguvu yote ya kazi gani
 
Then wao wanapata faida gani ikiwa huo ubunge hawautaki?

Wanatakiwa kuwa wazi tu kuwa Hao waliokwenda sio waliopelekwa tume ya uchaguzi
Kwa hiyo wataka CHADEMA wawe wazi mara ngapi? Kwa namna gani zaidi ?
 
Nec wanasema walipokea majina toka Cdm, spika anadai alipokea majina,akafanya kazi ya kuapisha. Nini kinachofuata?
 
Chadema wanaenda kufanyaje mahakamani ,wao kazi yao wameshamaliza kuwafuta uanachama na NEC itangaze siyo wabunge halali maana hawana chama
 
Binafsi, kwa kweli sifahamu CHADEMA wataenda mahakamani kufanya nini, yaani kufungua shauri gani hasa...

Kwa sababu wao kama chama, wamejiridhisha bila shaka yoyote kuwa utaratibu wa kichama ulikiukwa ktk uteuzi wa wabunge hao (hawakuteuliwa bali walijiteua wenyewe)....

Na CHADEMA kama chama wamechukua hatua kwa mujibu wa kanuni, sheria na katiba yao ya chama chao...

In my opinion, wanaopaswa kwenda mahakamani ni waliochukuliwa hatua yaani Halima Mdee na wenzake kama wanadhani wameonewa...

Otherwise mpaka hapo CHADEMA hawana business wala ushirika na hao kinamama waliokuwa wanachama wao unless otherwise....

Labda, CHADEMA kwa kuwa kuna dalili za jinai (forgery) ndani ya jambo hili, wanaloweza kufanya ni kuchukua hatua za kisheria kwa wote walioghushi nyaraka ikiwemo muhitasari wa kinachodaiwa kikao cha KK kujadili na kupitisha majina hayo na sahihi ya katibu mkuu...

Ishu ya hao kinamama wabaki kuwa wabunge au la si ya CHADEMA tena bali ni kila mtu ukiwemo wewe na mamlaka husika kuangalia na kuzingatia miongozo, kanuni, sheria na Katiba ya nchi zinasemaje juu ya ubunge wa hawa kinamama...
 
Nec wanasema walipokea majina toka Cdm, spika anadai alipokea majina,akafanya kazi ya kuapisha. Nini kinachofuata?
Spika athibitishe uhalali wa mchakato uliofuatwa kuyapata hayo majina.
 
kwani akaunti nyingine huwa zinatumiwa na watu wenye mawazo kulingana na msimu au huwa ni majukumu mahususi
 
Watu wanajua Spika wa CCM ana file milembe...hao NEC ndiyo kabisa wameboronda balaa..makaratasi mtaani kama mabaki ya bigijii...

Mkweli ni chama cha wananchi....chama makini...ever..uwe hutaki ama unataka ila ukweli ndiyo huo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…