Nani mwenye ujasiri wa kusahihisha kauli ya Mwalimu Nyerere katika historia ya TANU?

Nani mwenye ujasiri wa kusahihisha kauli ya Mwalimu Nyerere katika historia ya TANU?

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
WASIFU WA JULIUS NYERERE: NANI ATAKUWA NA UJASIRI WA KUISAHIHISHA KAULI YA MWALIMU PALE ALIPOKOSEA TAARIFA KATIKA HISTORIA YA TANU NA MAISHA YAKE MWENYEWE?

Nasoma kitabu cha historia ya Mwalimu Nyerere na kuna mengi nimejifunza ambayo kwa hakika nilikuwa siyajui lakini pia kuna mengi ambayo nimekutananayo ambayo nayajua kwa kuyasoma kabla katika Nyaraka za Sykes na haya ninayosoma leo baada ya miaka 30 kupita wakati mwingine hayashabiani na ushahidi wa nyaraka hizo nilizosoma.

Unawezekana muda ukalaumiwa kwa kupoteza kumbukumbu za binadamu.

Kutegemea mtu akaeleza historia yake tena katika hotuba baada ya zaidi ya miaka 70 kukosea si jambo la ajabu ila bei yake inakuwa aghali mno.

Kurasa za mwanzo tu katika kitabu cha pili cha Wasifu wa Julius Nyerere panaelezwa mkutano wa mwanzo ambao Nyerere alifanya Mbeya na katika mkutano ule wazee aliozungumzanao Mwalimu walionyesha hofu yao ya kudai uhuru kutokana na yale yaliyotokea katika Vita Vya Maji Maji iliyosababisha unyama mkubwa kutendeka dhidi ya wananchi walionyanyua silaha kupambana na Wajerumani.

Mwalimu katika hotuba yake ya kuaga aliyotoa Ukumbi wa Diamond mwaka wa 1985 kayaeleza haya na waandishi wa maisha yake na wao katika kuanza kueleza mwanzo wa harakati za Mwalimu kuwaamsha watu kujikusanya katika umoja kudai uhuru wameanza na hii hofu ambayo Mwalimu aliikuta kwa wazee alipowatajia jambo la kudai uhuru.

Mkutano wa kwanza wa Mwalimu Nyerere kuzungumza na wazee haukuwa Mbeya bali ulikuwa Morogoro ambako alikwenda na Zuberi Mtemvu mwezi August, 1954 mwezi mmoja tu baada ya kuundwa kwa TANU.

Mtemvu alimuomba baba yake Mzee Mwinshehe Manga Mtemvu awakusanye wazee wenzake ili wafanye mkutano wa ndani kuhusu TANU.

Bahati mbaya mkutano huu haukufanikiwa.

Mtemvu akamwandikia barua Ally Sykes kumfahamisha mambo mawali.

Jambo la kwanza alimweleza Ally Sykes yale yaliyowakuta yeye na Nyerere Morogoro kwa kumwambia kuwa ‘’Waluguru ni wagumu,’’ kwa maana kuwa wazee wa Kiluguru wameshindwa kuupokea ujumbe na wito wa TANU.

Jambo lingine alimfahamisha Ally Sykes kuwa amezungumza na Ali Mwinyi Tambwe kuhusu TANU na Ali Mwinyi amekubali kuwaunga mkono.

Barua hii Zuberi Mtemvu kaiandika kwa penseli (Zuberi M.M. Mtemvu to Ally Sykes, 15 th August, 1954).

Yawezekana haya maneno ya hofu ya kuwakuta wana TANU kama yale yaliyowakuta wapiganaji wa Maji Maji, Mwalimu aliyasikia Morogoro na ndiyo haya Mtemvu aliyomweleza Ally Sykes kuwa ‘’Waluguru ni wagumu.’’

Hofu hii ya Vita Vya Maji Maji Mwalimu bila wasiwasi aliisikia Lindi na Mikindani kwani huko kusini ndiko vita vile vilipopiganwa kwa wakati ule, kiasi cha miaka 50 tu iliyopita.

TANU haikufika Mbeya haraka hivyo.

Katika historia ya TANU hofu ya wananchi kuwafika yaliyowafika wapiganaji wa Maji Maji ilikuwa ikitumika sana Southern Province, sehemu za Lindi, Mikindani, Masasi na Nachingwea.

Wamishionari walikuwa wanawatisha waumini wao wakae mbali na TANU wasije wakafikwa na yale waliyowafika wazee wao baina ya mwaka wa 1905 na 1907 wakati wa vita vile.

Kupambana na propaganda hii waasisi wa TANU Lindi, Suleiman Masudi Mnonji, Yusuf Chembera na Salum Mpunga wakatuma ujumbe wa watu wawili, Salum Mpunga na Ali Ibrahim Mnjale, TANU HQ Dar es Salaam ambao ndiyo walikuwa wajumbe wa mkutano wa kwanza wa TANU 1955 wabaki nyuma baada ya mkutano wawafahamishe viongozi wa TANU propaganda inayopigwa Southern Province kuwazuia wananchi wasiunge mkono TANU kwa hiyo Nyerere aende haraka akazungumze na wananchi.

Mwalimu Nyerere alikwenda Lindi akifuatana na Ali Mwinyi Tambwe na alifanya mkutano mkubwa Golf Ground ambao haukupata kuonekana.

Ilikuwa huko Southern Province ndiko Mwalimu alipoelezwa hofu hii ya watu kunyongwa iliyokuwa inaenezwa kuwazuia wananchi wasijiunge na TANU kudai uhuru.

Mwalimu alifanikiwa kuvunja propaganda ile na TANU ikaenea kote - Lindi, Mikindani, Masasi na Nachingwea.

Ukiruka historia hii ya wana TANU wa Southern Province na propaganda ya Vita Vya Maji Maji ukaingia Mbeya kwa muasisi wa TANU Fatima bint Matola historia muhimu sana inakuwa imepotezwa.

Picha ya kwanza nyumba ya Ahmed Adam Mikidani aliyolala Mwalimu Nyerere katika safari yake ya Southern Province (Picha kwa hisani ya Adam Ahmed Adam).

Picha ya pili ni Salum Mpunga na ya tatu Yusuf Chembera.
 
WASIFU WA JULIUS NYERERE: NANI ATAKUWA NA UJASIRI WA KUISAHIHISHA KAULI YA MWALIMU PALE ALIPOKOSEA TAARIFA KATIKA HISTORIA YA TANU NA MAISHA YAKE MWENYEWE?

Nasoma kitabu cha historia ya Mwalimu Nyerere na kuna mengi nimejifunza ambayo kwa hakika nilikuwa siyajui lakini pia kuna mengi ambayo nimekutananayo ambayo nayajua kwa kuyasoma kabla katika Nyaraka za Sykes na haya ninayosoma leo baada ya miaka 30 kupita wakati mwingine hayashabiani na ushahidi wa nyaraka hizo nilizosoma.

Unawezekana muda ukalaumiwa kwa kupoteza kumbukumbu za binadamu.

Kutegemea mtu akaeleza historia yake tena katika hotuba baada ya zaidi ya miaka 70 kukosea si jambo la ajabu ila bei yake inakuwa aghali mno.

Kurasa za mwanzo tu katika kitabu cha pili cha Wasifu wa Julius Nyerere panaelezwa mkutano wa mwanzo ambao Nyerere alifanya Mbeya na katika mkutano ule wazee aliozungumzanao Mwalimu walionyesha hofu yao ya kudai uhuru kutokana na yale yaliyotokea katika Vita Vya Maji Maji iliyosababisha unyama mkubwa kutendeka dhidi ya wananchi walionyanyua silaha kupambana na Wajerumani.

Mwalimu katika hotuba yake ya kuaga aliyotoa Ukumbi wa Diamond mwaka wa 1985 kayaeleza haya na waandishi wa maisha yake na wao katika kuanza kueleza mwanzo wa harakati za Mwalimu kuwaamsha watu kujikusanya katika umoja kudai uhuru wameanza na hii hofu ambayo Mwalimu aliikuta kwa wazee alipowatajia jambo la kudai uhuru.

Mkutano wa kwanza wa Mwalimu Nyerere kuzungumza na wazee haukuwa Mbeya bali ulikuwa Morogoro ambako alikwenda na Zuberi Mtemvu mwezi August, 1954 mwezi mmoja tu baada ya kuundwa kwa TANU.

Mtemvu alimuomba baba yake Mzee Mwinshehe Manga Mtemvu awakusanye wazee wenzake ili wafanye mkutano wa ndani kuhusu TANU.

Bahati mbaya mkutano huu haukufanikiwa.

Mtemvu akamwandikia barua Ally Sykes kumfahamisha mambo mawali.

Jambo la kwanza alimweleza Ally Sykes yale yaliyowakuta yeye na Nyerere Morogoro kwa kumwambia kuwa ‘’Waluguru ni wagumu,’’ kwa maana kuwa wazee wa Kiluguru wameshindwa kuupokea ujumbe na wito wa TANU.

Jambo lingine alimfahamisha Ally Sykes kuwa amezungumza na Ali Mwinyi Tambwe kuhusu TANU na Ali Mwinyi amekubali kuwaunga mkono.

Barua hii Zuberi Mtemvu kaiandika kwa penseli (Zuberi M.M. Mtemvu to Ally Sykes, 15 th August, 1954).

Yawezekana haya maneno ya hofu ya kuwakuta wana TANU kama yale yaliyowakuta wapiganaji wa Maji Maji, Mwalimu aliyasikia Morogoro na ndiyo haya Mtemvu aliyomweleza Ally Sykes kuwa ‘’Waluguru ni wagumu.’’

Hofu hii ya Vita Vya Maji Maji Mwalimu bila wasiwasi aliisikia Lindi na Mikindani kwani huko kusini ndiko vita vile vilipopiganwa kwa wakati ule, kiasi cha miaka 50 tu iliyopita.

TANU haikufika Mbeya haraka hivyo.

Katika historia ya TANU hofu ya wananchi kuwafika yaliyowafika wapiganaji wa Maji Maji ilikuwa ikitumika sana Southern Province, sehemu za Lindi, Mikindani, Masasi na Nachingwea.

Wamishionari walikuwa wanawatisha waumini wao wakae mbali na TANU wasije wakafikwa na yale waliyowafika wazee wao baina ya mwaka wa 1905 na 1907 wakati wa vita vile.

Kupambana na propaganda hii waasisi wa TANU Lindi, Suleiman Masudi Mnonji, Yusuf Chembera na Salum Mpunga wakatuma ujumbe wa watu wawili, Salum Mpunga na Ali Ibrahim Mnjale, TANU HQ Dar es Salaam ambao ndiyo walikuwa wajumbe wa mkutano wa kwanza wa TANU 1955 wabaki nyuma baada ya mkutano wawafahamishe viongozi wa TANU propaganda inayopigwa Southern Province kuwazuia wananchi wasiunge mkono TANU kwa hiyo Nyerere aende haraka akazungumze na wananchi.

Mwalimu Nyerere alikwenda Lindi akifuatana na Ali Mwinyi Tambwe na alifanya mkutano mkubwa Golf Ground ambao haukupata kuonekana.

Ilikuwa huko Southern Province ndiko Mwalimu alipoelezwa hofu hii ya watu kunyongwa iliyokuwa inaenezwa kuwazuia wananchi wasijiunge na TANU kudai uhuru.

Mwalimu alifanikiwa kuvunja propaganda ile na TANU ikaenea kote - Lindi, Mikindani, Masasi na Nachingwea.

Ukiruka historia hii ya wana TANU wa Southern Province na propaganda ya Vita Vya Maji Maji ukaingia Mbeya kwa muasisi wa TANU Fatima bint Matola historia muhimu sana inakuwa imepotezwa.

Picha ya kwanza nyumba ya Ahmed Adam Mikidani aliyolala Mwalimu Nyerere katika safari yake ya Southern Province (Picha kwa hisani ya Adam Ahmed Adam).

Picha ya pili ni Salum Mpunga na ya tatu Yusuf Chembera.
Angalia picha:
Screenshot_20200616-231107.jpg
 

Attachments

  • SALUM MPUNGA.jpg
    SALUM MPUNGA.jpg
    5.4 KB · Views: 3
  • YUSUF CHEMBERA.jpg
    YUSUF CHEMBERA.jpg
    25.5 KB · Views: 3
Mzee wangu Mohamed Said, salam alaykum.
Kwanza naomba kutangaza maslahi, mimi ni muislam.
Pili naomba kumshukuru Mungu kwa kipaji kikubwa alichokujalia, una hekima, busara nyingi na upeo mkubwa wa upambanuzi wa mambo (kwa mtazamo wangu ).

Hoja yangu;
Mimi sio mtaalamu mbobezi wa historia kama wewe, lakini ipo mifano mingi inayoonyesha historia hukumbuka zaidi mambo makubwa na kwa uchache kuliko mambo madogo madogo kwa wingi (yaani historia iandike mpaka siku gani walikunywa chai nyumbani kwa nani!!!!???). Mfano 99% ya wazanzibari ni waislam lakini mimi namjua sheikh Abeid Aman Karume kama shujaa mkuu. Najua wapo mashujaa wengi nyuma yake lakini siwajui, akitajwa Karume tayari naona jambo la uhuru wa Zanzibar limekamilka. Je,? Haiwezi kuwa ni sheria hii ya historia ndio iliofanya hata hapa kwetu baadhi ya mambo ya kihistoria yadogoshwe na si kupuuzwa kwa mchango wetu waislam! !???

Hoja nyingine;
Mzee wangu, Katika tafiti zako ni mara nyingi umeamini taarifa hasa pale zinapotolewa na muhusika mwenyewe nikikunukuu unaita 'From horse's mouth
'. Sijawahi kukuona ukizitafutia uthibitisho zaidi taarifa za wazee wetu wa kiislamu. Katika mada hapo juu umemkosoa Nyerere (Horse's mouth ) kwa kumbu kumbu za mtu mwingine. Je, Horse's mouth inaheshimiwa kwa wazee wetu tu?

Hoja yangu nyingine:
Mzee wangu, ulicho kifanya hapo juu kisayansi kinahakikisha ubora wa utafiti wowote yaani kuhakikisha usahihi wa data kutakupelekea kufanya uchambuzi sahihi na kufikia hitimisho sahihi. Mara nyingi nimeona picha na maelezo, hamna shida tunaamini. Je, unatumia mbinu gani kuthibitisha usahihi wa taarifa hizo, isije kupikwa kama alivo pika Mzee Nyerere hapo juu? NB: Wazee wetu wengi tu wana tabia ya kujimwambafy mbele ya vijana kama vile walikua bora katika kila kitu. Mfano kujifanya walikua hodari wa masomo, kujifanya kuwajua watu mashuhuri au kusoma nao n.k n.k

Kwa leo naomba niishie hapa Kwanza mzee wangu. Nina mengi sana ninayotamani kujifunza kutoka kwako. Nitafurahi sana kujua kama una mahala unapopatikana kama mtu atawiwa kukuona, kukusalimu na kupata fikra zako.
 
Mzee wangu Mohamed Said, salam alaykum.
Kwanza naomba kutangaza maslahi, mimi ni muislam.
Pili naomba kumshukuru Mungu kwa kipaji kikubwa alichokujalia, una hekima, busara nyingi na upeo mkubwa wa upambanuzi wa mambo (kwa mtazamo wangu ).

Hoja yangu;
Mimi sio mtaalamu mbobezi wa historia kama wewe, lakini ipo mifano mingi inayoonyesha historia hukumbuka zaidi mambo makubwa na kwa uchache kuliko mambo madogo madogo kwa wingi (yaani historia iandike mpaka siku gani walikunywa chai nyumbani kwa nani!!!!???). Mfano 99% ya wazanzibari ni waislam lakini mimi namjua sheikh Abeid Aman Karume kama shujaa mkuu. Najua wapo mashujaa wengi nyuma yake lakini siwajui, akitajwa Karume tayari naona jambo la uhuru wa Zanzibar limekamilka. Je,? Haiwezi kuwa ni sheria hii ya historia ndio iliofanya hata hapa kwetu baadhi ya mambo ya kihistoria yadogoshwe na si kupuuzwa kwa mchango wetu waislam! !???

Hoja nyingine;
Mzee wangu, Katika tafiti zako ni mara nyingi umeamini taarifa hasa pale zinapotolewa na muhusika mwenyewe nikikunukuu unaita 'From horse's mouth
'. Sijawahi kukuona ukizitafutia uthibitisho zaidi taarifa za wazee wetu wa kiislamu. Katika mada hapo juu umemkosoa Nyerere (Horse's mouth ) kwa kumbu kumbu za mtu mwingine. Je, Horse's mouth inaheshimiwa kwa wazee wetu tu?

Hoja yangu nyingine:
Mzee wangu, ulicho kifanya hapo juu kisayansi kinahakikisha ubora wa utafiti wowote yaani kuhakikisha usahihi wa data kutakupelekea kufanya uchambuzi sahihi na kufikia hitimisho sahihi. Mara nyingi nimeona picha na maelezo, hamna shida tunaamini. Je, unatumia mbinu gani kuthibitisha usahihi wa taarifa hizo, isije kupikwa kama alivo pika Mzee Nyerere hapo juu? NB: Wazee wetu wengi tu wana tabia ya kujimwambafy mbele ya vijana kama vile walikua bora katika kila kitu. Mfano kujifanya walikua hodari wa masomo, kujifanya kuwajua watu mashuhuri au kusoma nao n.k n.k

Kwa leo naomba niishie hapa Kwanza mzee wangu. Nina mengi sana ninayotamani kujifunza kutoka kwako. Nitafurahi sana kujua kama una mahala unapopatikana kama mtu atawiwa kukuona, kukusalimu na kupata fikra zako.
Nyango...
Sijaelewa khasa nini unataka kujua.
Labda ungenifahamisha kwa maneno machache nipate kukujibu In Shaa Allah.
 
Really? Hao ambao siwaonei huruma ni akina nani? Hivi umewahi kuwaza namna mababu na mabibi zetu walivyoteseka ktk biashara ya utumwa? Ungekuwa na imani hata chembe ungeumia sana. Na wewe ulipenda waendelee kuteswa na waarabu na wazungu? Why unakosa imani na huruma kwa wenzio?

ID yako tu inaashiria jinsi ulivyo, huna imani wala huruma kwa binadamu wenzio,,,
 
Really? Hao ambao siwaonei huruma ni akina nani? Hivi umewahi kuwaza namna mababu na mabibi zetu walivyoteseka ktk biashara ya utumwa? Ungekuwa na imani hata chembe ungeumia sana. Na wewe ulipenda waendelee kuteswa na waarabu na wazungu? Why unakosa imani na huruma kwa wenzio?


Ziko wapi hizo picha za waarabu wakitesa babu zetu?????
 
ID yako tu inaashiria jinsi ulivyo, huna imani wala huruma kwa binadamu wenzio,,,
Waislam ndio wasio na huruma kwa binadamu wenzao.

Ndugu zao ni waislam wenzao tu, wengine ni Makafiri na wapi tayari kujilipua ili kuwaua

Hata huyu Mleta mada ana CHUKI SANA kwa Wakristo, sisi tunamfahamu na mada zake ambazo pia zina uzushi mwingi.

Nyerere ni Legend anayetambuliwa na Dunia sio hapa Tanzania tu.

Ni Baba wa Taifa hili.
 
Really? 😳😳😳 We ulikuwa mjakazi wa mwarabu nini? Maana tende tu ziliuza utu wa baadhi ya waafrika.

Kuwa mjakazi wa mwarabu haiondoshi ukweli,,nyie ni ndugu zangu lakini mnavyowafanyia waarabu sivyo, lazima tuwekane wazi mnawachukia sana waarabu/waislamu na huo ndio ukweli wenyewe. Kama wewe ni kidume kweli naomba hizo picha zikiwaonyesha waarabu wakiwatesa babu zetu, najuwa huna ni chuki tu zinawasumbua.
 
Waislam ndio wasio na huruma kwa binadamu wenzao.

Ndugu zao ni waislam wenzao tu, wengine ni Makafiri na wapi tayari kujilipua ili kuwaua

Hata huyu Mleta mada ana CHUKI SANA kwa Wakristo, sisi tunamfahamu na mada zake ambazo pia zina uzushi mwingi.

Nyerere ni Legend anayetambuliwa na Dunia sio hapa Tanzania tu.

Ni Baba wa Taifa hili.

Uislamu haufundishi kumchukia mwenzio, acha kuropoka.

Hivyo hayo ni mawazo yenu, na kufuata mnachoaminishwa na miungu yenu/mabeberu nanyi mkaamini,,,Mzungu hakuacha kitu kwa mtu mweusi 😁😁
 
Waislam ndio wasio na huruma kwa binadamu wenzao.

Ndugu zao ni waislam wenzao tu, wengine ni Makafiri na wapi tayari kujilipua ili kuwaua

Hata huyu Mleta mada ana CHUKI SANA kwa Wakristo, sisi tunamfahamu na mada zake ambazo pia zina uzushi mwingi.
Nafasiyerere ni Legend anayetambuliwa na Dunia sio hapa Tanzania tu.

Ni Baba wa Taifa hili.
Azarel,
Nafasi ya Mwalimu Nyerere kama Baba wa Taifa sidhani kama hata siku moja imepata kuwa suala la Watanzania kupingana.

Jina la Mwalimu Nyerere ni kubwa sana na watafiti wengi huja kunihoji kuhusu historia yake nami huwapa historia ya siku za mwanzo za Julius Nyerere na nawafikisha ilipokuwa nyumba ya Abdul Sykes.

Hapo nawaeleza ndipo safari ya Nyerere ya siasa ilipoanza.

Watafiti hawa wanasikitika kuwa hakuna alama yoyote ya kuonyesha historia hii kubwa ya mahali hapo.

Kisha nawachukua hadi Ukumbi wa Arnautoglo na nawapa historia ya ule uchaguzi wa 1953 kati ya Abdul Sykes na Nyerere.

Ukumbi ule ulipofanyika uchaguzi ule hivi sasa ni ukumbi wa mikutano.

Hawa watafiti huniuliza mbona hakuna alama yoyote kuonyesha historia hii?

Mimi huwaeleza ukweli kuwa historia hii bado haijatambuliwa.

Kisha huwapitisha Soko la Kariakoo Abdul Sykes alipokuwa Market Master na huwaeleza kuwa Mwalimu alianza kupata watu hapa sokoni alipokuwa akija ofisini kwa Abdul Sykes.

Wao hushauri kwa uchache kuwa kwenye nyumba ya Abdul Sykes na Ukumbi wa Arnautoglo na Soko la Kariakoo ziwekwe ''plaque,'' kubwa zenye kuonesha historia za hawa wazalendo wawili kwani huko ndipo Nyerere alipotokea na kuiteka Tanganyika nzima.

Mimi hutaabika sana nashindwa kuwaambia kuwa ipo kumbukumbu ya Julius Nyerere na TANU Mwananyamala nyumbani kwa Mzee Mwinjuma Mwinyikambi ambako kuna kibao kuwa TANU ilizaliwa hapo.

Ukweli ni kuwa sijakuwa na ujasiri wa kumpeleka mtafiti yeyote pale.

Watanzania hatupingani katika heshima ya Mwalimu Nyerere kama Baba wa Taifa.

Tatizo la historia ya Julius Nyerere ni kama hivi nilivyoeleza hapa na kwa kweli wengi wenu hamjui historia ya Mwalimu kwa uhakika wake.

Picha ya kwanza ni nyumba ya Abdul Sykes kama ilivyo hivi sasa na picha ya pili ni Ukumbi wa Arnautoglo na picha ya tatu ni Soko la Kariakoo.

Watafiti wa historia ya Mwalimu Nyerere mara nyingi wameniambia kuwa ni muhimu hizi kumbukumbu zihifadhiwe kwa angalau kuweka ''plaque,'' zinazoeleza umuhimu wa majengo haya na matukio yaliyopitika katika sehemu hizo.
 

Attachments

  • NYUMBA YA ABDUL SYKES ILIVYO SASA.jpg
    NYUMBA YA ABDUL SYKES ILIVYO SASA.jpg
    28.7 KB · Views: 3
  • ARNAUTOGLO HALL.png
    ARNAUTOGLO HALL.png
    81.2 KB · Views: 2
  • KARIAKOO MARKET 1950.jpg
    KARIAKOO MARKET 1950.jpg
    12.1 KB · Views: 3
Sasa nshagundua ujinga wako nini. Unahusisha waarabu na uislamu.kwahiyo unaona ni bora ungetawaliwa na mwarabu sababu ni mwislam.na waliofanya mapinduzi walikuwa dini gani?

Wewe nioneshe picha ambazo muhamad alkuwa akipigana na makuresh au alipokuwa amejificha kwenye pango na kuna watu wanamtafuta wamuue.

Tungekuwa na akili hiyo hata wazungu wangeachwa sababu wakristo wangeona ni wenzao. Huo ni ubwege. Unaamini mtu anayepinga ukoloni zanzibar anachukia uislamu wakati huo hujui mimi ni dini gani.

Hiki ni kiwango cha lami kabisa.

Kuwa mjakazi wa mwarabu haiondoshi ukweli,,nyie ni ndugu zangu lakini mnavyowafanyia waarabu sivyo, lazima tuwekane wazi mnawachukia sana waarabu/waislamu na huo ndio ukweli wenyewe. Kama wewe ni kidume kweli naomba hizo picha zikiwaonyesha waarabu wakiwatesa babu zetu, najuwa huna ni chuki tu zinawasumbua.
 
Mzee wangu Mohamed Said, salam alaykum.
Kwanza naomba kutangaza maslahi, mimi ni muislam.
Pili naomba kumshukuru Mungu kwa kipaji kikubwa alichokujalia, una hekima, busara nyingi na upeo mkubwa wa upambanuzi wa mambo (kwa mtazamo wangu ).

Hoja yangu;
Mimi sio mtaalamu mbobezi wa historia kama wewe, lakini ipo mifano mingi inayoonyesha historia hukumbuka zaidi mambo makubwa na kwa uchache kuliko mambo madogo madogo kwa wingi (yaani historia iandike mpaka siku gani walikunywa chai nyumbani kwa nani!!!!???). Mfano 99% ya wazanzibari ni waislam lakini mimi namjua sheikh Abeid Aman Karume kama shujaa mkuu. Najua wapo mashujaa wengi nyuma yake lakini siwajui, akitajwa Karume tayari naona jambo la uhuru wa Zanzibar limekamilka. Je,? Haiwezi kuwa ni sheria hii ya historia ndio iliofanya hata hapa kwetu baadhi ya mambo ya kihistoria yadogoshwe na si kupuuzwa kwa mchango wetu waislam! !???

Hoja nyingine;
Mzee wangu, Katika tafiti zako ni mara nyingi umeamini taarifa hasa pale zinapotolewa na muhusika mwenyewe nikikunukuu unaita 'From horse's mouth
'. Sijawahi kukuona ukizitafutia uthibitisho zaidi taarifa za wazee wetu wa kiislamu. Katika mada hapo juu umemkosoa Nyerere (Horse's mouth ) kwa kumbu kumbu za mtu mwingine. Je, Horse's mouth inaheshimiwa kwa wazee wetu tu?

Hoja yangu nyingine:
Mzee wangu, ulicho kifanya hapo juu kisayansi kinahakikisha ubora wa utafiti wowote yaani kuhakikisha usahihi wa data kutakupelekea kufanya uchambuzi sahihi na kufikia hitimisho sahihi. Mara nyingi nimeona picha na maelezo, hamna shida tunaamini. Je, unatumia mbinu gani kuthibitisha usahihi wa taarifa hizo, isije kupikwa kama alivo pika Mzee Nyerere hapo juu? NB: Wazee wetu wengi tu wana tabia ya kujimwambafy mbele ya vijana kama vile walikua bora katika kila kitu. Mfano kujifanya walikua hodari wa masomo, kujifanya kuwajua watu mashuhuri au kusoma nao n.k n.k

Kwa leo naomba niishie hapa Kwanza mzee wangu. Nina mengi sana ninayotamani kujifunza kutoka kwako. Nitafurahi sana kujua kama una mahala unapopatikana kama mtu atawiwa kukuona, kukusalimu na kupata fikra zako.
Mheshimiwa pamoja na na hoja zako kuwa za wazi na ukweli...mleta mada eti hajakuelewa?!!!

Huyu mzee anachokifanya wakati mwingine ni kuwafanya wajinga hata hao anaokesha akijiadai anawatetea
 
Mheshimiwa pamoja na na hoja zako kuwa za wazi na ukweli...mleta mada eti hajakuelewa?!!!

Huyu mzee anachokifanya wakati mwingine ni kuwafanya wajinga hata hao anaokesha akijiadai anawatetea
Mzizi...
Kweli sijaelewa .

Ikiwa wewe umeelewa wepesi ni kunifahamisha ili nijibu.

Ikiwa tutalaumiana tutabaki hatuna jibu.
 
Back
Top Bottom