Nani ni shabiki wa Yanga, nani ni shabiki wa Simba kwa watu maarufu unaowafahamu?

Mc cane

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
5,570
Reaction score
10,517
Wakuu salaam,

Kwa Ufupi naomba tutaje watu maarufu kama wachezaji wa zamani, wachezaji wa sasa, Watangazaji wa michezo, wanasiasa n.k. ambao ni washabiki wa Yanga au Simba.

Wengi (wahusika) wamekuwa wakificha, lakini kwa kuwa sisi tumekua nao, tumesoma nao, tunafanya nao kazi, tunaishi na ndugu zao, kwa namna moja au nyingine tutakuwa tunafahamu timu wanazoshabikia kati ya hizo mbili

Mimi naanza na Kitenge ni Yanga, Shafii Dauda ni Simba, Kikwete ni Yanga, Makonda ni Simba

Tuendelee
 
Mwigulu Yanga, the late Mkapa Yanga
 
January Makamba na baba yake Simba
 
The late Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Yanga, the late Alli Abeid Karume Yanga
 
Jonas Mkude simba, Ajib Simba
 
Yanga: Nape Mnauye, Lady Jaydee, Mwakyembe, Edo Kumwembe, Kiba, AY, Joketi, Irene Uwoya, Ray Kigosi, Anne Makinda, Mizengo Pinda, Kinana, Freeman Mbowe, Jenista Mhagama, Venace Mabeyo, Lipumba, Mheshimiwa Temba, Cheyo, Tundu Lisu, Boniface Wambura, Dkt Sheini, Lowasa, Mzee wa Upako
Simba: Sugu, Profesa Jay, JB, Mwana-FA, Tulia, Ali Choki, Kigwangala, Sofia Simba, Ramadhani Dau, Mondi, Gwajima...
 
SIMBA SC : Kibadeni, Ismail Aden Rage, Azim Dewji, Bakhresa Said, Suleiman Matola, Hassan Mgosi, .Mo Dewji, Hans Pope, Haruna Moshi, Naseeb Abdul, Tunda Man na wengine wengi.

©Simba Nguvu Moja
 
Edo simba mkuu, kwa wengine nakubaliana na wewe

Simba mwingine Zito Zuberi Kabwe
 
Nimepenyezewa hapa kumbe hata Harmonize ni Simba, ila kibiashara imebidi atumbuize Wiki ya Wananchi baada ya Azam kumtumia Kiba
 
Nimekua nae huyo namjua vizuri sana na pia mnazi mkubwa wa Arsenal. Kwa Yanga anajificha tu. Ila mwanajangwani kindakindaki huyo
Basi atakuwa amejitahidi sana kujificha, maana wengi wanamchukulia Edo Kumwembe kuwa ni Simba
 
Ndivyo watu wanavyo jua hivyo, kama ni Yanga amejitahidi sana kutoonesha
Basi atakuwa amejitahidi sana kujificha, maana wengi wanamchukulia Edo Kumwembe kuwa ni Simba
 
Basi atakuwa amejitahidi sana kujificha, maana wengi wanamchukulia Edo Kumwembe kuwa ni Simba
Anajificha lakini anaumia sana Yanga ikifanya vibaya. Hata kwa Arsenal anajificha kwa Liverpool
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…