Nani wa kulaumiwa mkanganyiko wa zoezi la sensa.

Kachanchabuseta

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2010
Posts
7,264
Reaction score
678
Kumekuwa na wimbi kubwa la watu kujiandaa kugombea sensa ya makazi na watu
huku wangine wakisema kuwa haina tija kwa taifa na kwa yeye binafsi. Napenda kuwapa
onyo kwa wote ambao wanampango wa kugomea hii sensa hawatapewa vitambulisho vya utaifa.

Hizi takwimu za sensa ndo zitatumiaka kuandaa vitambulisho vya UTAIFA

Na kwa wale wanaosema watashianda kwenye majumba ya kuabudia na kutoka nyumbani mapema na
kurudi wamechelewa, nawaonya mkae majumbani muhesabiwe maani hii itakukosesha kitambulisho chako cha
uraia maana hutahesabika kama mtanzania


Ujumbe:Usipoteze utaifa wako kaa uhesabiwe
:israel:
Dr. Kupeng'e
PHD, Sockholm University
 
kama kutokuwa na kitambulisho kutaniondolea sifa ya kuwa mtanzania ....nitachoma moto passport, cheti cha kuzaliwa na wanipeleke kwetu wanakokujua wao.
 
asante sweetie. msalimie mumeo baba mwanaisha
 
DR. Kupeng'e wewe ni Bakwata au Balukta? Gamba au Gwanda?
Sunny au Shiite? Funguka Dr!
 
hivi bado unafikiri watanzania ni wapumbavu kiasi hicho kwa hiyo nisipo hesabiwa serikali yaccm itanitafutia uraia wa nchi nyingi..kawadanganye wehu wenzako tena mkinizingua hata mimi si hesabiwi nione ninavyokosa uraia..
 

Dr umetoa pumba zako! shame on you. Haya ni mazoezi mawili tofauti. Sensa ni sensa inajitegemea na zoezi la vitambulisho vya kitaifa ni zoezi tofauti. Au una udaktari wa magamba???? Umeaibisha wasomi wa kweli kama kweli you are a PhD holder- changanua mambo kama Dokta siyo kupotosha watu hapa.
 
Kadiri ninavyokumbuka,viongozi mbalimbali waandamizi nchini akiwemo Mwenyekiti wa Tume ya Maoni ya Katiba,Mh. J.S. Warioba,walishauri kuwa wachache wasikilizwe. Ni wale wanaogomea na kupinga uwepo wa Muungano. Sina hakika kama tayari. Tena,wapo 'wachache' waliotangaza kugomea sensa. Ushauri wa kusikilizwa mbona haupo? Wanapuuzwa? Serikali inajua athari ya kupuuza? Leo ni leo...
 
Ph D siku hizi hazina maana! Hata Mrema anayo!
 

Kwa hiyo Utanzania ni kuhesabiwa!??, Acha kudhalilisha taifa na Vinjaa vyako.
 
Dr huyu ni Mhadhili wa chuo kikuu cha unafiki!
 
View attachment 62803

Nombeni lift. NAHITAJI KUONGELEA SENSA KWA UHURU. CHOMBO GANI MNAKIJUA NIENDE KUONGELEA. NAWOMBENI JAMANI TAFADHALI. LEO NDIO SIKU YA MWISHO. Iiiiiii! mhhhh!!!!! iiiiiiiiii!!
 
Hata mkisema nini Mimi na kaya yangu hatutakubali kuhesabiwa mnatutishia uraia? Uraia wenyewe wa Tanzania! Mtupeleke basi huko kwetu Shenz type

 
Phd za akina Hemed wa bongo movie hizo wala diploma huna kama kweli una phd basi umegush.kwakifupi mtanzanis ashajitambua hivo vitisho ilikua enzi zile za ujamaa sio leo kawadanganye haohao waislam wasio na msimamo ila mwenye msimamo hakuna kuhesabiwa huo ndo mpango mzima!
 
PHD propaganda, any way ziangalie hoja hizi za serikali na majibu waliyopewa may be kuna cha kujadili

1Serikali haiwezi kurejesha kipengele hicho kwa kuwa ‘Baba wa Taifa'alikiondosha ili kujenga umoja wa Kitaifa. Haya yalisemwa na viongozi waSerikali katika mkutano wake na viongozi uliofanyika Dodoma tarehe 11 Juni2012.

2 Kuhesabiwa watu kwa msingi wa dini zao kutapekelekea uvunjifu wa amani nautulivu nchini.

3 Serikali haipangi maendeleo kwa kuangalia dini (haya yalisemwa na Wazirikatika ofisi ya Rais Sera na Uhusiano, Stephen Wasira katika semina hiyo Dodomana Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika kujibu maswali ya papo kwa papo bungenitarehe 09 August 212.

4 Serikali ya Tanzania inafuata utaratibu wa Sensa wa Kimataifa ambao nikuhesabiwa watu bila ya kuhusisha kabila wala dini zao.


MAJIBU

1. Anayotamka ‘Baba wa Taifa' si wahyi (ufunuo) kutoka mbinguni, ni yeye ndiealietuletea sera ya chama kimoja, na azimio la Arusha na siasa ya Ujamaa nakujitegemea. Sera sote hizo zimeshindwa na hili la kuondoa kipengele cha dini badalaya kuleta umoja wa kitaifa umeleta mtengano kwa sababu limeanza kuamsha hisiaza dhulma na upendeleo dhidi ya Waislam na kuibuka takwimu zisizo sahihi. Nakwa hilo nalo Serikali ni lazima iweke pembeni fikra hizi za ‘Baba wa Taifa'ili kuokoa nchi na uvunjifu wa amani.

2. Kuacha kukitia kipengele cha dini katika takwimu ya kitaifa ndio ambakokunaweza kuvunja amani hasa pale ambapo baadhi ya raia kuhisi kwambawanabaguliwa kwa madai kwamba wao ni wachache na wanadhulumiwa na kunyimwa hakizao nyingi. Hii ndio inaweza kuleta uvunjifu wa amani. Isitoshe nchi nyingizikifanya takwimu zinaweka kipengele cha kujua dini za watu. Nchi kamaMarekani, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, India, Kenya, Uganda n.k. zinafanyahivyo na hujasikia hata nchi moja duniani kumetokea uvunjifu wa amani kwasababu hiyo.

3. Si kweli kwamba Serikali haipangi maendeleo yake kwa kuzingatia dini kwasababu Serikali haina dini. Ukweli ni kwamba Serikali inapanga maendeleo yakekwa kuzingatia sana dini lakini ni ya kikristo. Mfano ni ule mkataba wamaelewano baina ya Serikali na Kanisa (MOU), ahadi ya Serikali ni "Kushirikianana Makanisa kupanga sera na maendeleo ya sekta ya Elimu, Afya na huduma zaJamiii." Je hii si mipango ya maendeleo. Mkataba huo (MOU) umetoa mamlaka yakuundwa kwa tume ya kikristo ya huduma ya Jamii (CSSC) kwa lengo la kuunda serazinazofanana kwa huduma za makanisa na afya na elimu wa makubaliano na Serikaliya Tanzania.

Pia mkataba huo umelenga kuwa na utekelezaji sawa kwa Serikali na makanisakatika maendeleo ya jamii. Je, huu si mpango wa maendeleo baina ya Serikali naWakristo.

Katika kifungu cha 11 cha mkataba huo kinasema:
"Serikali ni lazima itoe nafasi za ajira katika vyuo vyake vya Ualimu (TTC)kwa Wakufunzi wa kikristo kufundisha watu wataofuzu kama Walimu kwa ajili yashule za Makanisa zilizoanzishwa."
Je, hii si mipango ya maendeleo kwa kuzingatia dini?

Kutokana na makubaliano hayo baina ya Serikali na kanisa, imelazimika Serikalikuyapa makanisa mabilioni ya fedha za wa-Tanzania kila mwaka katika utekelezajiwa mkataba huu. Mfano mwaka 2008 Serikali iliyapa makanisa jumla shilingibilioni 170 (Gazeti la Jambo Leo la Jumapili 20/03/2011) liliandika hivi:

"Mwaka 2009 Serikali iliyapa makanisa shilingi bilioni 45. Mwaka 2010iliyapa shilingi bilioni 61.9."

Kwa maana hiyo Serikali kuanzia 2008 hadi 2011 imeyapa makanisa na taasisi zakeshilingi billioni 331. Jee Waislam na taasisi zake wamepewa nini?

Pia iweleweke kwamba zaidi ya asilimia 54 ya bajeti ya Wizara ya Afya inakwendakwenye vituo vya Afya, zahanati, mahospitali na taasisi nyingine za afya zakikristo. Je fedha hizi zinaweza kutoka bila ya Serikali kuwa na mipango yamaendeleo?

4. Hoja ya kwamba Serikali inafuata mpango wa Sensa wa kimataifa unaiohusishadini wala kabila si ya kweli kwa sababu utafiti unaonyesha kwamba Umoja waMataifa unataka Sensa iwe na kipengele cha dini, kabila, utaifa na lugha n.k.Hii inasaidia kuleta ufahamu na kujuana na hili limebainishwa katika Quran paleAllaam (Subhaanahu wa Ta'ala) Aliposema:

يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنَّا خَلَقْنَاكُم مِّن ذَكَرٍ وَأُنثَىٰ وَجَعَلْنَاكُمْشُعُوبًا وَقَبَائِلَ لِتَعَارَفُوا ۚ إِنَّ أَكْرَمَكُمْ عِندَ اللَّـهِ أَتْقَاكُمْ

"Enyi watu Hakika Sisi tumewaumbeni kutoka na Mwanamme (Aadam) na Mwanamke(Hawaa) na tumewajaalieni mataifa na Makabila mbali mbali ili mpate kujuanahakika mbora wenu mbele ya Allaah ni Mchaji Allaah zaidi katika nyinyi." [Al-Hujuraat:13].

Ili kupatikana Sensa iliyo sahihi kitengo cha Sensa cha Umoja wa mataifakimetoa maelekezo yafutayo kwa nchi wanachama zinazotaka kufanya Sensa.Kipengelle nambari 2.109 hadi 2.111 chasema hivi:

"For the benefit of users of the data who may not be familiar with all ofthe religions or sects within the country as well as for the purposes ofinternational comparability, the clasifications of the data should show eachsect as a sub category of religion of which it forms a part. A brief statementof the tenets of releigions or sects that are not likely to be known beyond thecountry or region would also be helpful." (www.unistats.un.org [5]).

Tafsiri
"Kwa faida ya watumiaji wa Takwimu ambao wanaweza wakawa hawafahamu dinizote na madhehebu yote yaliyopo katika nchi, vile vile kwa madhumuni yaulinganishaji wa kimataifa, uchambuzi wa takwimu lazima uonyeshe kila dhehebukama sehemu inayounda dini nzima kwa ujumla wake. Maelezo mafupi ya waumini wadini au madhehebu ambayo yanawerza yakawa hayafahamiki nje ya nchi au ukandayangeweza kuwa ni msaada. (Angalia tovuti www.unistats.un.org [5]).

Hii inaonyesha wazi kwamba Umoja wa Mataifa wenyewe wanataka kipengele cha dinikuwepo kwenye Sensa kwa faida ya wote. Kwa nini basi Serikali ya Tanzaniaikatae kuweka kipengele cha dini katika Sensa ilhali yenyewe ni mwanachamamwenye kufuata mikataba ya Umoja wa Mataifa?


 
Udaktari unadhalilika sana siku hizi dah......yaani huyu Dr. nae kajenga hoja hapa......!!!!!!!

Hivi mtu akiamua kuwa mjeuri akakuambia yeye ni machinga mwaka wa 20 sasa hajawahi kuwa na kitambulisho na maisha yake hayana uhusiano wowote na kitambulisho wala census so hana haja nacho so hashiriki na hiyo census yenyewe .......unafanya nini there after??????
 

Well said sir, tafadhali weka pdf ya MOU kila siku tunasikia MOU tuu, ungeipost hapa
 
kamtishe anayekupumilia!hakuna faida ya sensa kwa nchi ya kifisadi kama tanzania!hapo ni kula pesa ya unfpa tuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…