Nani yupo nyuma ya Fred katika dili la Simba?

Kama ulikuwa na jibu uzi umeleta wa nin hapa na kwanini unatumia akili zako ndogo kujadili akili kubwa huoni kama unajitafutia magonjwa ya moyo bure ahahahah
[emoji16][emoji16][emoji16] kumbe jibu analo

Yanga hawataki na sisi tulete jezi makini kama zao
 
Mafanikio ya Simba yatambeba, yeye akomae na TBS kuchoma feki
hakika mkuu. pale pesa ipo sana,akiweka mkakati mzuri wa kupambana na vishoka itapiga hela sana. kwenye upande wa marketing yupo vizuri sana. Kizuri zaidi anapanua wigo wa bidhaa.
 
Nyuma yake yupo Mo anayachambua mambumbumbu/Mikia/Bodaboda kama samaki siku yakija kupata akili kuwa tumeibiwa Mo tayari atakuwa amepata chake
 
Nimemsikiliza vizuri huyo "vunjabei" na kutokana na maongezi yake anaonekana atafanikiwa akipata msaada toka serikalini, Simba na wapenda michezo kwa ujumla. Kwa maelezo yake inaonekana anajua wakina nani huwa wanaleta jezi feki na sehemu wanapozitengeneza hizo jezi feki huko China. Na kwakua amefanya biashara muda mrefu China na hata bongo anaijua vizuri basi ni jukumu la TRA na vyombo vya dola kumsaidia pale atakapoleta taarifa za uhakika ili watuhumiwa wakamatwe na mizigo yao itaifishwe/iharibiwe ikikamatwa bandarini. Kwa kufanya hivyo serikali itakuwa inapata kodi stahiki kutoka kwa wafanya biashara halali kama "vunjabei" na vilabu vyetu vyote vitapata udhamini unaostahili kutokana na mauzo ya jezi na bidhaa nyingine kwa kupitia nembo za vilabu.

Kuna watu hapa wanabisha na kuona udhamini wa bilioni mbili kuwa ni mkubwa. Kiuhalisia kabisa kwa timu kama Simba au Yanga udhamini wa kutengeneza bidhaa kupitia nembo ya vilabu hivi viwili haupaswi kuwa chini ya bilioni 10 iwapo kutakuwa na usimamizi sahihi na kuzuia bidhaa feki zisiingie sokoni. Hizi timu inakadiriwa kila moja kuwa na wapenzi/mashabiki wasiopunguwa milioni 20. Je tumeshawahi kujiuliza kuwa iwapo wapenzi/mashabiki milioni 2 tu wakinunua jezi za juu tu kwa kati ya TZS 25,000 mpaka 35,000 ni kiasi gani kitapatikana kama faida baada ya kuondoa gharama? Hapo bado hujakutana na wale wapenzi/mashabiki wehu kama laki 5 hivi hao wakanunua bidhaa nyingine zote kama skafu, cover za simu, kofia n.k.

Ni wakati sasa wa kuwapa sapoti badala ya kuwakatisha tamaa watu waliojilipuwa kama "vunjabei" ili wakifanikiwa vilabu vyetu vitafaidika na serikali nayo itapata kodi stahiki.
 
Sasa kwa hesabu zako hizo unazoona hazina tija ni nan amtumie kwenye biashara isiyo na faida?
 
Nahisi ni Mradi wa JPM
 
We jamaa una akili fupi we kama huna hela unadhani watu wote hawana hela et?
 
Mashabiki wa Simba ni mambumbumbu - Aden Ismail Rage, Mwenyekiti Mstaafu wa Simba Sports
Unajua mara ya kwanza kipindi nakusoma nikajua labda mtu mwenye akili amepost ili tupate undani wa hili dili la Fred, kumbe mwanautopolo mwenye wivu wa kumaskini, lazima wew ni miongoni wa wanyonge, wanoishi chini ya dola 1 kwa siku.
 
Tulihoji hapa, tukabezwa
 
Mo Sports
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…