Nani yupo sahihi,Afande Sele au Mrisho Mpoto?

Nani yupo sahihi,Afande Sele au Mrisho Mpoto?

Kama nilivotangulia kusema awali hii dhana ya uzawa ni dhana ya watu wabinafsi kupindukia na most of them ni kutoka mataifa duni kupindukia justin bieber sio mmarekan anold schwazniger sio mmarekan celine dion pia ni mkanada unless kama case study yako ni north korea au somalia mpoto yuko sawa kabisa unless kama hilo shavu angempa fally ipupa ila mzee wa masauti tuko nae mitaani uku na punde anaukana uraia wake wa kongo nyie bado mnamuona sio mzalendo
braza mbona mgumu kuelewa, wamerekani asili ni watu kama millioni 5 tu huku 98% ni wahamiaji kule hivyo kusema kila sekta itashikwa na wazawa ni uongo.

sasa kuendelea kunipa mfano toka marekani unapoteza muda maana kule karibu wote ni wahamiaji

je huku kwetu hali ikoje, kwa nini umuondoe mtanzania na kumpa mgeni(umeupimaje uzalendo wake)
 
Uzalendo sio rangi au asili ya nchi unakotoka!Bali ni fikra na utayari kuipigania nchi kwa ajili ya maendeleo na ukombozi wa wanyonge!Alichoeleza mpoto kina maana na ndio fikra hasa za uzalendo!Kuna mijitu imezaliwa hapa na mijizi haina huruma na wanyonge,kisa mweusi utamwita mzalendo?lakini kuna mtu mfano prof shivji ni muasia kwa asilia lakini ana imani na yuko tayari kuipigania TZ mpaka kifo tutamwitaje??
Afande sele akue....

Huyo prof shivji namueshimu sn kwa cv yake iliyotukuka ila alichotufanyia kwenye katiba mpya Mungu amsamehe huenda maslahi yalimpenda zaidi akaweka usomi wake mfukoni
 
MANYWELE PEKUPEKU YUPO SAHIHI KWA FIKRA ZAKE. NI MSALITI MNAKUMBUKA ALIVYOJITANGAZA NI MKENYA KWENYE ONESHO FULANI HUKO MAJUU!?
Hapa alichemka sana na sikuwahi kuamini matango pori aliyotulisha kuwa alikuwa hajui jinachoendelea aseme njaa aka pesa ndo ilimfanya awe hivo
 
Maneno Makali ya AFANDE SELE kutoka Instagram Kwa MRISHO MPOTO na Majibu ya MPOTO kwa AFANDE SELE...

Afande Sele King - Rafiki yangu mkubwa mjomba mpoto kama ni kweli wewe ndio ulikua kinara ktk kusimamia utayarishaji wa wimbo maalumu wa kuhamasisha uzalendo kwa taifa halafu ukashawishi kuondolewa kwa baadhi ya wasanii wazawa ndani ya wimbo huo na badala yake ukampa nafasi rafiki yetu christian bella kushiriki ktk wimbo huo unaowahusu watanzania wkt ukijua wazi kuwa bella pamoja na ukweli ni rafiki yetu sana lkn bado yeye sio mtz bali ni mcongoman....ktk hili mjomba umetukosea sana watanzania wenzako na kwa hakika kama ingekua kitendo chako hicho umekifanya kwa nchi zilizoshiba uzalendo na zisizovaa joho la unafki mjomba ulistahili kukatwa nywele zako na kupigwa risasi angalau tano kichwani kwa uchache tena hadharani kwani ulichofanya ni usaliti kwa nchi yako na ni aina flani ya uhaini...

Majibu

Mrisho Mpoto Akijibu - Kaka yangu @afandeseleking Bado narudia kusema kwamba heshima nnayokupa inatoka Mbali sana kwenye chumba cha nne cha moyo Wangu... Sihitaji kupoteza wino Mwingi kukukumbusha tofauti iliyopo kati ya UZALENDO, UZAWA na URAIA kwasababu nina uhakika unazifahamu vyema isipokuwa huenda leo haujaamkia ule ubavu sahihi na ule wa ukarimu wako ulionao siku zote, mpaka ukakataa uwepo wangu hapa Duniani Kwa kunichagulia adhabu ya kupigwa risasi tano tena za kichwa... kwakua hukuniuliza hili jambo kabla Itoshe kusema hunitaki tena...hivyo basi kabla sijapigwa hizo risasi tano nitakachofanya ni kukupa maelezo machache yatakayokufanya uipate picha ya UZALENDO.. Hivi unajua kama John Okello alipigania uhuru wa Zanzibar!? Majeshi yetu yamepigania uhuru wa msumbiji na hata Chegu sio mcuba na alipigania uhuru wa Cuba na Congo pia.. Na je unajua kama kuna wazawa wanaoangamiza maslahi ya nchi na kuna wazalendo wasiobagua!? Kaka, Afrika ni moja na waafrika wote ni ndugu zetu ( umajumui Afrika, tena ukichimba huko sana kwa hapa nchini utakuna na Prof Shivji) .. na ndio maana hata mwenge wa uhuru uliwekwa juu ya mlima kilimanjaro ili kumulikia nchi nyingine.. Kumbuka hiyo mitizamo ya KIUZAWA Mwalimu aliita mitizamo membamba.. kwa maana ya kwamba ipo kwa ajili ya Kuiangamiza afrika

Na mwisho ningependa kukuuliza--->Je umezisikia shangwe za wazalendo na wazawa leo hapa dodoma baada ya kusikia Babu Seya na familia yake wamepewa msamaha wa rais!!? Wewe ni RASTA kaka.. kumbuka siku zote CHUKI HUMUUMIZA ANAYEIHIFADHI.. [HASHTAG]#AfrikaUnite[/HASHTAG] ✊


Nani yupo sahihi kati ya hawa mafahari wawili?
Je kuwa Mzalendo ni lazima uwe mzawa wa nchi husika?

Haya masanii yote ni ya ccm bei zao zinajulikana corridor za lumumba
 
Ni ngumu sana kutofautisha uzalendo na asili ya mtu
 
Christian bella ametoa mchango mkubwa kwenye tasnia ya muziki nchini kuliko huyo bwana sele
 
Reading from here, Mpoto ameijibu vzr! Watanzania wenyewe baadhi c wa nchi hii kiuhalisia.

My dad ni wa mashariki ya kati, but I am a Tanzanian die hard! Am I not mzalendo kwa defn ya Sele?
 
wote ni marasta wala nyama, ndo maana wanabishana, kisa utofauti wa siasa na vyama, hawatoacha kulumbana
 
Mkuu kwnye hili naomba nipingane na wewe unless kama umeanza kusikiliza mziki miaka ya 2012
Nimeanza kumsikia sele wakati wacha kupiga mayowe inatoka.kwenye chorus inasikika sauti ya jay moo.hakuna kipya alichokileta kwenye game.maudhui ya nyimbo zake nyingi ni kukosoa wasanii wenzie.hata wewe nkikuuliza unitajie nyimbo kali ya bwana msindi aliyowahi imba peke yake bila kumshirikisha msanii mwengine sijui utanitajia wimbo upi.


The nigga was/is overated na ufalme wa rhymes feki wa gazeti la udaku.hivi kweli jamaaa anaweza kuwekwa kwenye kundi la washairi kweli?.kwa punchlines zipi,flow ipi,metaphors zipi,wordplay ipi,vina vipi?.
 
Mrisho ni bonge la mnafiki ondoa maneno yasio na tija TENA kwenye uzani hayafiki haya robo gram unajitetea kwa unafiki uliotenda hatuwezi kukuelewa labda ukamueleze mwanao nae ata itika na sio kukubali
 
Huwezi waacha wasanii wazawa ukawachukua wageni huo ni unafiki.

Sele yupo sahihi 100%.
 
Nimeanza kumsikia sele wakati wacha kupiga mayowe inatoka.kwenye chorus inasikika sauti ya jay moo.hakuna kipya alichokileta kwenye game.maudhui ya nyimbo zake nyingi ni kukosoa wasanii wenzie.hata wewe nkikuuliza unitajie nyimbo kali ya bwana msindi aliyowahi imba peke yake bila kumshirikisha msanii mwengine sijui utanitajia wimbo upi.


The nigga was/is overated na ufalme wa rhymes feki wa gazeti la udaku.hivi kweli jamaaa anaweza kuwekwa kwenye kundi la washairi kweli?.kwa punchlines zipi,flow ipi,metaphors zipi,wordplay ipi,vina vipi?.
Nachokiona mkuu humkubali Sele, lakini naamini kama kweli tunaangalia watu ambao wameweka msingi wa huu mziki wa bongo jamaa naye hatuwezi kudharau mchango wake. Ni kweli jamaa hakuwa na sauti nzuri ya kuimba chorus kiasi ilibidi ashirikishe watu wa kumuimbia chorus. Jamaa ana heat song nyingi; ukiachana na hiyo mayowe kuna mkuki moyoni, mtu na pesa, darubini kali, dini tumeletewa, mtazamo, uwanja mpya, karata dume, ndugu zangu,usinichukie et al, zote hizo zilileta changamoto.

Bella ni mwanamziki mzuri lakini kusema Bella ana mchango mkubwa kwa muziki wa bongo kumzidi Msindi sidhani kama ni sawa. (Mleta uzi atatusamehe kwa kuingiza uzi wetu ndani ya uzi wake)
 
Nimeanza kumsikia sele wakati wacha kupiga mayowe inatoka.kwenye chorus inasikika sauti ya jay moo.hakuna kipya alichokileta kwenye game.maudhui ya nyimbo zake nyingi ni kukosoa wasanii wenzie.hata wewe nkikuuliza unitajie nyimbo kali ya bwana msindi aliyowahi imba peke yake bila kumshirikisha msanii mwengine sijui utanitajia wimbo upi.


The nigga was/is overated na ufalme wa rhymes feki wa gazeti la udaku.hivi kweli jamaaa anaweza kuwekwa kwenye kundi la washairi kweli?.kwa punchlines zipi,flow ipi,metaphors zipi,wordplay ipi,vina vipi?.


Binafsi naiona chuki tu hapa
 
Mabishano yote yapo juu ya jambo la kijinga hivyo wote wajinga tu.
 
Back
Top Bottom