Nani yupo sahihi,Afande Sele au Mrisho Mpoto?

Nani yupo sahihi,Afande Sele au Mrisho Mpoto?

Maneno meeeeengi na ngonjera hakuondoi definition ya Uzalendo.

patriotism
ˈpeɪtrɪətɪz(ə)m/
noun
noun: patriotism
the quality of being patriotic; vigorous support for one's country

Huwezi kuwa mzalendo kwa nchi isiyo yako. Askari wetu kwepo Congo, hakumaanishi wao ni Wazalendo wa DRC, NO. Christian Bella anaweza kuipenda Tanzania, lakini hawezi kuwa mzalendo kwa nchi yetu. Hawezi kuipigania Tanzania dhidi ya nchi yake, na hapo ndio maana ya uzalendo inapatikana.
 
Nachokiona mkuu humkubali Sele, lakini naamini kama kweli tunaangalia watu ambao wameweka msingi wa huu mziki wa bongo jamaa naye hatuwezi kudharau mchango wake. Ni kweli jamaa hakuwa na sauti nzuri ya kuimba chorus kiasi ilibidi ashirikishe watu wa kumuimbia chorus. Jamaa ana heat song nyingi; ukiachana na hiyo mayowe kuna mkuki moyoni, mtu na pesa, darubini kali, dini tumeletewa, mtazamo, uwanja mpya, karata dume, ndugu zangu,usinichukie et al, zote hizo zilileta changamoto.

Bella ni mwanamziki mzuri lakini kusema Bella ana mchango mkubwa kwa muziki wa bongo kumzidi Msindi sidhani kama ni sawa. (Mleta uzi atatusamehe kwa kuingiza uzi wetu ndani ya uzi wake)
Mkuu hujanijibu bado .nitajie wimbo wa afande sele wa peke yake mkali/uliohit ambao hata leo unaweza ukausikiliza na ukakukonga moyo.
 
Uzalendo ni kuipenda NCHI yako na kuiunga mkono siku zote wakati wowote, pia ni kuiunga mkono SERIKALI yako kwenye mambo ya maana.

Kuiunga mkono serikali muda wowote sio uzalendo hata kidogo. Kuikosoa pale inapokengeuka ni moja ya majukumu ya mzalendo.
 
Maneno Makali ya AFANDE SELE kutoka Instagram Kwa MRISHO MPOTO na Majibu ya MPOTO kwa AFANDE SELE...

Afande Sele King - Rafiki yangu mkubwa mjomba mpoto kama ni kweli wewe ndio ulikua kinara ktk kusimamia utayarishaji wa wimbo maalumu wa kuhamasisha uzalendo kwa taifa halafu ukashawishi kuondolewa kwa baadhi ya wasanii wazawa ndani ya wimbo huo na badala yake ukampa nafasi rafiki yetu christian bella kushiriki ktk wimbo huo unaowahusu watanzania wkt ukijua wazi kuwa bella pamoja na ukweli ni rafiki yetu sana lkn bado yeye sio mtz bali ni mcongoman....ktk hili mjomba umetukosea sana watanzania wenzako na kwa hakika kama ingekua kitendo chako hicho umekifanya kwa nchi zilizoshiba uzalendo na zisizovaa joho la unafki mjomba ulistahili kukatwa nywele zako na kupigwa risasi angalau tano kichwani kwa uchache tena hadharani kwani ulichofanya ni usaliti kwa nchi yako na ni aina flani ya uhaini...

Majibu

Mrisho Mpoto Akijibu - Kaka yangu @afandeseleking Bado narudia kusema kwamba heshima nnayokupa inatoka Mbali sana kwenye chumba cha nne cha moyo Wangu... Sihitaji kupoteza wino Mwingi kukukumbusha tofauti iliyopo kati ya UZALENDO, UZAWA na URAIA kwasababu nina uhakika unazifahamu vyema isipokuwa huenda leo haujaamkia ule ubavu sahihi na ule wa ukarimu wako ulionao siku zote, mpaka ukakataa uwepo wangu hapa Duniani Kwa kunichagulia adhabu ya kupigwa risasi tano tena za kichwa... kwakua hukuniuliza hili jambo kabla Itoshe kusema hunitaki tena...hivyo basi kabla sijapigwa hizo risasi tano nitakachofanya ni kukupa maelezo machache yatakayokufanya uipate picha ya UZALENDO.. Hivi unajua kama John Okello alipigania uhuru wa Zanzibar!? Majeshi yetu yamepigania uhuru wa msumbiji na hata Chegu sio mcuba na alipigania uhuru wa Cuba na Congo pia.. Na je unajua kama kuna wazawa wanaoangamiza maslahi ya nchi na kuna wazalendo wasiobagua!? Kaka, Afrika ni moja na waafrika wote ni ndugu zetu ( umajumui Afrika, tena ukichimba huko sana kwa hapa nchini utakuna na Prof Shivji) .. na ndio maana hata mwenge wa uhuru uliwekwa juu ya mlima kilimanjaro ili kumulikia nchi nyingine.. Kumbuka hiyo mitizamo ya KIUZAWA Mwalimu aliita mitizamo membamba.. kwa maana ya kwamba ipo kwa ajili ya Kuiangamiza afrika

Na mwisho ningependa kukuuliza--->Je umezisikia shangwe za wazalendo na wazawa leo hapa dodoma baada ya kusikia Babu Seya na familia yake wamepewa msamaha wa rais!!? Wewe ni RASTA kaka.. kumbuka siku zote CHUKI HUMUUMIZA ANAYEIHIFADHI.. [HASHTAG]#AfrikaUnite[/HASHTAG] ✊


Nani yupo sahihi kati ya hawa mafahari wawili?
Je kuwa Mzalendo ni lazima uwe mzawa wa nchi husika?
ni kwel uzawa co hoja lakini inauma Kuwaacha wazawa sababu ni nyimbo ya Tanzania na co Africa
 
Mimi ni Adui no.1 wa Sera za ccm, Lakini kwa Hii LA uzalendo na maana halisi ya Uzalendo Mpoto Ameongozwa na Akili kubwa na Hekima ya Hali ya Juu sana Huyo Afande nadhani Bangi zimemuathiri sana, Uzalendo Ingekuwa ni uzawa Leo Tusingepeleka Askari wetu Kongo tungewaacha wakongo wauane wao kwa wao Uzalendo ni zaidi ya uzawa
 
Watunge wimbo wabishanie kwenye wimbo... Ila nawaza, kuna msanii wa Tanzania anayeishi nje ya nchi ataruhusiwa kuimba wimbo wa kuhamasisha uzalendo kwenye nchi hiyo?

Let us assume bwana "Harmorapa" anaishi Kigali Rwanda, atashirikishwa kwenye wimbo wa uzalendo wa wanyarwanda?
Hiyo inategemea na wasanii wa nchi husika
 
kama ni kuhamasisha uzalendo kwa Taifa ..basi ni vema wazawa wawe kipaumbele lakin yote 9 .......10 mbona sioni kama ni sahihi kwa hawa watu tena watanzania kujibishana kwenye mitandao ya kijamii.Mbona wanaweza kuwasiliana private na wakarekebishana mitazamo yao pasipo kuleta picha ya kutoelewana baina yao..ushauri wangu tu kwao wawe watulivu...wakutane wawili wawekane sawa .......
 
Maneno meeeeengi na ngonjera hakuondoi definition ya Uzalendo.

patriotism
ˈpeɪtrɪətɪz(ə)m/
noun
noun: patriotism
the quality of being patriotic; vigorous support for one's country

Huwezi kuwa mzalendo kwa nchi isiyo yako. Askari wetu kwepo Congo, hakumaanishi wao ni Wazalendo wa DRC, NO. Christian Bella anaweza kuipenda Tanzania, lakini hawezi kuwa mzalendo kwa nchi yetu. Hawezi kuipigania Tanzania dhidi ya nchi yake, na hapo ndio maana ya uzalendo inapatikana.
Hapa umenena mkuu nasubilia mwingine aniweke sawa maana😵😵😵😵
 
Mpoto yuko sawa sana hii dhana ya uzawa iko kwa nchi maskini sana pia inachangiwa sana na ubinafsi uliokubuhu kama jambo linafanyika kwa maslah mapana ya nchi hakuna haja yakuangalia ni nan anayelifanya ndio maana kwenye jesh la marekan kunawapare kibao mpaka wamatengo tukija kwenye soka ufaransa ni mfano tosha na balaa lake wote tunalijua namaliza kwakusema afande mbinafsi kwa kiwango cha kawaida kabisa
Kuna kipindi wamarekani walitaka Obama asichaguliwe kwa sababu sio Mmarekani.
Hapa unasemaje!
 
Mrisho amejikita kwa pfof Shivji na mifano ya kina Okello katika kuonyesha uzalebdo. Lkn bado mjadala unaweza kuendelea kwamba ni kweli wazawa wameshindwa kuwa wazalendo mpaka wapatikane wageni? Mie namuona Mrisho amekimbia hoja ya msingi hapa. Katuhumiwa kumtowa mzawa na kumuingiza mgeni je kafanya kweli hivyo au hakufanya? Badae ndio tuendelee na ngonjera za kina Okello.
 
braza mbona mgumu kuelewa, wamerekani asili ni watu kama millioni 5 tu huku 98% ni wahamiaji kule hivyo kusema kila sekta itashikwa na wazawa ni uongo.

sasa kuendelea kunipa mfano toka marekani unapoteza muda maana kule karibu wote ni wahamiaji

je huku kwetu hali ikoje, kwa nini umuondoe mtanzania na kumpa mgeni(umeupimaje uzalendo wake)

Sawa mkuu kama marekan wenyeji ni red indians pekee sisi hapa kwetu wangoni wametoka south,wamasai ethiopia,pia kuna wamalawi,waha wamtoka burund wahaya uganda wamakonde msumbiji tunawajaluo pia uzawa ni ubinafsi na ubaguz nasisitiza fatilia historia ya africa na historia ya wabantu sis hatuna tofaut na marekan
 
Mimi ni Adui no.1 wa Sera za ccm, Lakini kwa Hii LA uzalendo na maana halisi ya Uzalendo Mpoto Ameongozwa na Akili kubwa na Hekima ya Hali ya Juu sana Huyo Afande nadhani Bangi zimemuathiri sana, Uzalendo Ingekuwa ni uzawa Leo Tusingepeleka Askari wetu Kongo tungewaacha wakongo wauane wao kwa wao Uzalendo ni zaidi ya uzawa
Totally wrong, wewe na huyo Mrusha Mpotoshaji. Askari wetu walioko DRC sio Wazalendo wa DRC. Wapo pale kazini tu. Amiri Jeshi wao ni Rais wetu na sio Rais wa Congo. Leo hii Congo wakitukorofisha, hawatapigana upande wa Congo, watakuwa upande wetu kuonesha uzalendo kwa nchi yao.

Huwezi kuwa Mzalendo kwa nchi ya mwenzio, unless you are stupid, lkn unaweza kuipenda nchi nyingine.
 
Kuna kipindi wamarekani walitaka Obama asichaguliwe kwa sababu sio Mmarekani.
Hapa unasemaje!
Hio ilikua hoja ya kisiasa tu ndio maana walimpa mihula miwili they dond give a damn about where you come from ila utafanyanin?
 
kwahicho alichokijibu mpoto nahoja za ushahidi wake alizozitoa nampa..tano katisha
nampnda afande sele yule mwenye mitazamo chanya wakipindi cha mkuki moyoni...lakini hapa amefeli..hata Michael Jackson alimuimbia msichna wakiliberia wimbo nakuitukuza Liberia sio kwamba America ilikuwa imeishiwa warembo...Bob Marley nae alituasa Africa kuungana nakuwa kitu kimoja sio kwamba yeye alikuwa niraia wkutoka Africa..tena akashindilia msumari wamwisho kuipamba Zimbabwe ktk tungo zake murua...
afande sele alikuwa sahihi alipotoa mtazamo wake juu ya kanumba dhidi ya lulu...
ila hayupo sahihi ktk hili ..yeye anajuaje labda Bella tayari keshapewa uraia wanchi hii..

then unapokuwa nahekima nabusara kunamambo mengine unastahiki kuynyamanzia kimya hata kama nimabaya.. lakini kwakuwa haywezi kukudhuru hugeuka nakuwa sawa najema lisilo nafaida
 
Mkuu hujanijibu bado .nitajie wimbo wa afande sele wa peke yake mkali/uliohit ambao hata leo unaweza ukausikiliza na ukakukonga moyo.
watu na Pesa ..mkuu nibonge ya ngoma..
 
MPOTO YUKO SAHIHI ILA KWA TAHADHARI



KWA MFANO
IKITOKEA MGONGANO WA MASLAHI KATI YA DRC NA TZ, CHRISTIAN BELA ATAKUWA TAYARI KUTUMWA NA DRC DHIDI YA TZ ILA HAWEZ KUTUMWA NA TZ DHDI YA DRC.

NADHANI NIMEELEWEKA
 
Back
Top Bottom