Nani Zaid? Mpina, Lisu, Lema...!

Nani Zaid? Mpina, Lisu, Lema...!

Head teacher

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2012
Posts
1,796
Reaction score
412
Ukiniuliza nani anafaa kuwa rais wa Tanzania 2015 nitasema ama Mpina, au Lisu,au Lema. Nawatazama viongozi hawa vijana kama alama ya mabadiliko kwa ustawi wa taifa letu. Viongozi hawa wapo wazi na wala hawana chembe ya unafiki. Ujasiri wao ndani na nje yabunge naweza kuiita ni asilia (in-born), si kama baadhi ya viongozi wengine vijana ambao wana ujasiri wa kutengezezwa. Mfano wa hawa ni Makamba Jr, Mnyika, Filikunjombe, n.k... Kwa upande wangu ningefurahi kama Mpina atakuwa rais wa Tanzania. Naona wivu sana nikiangalia safu ya viongozi wakuu wa Kenya, akina Uhuru, Rutto, nk wote vijana. Kwanini hapa Tanzania tuendelee kung'ang'ania kuongozwa na wazee kama Kikwete, Slaa, Lowasa, Membe, Sita, Wasira! Tumekosa nini sisi vijana?
 
Lissu ana akili saana. Lema ni jasiri saana. Mpina ni mnafiki
 
We wa wapi wewe? Mpina ndo amekutuma uje upime hapa kama anakubalika? Huyo huwezi kumweka kundi 1 na hao makamanda ni mnafiki wa kutupwa!
 
We muamiaji haramu,nani kakuruhusu kujiita head teacher alafu unapima kina cha maji kwa miguu yote miwili?
Usijaribu tena kumlinganisha au kumweka pamoja kamanda wetu yeyote yule na gamba lolote.Gamba ni gamba hata kama ni la mbu!
Isitoshe watz tunaye rais wetu wa moyoni anaitwa DR.W.P.SLAA(2015 na kuendelea) chomoa MPINI wako kina Lema,Lissu hapana gamba lolote la kulinganishwa/kufananishwa nao.
 
Teh teh, umeona utumie kete ya vijana, any way nadhani wote wana sifa za kuchaguliwa, hata yule aliyewahonga vijana wa vyuo vikuu simu ili ionekana kwamba anakubalika!
 
Back
Top Bottom