Naomba elimu kuhusiana na sheria inayohusika na maswala ya madai (haswaa mikopo)

nerilan

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2013
Posts
454
Reaction score
691
Habari zenu wanajukwaa. ..

Kama kichwa hapo juu kilivyo, ningeomba utaalamu wenu katika jambo hili ili nami niweze kuelewa vizuri..


Pindi mtu anapoingia mkataba wa mkopo, akaanza kulipa lakini kwa namna yoyote ile akashindwa endelea kulipa katikati ya urejeshwaji wa mkopo, sheria inazungumza nini kuhusu mtu huyu?, je sheria inaruhusu mkopeshaji kuuza dhamana za mkopaji hata kama muda wa mkataba haujaisha na bila kutoa notice ya maandishi kwa mdaiwa?.. Naomba tuanzie hapo kwanza......

Shukrani
 
Kutokana na maelezo yako,chanzo cha madai yako/hayo yanatokana na mkataba.Hivyo itategemea kwanza mkataba wako unasemaje juu ya malipo na juu ya dhamana.Madai ya kimkataba huanzia kwenye mkataba wenyewe.

Kwa ziada tu, ''mortgage is always a mortgage '' hii ina maana kuwa dhamana ya mkopo itaendelea kuwa dhamana na si vinginevyo.Dhamana haimaanishi kuhamisha umiliki wa mali iliyowekwa dhamana kwenda kwa Mkopeshaji.Lengo la dhamana ni kulinda mkopo.Hivyo ni lazima mkopaji awe ameshindwa kabisa kulipa mkopo husika na ni lazima muda wa mkopo kwa mujibu wa mkataba uwe umekwisha na kwa kifupi mkopaji awe ameshindwa kulipa deni ndipo utakuwa na haki ya kupiga mnada mali iliyowekwa dhamana baada ya kumtaarifu mkopaji au kwa amri ya Mahakama.
 



Asante sana kwa maelezo mkuu. Vipi kama mkataba umeainisha kuwa endapo mkopaji atashindwa rejesha hata rejesho moja basi mali uake itapigwa mnada?, pia inakuwaje endapo mkopaji akawa kaondoka/katoroka bila kutoa taarifa kwa mkopeshaji alikokwenda?, hii ina mpa haki gani mkopeshaji kuhusiana na mkopo aliokopesha na dhamana kwa ujumla?.. Ataruhusiwa kuinadi dhamana hiyo in absence ya mkopaji?
 

Mkataba ni zao la matakwa ya wahusika katika mkataba na Mahakama kazi yake ni kutafsiri malengo ya wahusika na kulinda maslahi yao ndani ya mkataba.

Hata hivyo,Mahakama katika kutafsiri Mkataba inatikiwa kuzingatia sheria za nchi,taratibu na kanuni za kisheria zinazojulikana.

Hata hivyo ndani ya mkataba kunaweza kuwepo na kipengele ambacho kwa taathira yake kina maana kubwa zaidi ya ile inayoonekana wazi.

Nirudi kwenye maswali yako.
(1) Hapo awali nilisema kuwa lengo la dhamana si kuhamisha umiliki wamali ya mkopaji kwenda kwa mkopeshaji bali lengo ni kulinda mkopo.Hii ni kanuni ya kisheria inayotawala mambo ya mikopo inayoambatana na dhamana (Mortgage ).Kanuni hii haipo kwa ajili ya kuzuia haki za Mkopeshaji lakini ipo kwa ajili ya kulinda dhamana.

Dhamana inatakiwa kuuzwa baada ya mkopaji kushindwa kulipa mkopo,hii ina maana tarehe ya mwisho ya kulipa mkopo inaweza kuzingatiwa na Mahakama katika kutoa amri ya kupiga mnada dhamana.

(2)Hakuna sheria inayomzuia mkopaji kwenda kokote atakako na wala hatakiwi kumuomba ruhusa au kumtaarifu Mkopeshaji mahali anapokwenda,dhamana yake ndiyo ulinzi wa Mkopeshaji.

No consultation fee
 


Hapo nomekuelewa vizuri mkuu, shukrani
 
mm nina mpango wa kuwa na kampuni ya mikopo unaweza ukanitumia namna mkataba ya mikopo inavyotakiwa Kuwa??? email. sisacosmas gmail.com
 
huo mkopo ni wa riba, na je mlipeana tu au kuna kitu kiliwekwa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…