Naomba hili lililojitokeza Uwanja wa Ndege wa Entebbe lisije likajitokeza JNIA

Naomba hili lililojitokeza Uwanja wa Ndege wa Entebbe lisije likajitokeza JNIA

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Abiria wanaosafiri kwenda nchi za nje kupitia Uwanja wa Ndege wa Entebbe nchini Uganda wamelalamika vitendo vya wafanyakazi wa Uhamiaji kuwalazimisha watoe hela (chochote kitu) pale wakiwa wanaelekea kupanda ndege hali inayosababisha wengine kuchelewa ndege na wengine kuchelewesha ndege kuanza safari yake kwa wakati.

Taarifa: BBC Swahili

Yaani kabisa GENTAMYCINE nimejichangachanga weeee na huu umasikini wangu na nikapata nauli ya kwenda kubeba maboksi kwa Biden (Marekani) halafu nipo JNIA abiria tunatakiwa kwenda, sasa ndani ya ndege mfanyakazi wa Uhamiaji Tanzania ananizuia kuwa siwezi kuingia ndani ya bung'o (ndege) mpaka nimtoe kwanza na hela?

Na hivi nilivyo na Mkanda Mweusi wa Kung Fu halafu nafundisha ndondi mabondia mbalimbali uswahilini ambao hata Mwakinyo na Mandonga wanawaogopa kupambana nao, ukinizuia tu kama walivyofanyiwa abiria wa Entebbe Airport nchini Uganda jua utayaanza maisha yako rasmi ama ICU Muhimbili au katika friji za wodi namba 26 (mortuary) ya Muhimbili National Hospital. Kudadadeki!
 
Sawa
Weka picha tukuone ukiruka hayo mateke na mkanda wako mweusi
 
Sawa
Weka picha tukuone ukiruka hayo mateke na mkanda wako mweusi
Hana lolote huyu nyauba anakaa kawe ukwamani, kapanga nyumba ya mzee mapupu! Hana maana..anakopa balimi Open Air na company yake kubwa ni Dkt Komba mtoa mimba maarufu[emoji23][emoji23] namsubiri aje!
 
Mwaka fulani nilikuwa nasafiri na bus la spider kwenda Zimbabwe tumefika border ya Zambia na Zimbabwe Chirundu, konda wa bus (Spider bus)akatangaza kila mtu awake Randi 100 kwenye passport bila hivyo uvuki border niligoma kutoa
 
Back
Top Bottom