Kuna aina mbili, tuanze na ya kupika.
Mahitaji
Mbilimbi
Nyanya
Kitunguu
Kitunguu saum
Tangawizi
Pilipili
Chumvi
Binzari ya njano
Hapa osha mbilimbi zako, tia chumvi na uzichemshe.
Zikiiva zichuje maji kisha ziweke kwenye maji baridi na uanze kuzitoa Moyo (vile vikamba vya ndani) huwa vina ukakasi.
Pembeni andaa pilipili, kitunguu saumu, tangawizi kiasi, kitunguu maji, nyanya kiasi na binzari ya njano (tumeric powder)
Visage vyote au katakata na upashe mafuta uviweke jikoni...
Mchanganyiko wa nyanya ukiiva weka zile mbilimbi ulizochemsha, vichanganye vizuri.
Ikiiva epua tayari Kwa kuitumia, unaweza Kula na mihogo, ugali, chipsi nk