Naomba kuelimishwa juu ya sizes za viwanja (plots)

bwegebwege

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2010
Posts
1,072
Reaction score
186
Wakuu, habari za weekend.

Naomba kuelimishwa kidogo:

  1. Hivi hadi kiwanja kiwe classified kama either LOW DENSITY, MEDIUM DESNITY au HIGH DENSITY kinatakiwa kuwa na VIPIMO (sqm) zipi?
  2. Napata wapi TABLE/SCHEDULE inayooonesha sizes mbalimbali za viwanja?
Naombeni kuelimishwa
 
0-600 sqm Hight density
600- 1200 sqm Mediuam Density
1200 + Low Density

Hiv ndivyo nijuavyo mimi, wengine watakuelewesha zaid
 
Na hii tofauti inanuia nini....yaani ni kwanini wana vi classify kwa hizo densities
0-600 sqm Hight density
600- 1200 sqm Mediuam Density
1200 + Low Density

Hiv ndivyo nijuavyo mimi, wengine watakuelewesha zaid
 
Na hii tofauti inanuia nini....yaani ni kwanini wana vi classify kwa hizo densities
Kma utakua umesoma geography , density inapima mkusanyiko wa watu, so kua low density inamaana mkusanyiko wa watu ni mdogo, then high, mkusanyiko ni mkubwa,
Mfano kiwanja cha sqm 1400 ambacho anaishi mtu mmoja mbezi beach ( low density), ukija magomeni kagera, tandale kwa tumbo, vingunguti kwa mnyaman au popote uswahilini , ni makazi ya watu kumi au zaidi( high density) ata ukiangusha kijiko jiran anasikia.
Hope nimejaribu kukuelewesha
 
Umemaliza Kiongozi
 
Kwanini waliopima viwanja masaki, Osterbay, mikocheni, mbezi beach, wasingepima kwa vipimo ivyo ivyo kwa maeneo ya sinza kijitonyama magomeni manzese au kuna mtu alizembea maeneo ayo?
 
Kwanini waliopima viwanja masaki, Osterbay, mikocheni, mbezi beach, wasingepima kwa vipimo ivyo ivyo kwa maeneo ya sinza kijitonyama magomeni manzese au kuna mtu alizembea maeneo ayo?
una hela ya kununua kiwanja icho ? Au unataka wenye uwezo huo waishi na waswahili wakeshea vigodoro ?
 
Nimekuelewa, sikujua kama density hii ina apply kwenye eneo hilo
 
una hela ya kununua kiwanja icho ? Au unataka wenye uwezo huo waishi na waswahili wakeshea vigodoro ?
Kwa enzi za dhamani wazee wetu wange weza kinunua kama waliweza kununua maeneo mengi tu mjini kwa miaka iyo wangeweza tu kwa maana avikuwa bei kubwa , yan wangejitaid kuvipima ata nusu tu ya ukubwa wa Viwanja vya osterbay naamin sinza kijitonyama manzese kungekuwa kuzur sana.
 
Asante kwa somo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…