Wadau,
Kwa unyenyekevu naomba kufahamishwa kwa mtu yeyote anayejua shule yoyote ya msingi ya Kikristo iliyoko katika maeneo ya Goba, Mbezi au Madale, Kunduchi, au Mbezi Beach. Kama unafahamu shule ya namna hii iliyoko eneo lolote jingine Dar es Salaam. Naomba pia kufahamishwa ingawa kipaumbele ni maeneo niliyoyataja.
Ninaposema shule ya Kikristo namaanisha shule ambayo inaweka msisitizo kwa watoto kujifunza masomo ya kawaida lakini pia na neno la Mungu, ikiweka msingi kuwa mtoto anahitaji kulelewa katika maadili ya kibiblia na kufundishwa kulishika na kuliishi neno la Mungu. Kipaumbele ni shule ambazo zinafuata mfumo wa Tanzania wa NECTA, lakini kama zipi zinzofuata mfumo au mtaala wowote mwingine itakuwa vema pia kuzifahamu.
Wenzetu Kenya wana shule kama hizi hapa chini, itakuwa vema kufahamu kama kuna shule za namna hii hapa kwetu Tanzania.
Thika Road Christian School , Curriculum
Jabali Christian Schools , Home
Natanguliza Shukrani
Kwa unyenyekevu naomba kufahamishwa kwa mtu yeyote anayejua shule yoyote ya msingi ya Kikristo iliyoko katika maeneo ya Goba, Mbezi au Madale, Kunduchi, au Mbezi Beach. Kama unafahamu shule ya namna hii iliyoko eneo lolote jingine Dar es Salaam. Naomba pia kufahamishwa ingawa kipaumbele ni maeneo niliyoyataja.
Ninaposema shule ya Kikristo namaanisha shule ambayo inaweka msisitizo kwa watoto kujifunza masomo ya kawaida lakini pia na neno la Mungu, ikiweka msingi kuwa mtoto anahitaji kulelewa katika maadili ya kibiblia na kufundishwa kulishika na kuliishi neno la Mungu. Kipaumbele ni shule ambazo zinafuata mfumo wa Tanzania wa NECTA, lakini kama zipi zinzofuata mfumo au mtaala wowote mwingine itakuwa vema pia kuzifahamu.
Wenzetu Kenya wana shule kama hizi hapa chini, itakuwa vema kufahamu kama kuna shule za namna hii hapa kwetu Tanzania.
Thika Road Christian School , Curriculum
Jabali Christian Schools , Home
Natanguliza Shukrani