ENANTIOMER
JF-Expert Member
- Sep 22, 2014
- 1,419
- 804
Jaman naomba kufahamishwa kwa wale ambao wapo kwenye sekta ya elimu (walimu)kwa sasa mishara kwa level ya cheti, stashada na shahada ni kiasi gani kwa maana mm pia najiaanda kuwa mwalim.
kwakua unataka kuwa mwalimu na umeshapata data juu wa udogo wa mshahara, basi unatakiwa kujipanga ili usizeeke ukiwa na hali mbaya.
Fahamu ya kwamba, hata secta zetu (secta nyingine) ni siri yao tu. Hata kwetu hali sio nzuri. Ila kwa uchache watu, ndio maana kilio chatu hakina sauti kama cha walimu.
Pengine tunafanya kazi chini ya sheria kali na adhabu ya kupata ajira ikiwa tutatimulia mahali tulipo, ndio sababu ya kuishi kama mabubu.
Kwa kua uko katika utafutaji, basi kufanya kazi zaidi ya moja ni bora zaidi! Ndio maana hata viongozi wa nchi yetu wana vyeo lukuki, wakati huo huo wakifanya biashara mbalimbali.
Vyeo lukuki haina maana kua watu wa kushika nafasi hawapo, bali inamaana kua wao wako katika utafutaji.
Kazi zaidi ya moja ndio mkombozi wa kila mtu!