Naomba kufahamu kuhusu Power Mabula

Panzi Mbishi

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2021
Posts
2,231
Reaction score
2,904
Wakubwa Salaam,
Kama title inavyojieleza, napenda kujua historia ya huyu mwamba aliyetikisa kwa umwamba miaka ya nyuma yuko wapi kwa sasa? Alifariki? Lini? Akiwa na Umri gani?
Kama yupo ana umri gani sasa hivi?


Nakumbuka miaka ya nyuma alikula sana hela za maonyesho ya wazi na ya ndani, ilikuwa uwezo wake binafsi au kuna ziada?

NB: Nahisi huyu jamaa ni masalia ya wanefili
 
Nenda kwenye jukwaa la historia... Utapata majibu yako huko.
 
Niliwahi kumuona akifanya show zake Nyarugusu Geita miaka hiyo wengi humu bado mnanyonya au bado mko katika viuno vya wazazi wenu (1986/7). Alikuwepo na mwingine power Geita lakini alishafariki .

Kwa ujumla sijui aliishia wapi [emoji87][emoji102]

Odhis *
 
Alikuwa na show yake moja, anawekewa jiwe kubwa sana kifuani, (sio Meko). Uzito tu wa like jiwe unakufanya upate korona na ukiwa umeacha kiasi kikubwa sana cha mboji sakafuni.
Akishawekewa jiwe hilo, hutafutwa mtu mwenye nguvu zake, Kisha huanza kulipiga na nyundo kubwa Sana.
Power Mabula alistaafu michezo yake baada ya kwenda Rukwa, sumbawanga, huko alipita mitaani akiwa juu ya Land Rover 109, akionyesha promo.
Kuna mtaa unaitwa Mazwi, akakuta mtoto wa miaka mitano analisukuma Scania na trela lake, akastaabu sana, akauliza baba yako Yuko wapi? Akajibiwa kaenda kuuleta mlima uleeeee, auweke jirani na nyumba yetu
 
[emoji23][emoji23][emoji23]
 
😂😂😂😂😂✌️ pisi en lavu ..
 
Bujibuji bana acha kamba mimi nimesoma jangwani primary school na mazwi secondary school
 
Mkuu Mara ya mwisho kumuona Mimi iliikuwa miaka ya 2000's kama sijakosea,alikuwa kahama -shinyanga katika Kijiji cha Segese,hapo hakuwa tena akifanya viinimacho macho vyake,alikuwa ameokoka na anahubiri neno la bwana,hadi sasa Leo hii sijui yuko wapi
 
mwishoni mwa miaka ya 90 aliwahi kufanya mahojiano na kituo kimoja cha television. sina hakika ni itv au dtv. alieleza historia yake kwa undani.

tembelea studio ya itv au dtv kaulize kuhusu power mabula. nahisi watakuwa na clip zake kwenye library zao.
 
[emoji23][emoji23][emoji23] heshima yako bujibuji
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] khaaaaah lol
 
chai
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…