Jibu ni rahisi sana.
Msanii anapoitwa kwenye interview inategemea ameendaje, mfano, diamond platnumz ameitwa kwenye interview Jana na kituo cha media ni kubwa ambayo ni clouds FM, nikimaanisha kubwa kwa sababu inajulikana karibia afrika ya mashariki na hata Tanzania nzima pekee,
Kwa hiyo anapoitwa ina maana ni bure hawawezi kumlipa wala yeye hatoi pesa, kwa sababu tayari ni msanii mkubwa Mwenye jina kila kona ya bara la afrika ndiyo maana anayo haki ya kufanya maamuzi yafuatayo,
1. Kukataa kwenda kwenye interview.
2. Kuomba kulipwa kiasi kadhaa cha pesa kwenye hiyo interview.
3. Kuomba kuwalipa hao media baada ya interview,
Kulipa interview ni pale msanii anapokuwa mchanga na anahitaji kujulikana kimataifa, au kitaifa ndiyo anaweza kulipa pesa ili afanye interview na nyimbo zipigwe kila mara redioni na runingani,
Ukiona msanii mkubwa ameitwa kwenye interview ujue media wamemkubali na hawatoi pesa yeyote, wala hawamlipi pesa yeyote.
Labda ukute kituo / media haijulikani na wanahitaji kujulikana hapo watamchukua msanii mkubwa wanamlipa wakimchukua msanii mdogo hawamlipi.