Naomba kujua changamoto za kufunga Turbocharger kwenye gari

Dereva Suka

Senior Member
Joined
Sep 25, 2014
Posts
176
Reaction score
289
Wakuu kama uzi unavyojieleza hapo juu ni kweli kabisa napenda sana gari zenye turbo kama vile Subaru au gari ndogo yeyote ambayo imefungwa turbocharger
Tatizo sina uzoefu nazo hasa katika changamoto zake.

Wataalamu au wazoefu wa turbo mnisaidie hapa kama kuna ulazima sana wa kuwa na gari yenye turbo au huwa zinasababisha matatizo gani sana zikifungwa katika gari.

Napenda sana mlio wake ikiwa kwenye Subaru au ikifungwa kwenye Scania Bus mfano kuna basi moja inaitwa Asante Rabi ukikaa karibu na dereva pale utapenda wakati inafungua turbo.

MASWALI MENGINE KUTOKA KWA WADAU:
Turbo inasaidia nini ama ina faida gani kwenye injini?

Na hasara zake ni zipi kwenye injini?

Ni gari yoyote yaweza kufungwa turbo?

-Kaveli-
===
MAONI YALIYOTOLEWA NA WADAU:
-------------
-------------
-------------
-------------
-------------
 
Turbo inafunguka at certain rpm ndio unasikia ule mlio wake, ukiwasha ukatulia gari turbo itakuwa inazunguka with no effects.hata ukiwa unaendesha slow pia turbo itazunguka, ukikamua ndo inafunguka
sio kweli kuwa haina effect. effect ipo hata gari ikiwa haijabinywa sana inakuwa tofaut kidogo na same engine isio na turbo isipokuwa boosting ni kidogo sana na sijui mnavyosema turbo ikifunguka sijui mnamaanisha nini
 
Turbo inasaidia nini ama ina faida gani kwenye injini?

Na hasara zake ni zipi kwenye injini?

Ni gari yoyote yaweza kufungwa turbo?

-Kaveli-
 
sio kweli kuwa aina effect ...effect ipo hata gari ikiwa haijabinywa sana inakuwa tofaut kidogo na same engine isio na turbo ispokuwa boosting ni kidogo sana na sijui mnavosema turbo ikifunguka sijui mnamaanisha nini

Mkuu tatizo wewe si mtu wa magari kiivo itakuwa ndio maana hufahamu maneno turbo ikifunguka. Anyways, ushawahi kusikia kitu Turbo Lag? Hebu ulizia turbo lag kisha njoo unambie kama turbo ikiwa idle au slow driving kuna any perfomance gain.

Turbo inategemea kzungushwa na exhaust gases, gari inapokuwa idling au inapokuwa in lower rpm hio turbo inazunguka mzunguko wa kawaida tu ambao hauna athari katika mashine, lakini unapokanyagia labda ukafika 4000RPM utaanza kusikia mluzi hapo ndio tunasema turbo imefunguka kwa sababu hapo ndio utaona perfomance gain. (inategemea na aina ya turbo inaweza kufunguka 4000rpm au mpaka ifike juu zaidi)
 
Wataalamu wa mambo ya magari, nimeomba kufahamishwa hiyo 'turbo' huwa inasaidia nini kwenye injini? na je ina disadvantages zozote kwenye injini?

Naona mnaruka ruka tu as if hamuoni swali langu.

-Kaveli-
 
Turbo inasaidia nini ama ina faida gani kwenye injini?

Na hasara zake ni zipi kwenye injini?

Ni gari yoyote yaweza kufungwa turbo?

-Kaveli-
turbo inasaidia kuongeza performance ya engine.

haina hasara yoyote kwa engine kama ikifungwa na kuwa maintained vizuri

ndio gari yoyote inaweza fungwa turbo lakini yafaa upate mtaalam wa engine tuning & mapping ili usijeharibu engine kwa (kwa gari ambazo ni naturally aspirated/hazina turbo)
 


Shukrani mkuu.

Inaongeza 'performance' ya engine kwa maana ipi... kwamba gari inakuwa inapata kukimbia (speed) zaidi?

-Kaveli-
 
inategemea na application lakini turbo husaidia acceleration ya gari kuwa kubwa hivyo kuifanya ifikie top speed kwa haraka zaidi


Ahaaa, kwamba injini inachanganya kwa haraka zaidi towards top speed ya gari husika. Ok nimeelewa mkuu.

Mfano kukawa na Vits mbili same model, same engine capacity. Vits X ikafungwa turbo. Vits Y haina turbo.

So hapo mwenye Vits X atamuacha mbio huyo mwenye Vits Y. That's it?

-Kaveli-
 
chilubi,
Mkuu to the best of my mechanics , turbo huwa iko on as long as gari imewashwa , hio lugha ya kusema turbo imefunguka ni ya kimtaani zaidi kuliko kitaalam, ,Kuna magari ya na turbo pressure gauge ,inajieleza vizuri tu hii theory , ni kwamba ukizima gari turbo boost pressure inakuwa zero kpa ,! Na gari ikiwaka inapanda kutegemeana na engine load.

Umezungumzia turbo lag, kimsingi ni tofauti Kati ya normal boost na high boost, haimaanishi kuwa ni turbo on and off , kitaalam unatakiwa kuendesha gari Bila kuhisi turbo lag , ukiwa una fee lag jua unatumia Moto mwingj bila lazima , na trip zako zote zitakua very heavy kwenye diesel consuption.

Lakini pia Kuna Variable geometry turbocharger (vgt), gari Kama iveco stralis , turbo za aina hi zinakua na maximum boost , even at idle.

Mluzi mzuri wa turbo tunaousikia , unamaanisha kuwa turbo inafanya kazi karibu na uwezo wake wa juu kabisa , tunashauriwa Kama una drive economically huo mluzi usiusikie Sana kwa kuwa pump inject mafuta mengi ili iendane na air pressure.
 
Wataalamu wa mambo ya magari, nimeomba kufahamishwa hiyo 'turbo' huwa inasaidia nini kwenye injini? na je ina disadvantages zozote kwenye injini?

Naona mnaruka ruka tu as if hamuoni swali langu.

-Kaveli-
Gari zote huwa zinategemea vacuum inayojitengeneza kwenye engine ili kuvuta hewa.. Jambo hili kwa kuwa ni tendo la hiyari basi hewa huchelewa kujaa kwenye engine kitendo kinachosababisha gari kuwa na guvu kidogo.. Turbo ni pampu inayozungushwa na moshi wa injini kujaza hewa safi kwenye injini na kulazimisha mlipuko wa ndani wa haraka...
 
t blj,

Mkuu hakuna mahala nimesema kuwa eti turbo inakuwa imezima. gari ukiwasha turbo inazunguka lakini mzunguko wake hauleti effect ya kuingiza more air in the car, kutegemeana na aina ya turbo inahitajika pressure kutoka exhaust gases ili kufanya mzunguko wenye kuleta athari. Turbo kufunguka maanake sasa engine inapata more air and more fuel for boost. To the best of your mechanics nategemea utakuwa unatambua kuw kwenye kila rpm kuna difference ya mafuta na air pumped into the engine na pia kunakuwa na different HP measurement kwenye hizo rpm, mfano ukitazama specs za gari labda tuseme Subaru forester, katika spec sheet yake utaona kitu 240HP @ 6500 rpm, maanake ikifika 6500 rpm gari hio inakuwa na 240 hp, na ukiwa katika may be 3000 rpm, huna 240 HP. Na turbo nayo ikifika certain RPM ndio inaleta difference.

Turbo Lag: This is the time between the demand for an increase in power (the throttle being opened) and the turbocharger(s) providing increased intake pressure, and hence increased power. Throttle lag occurs because turbochargers rely on the buildup of exhaust gas pressure to drive the turbine.

Hio ndio maana ya turbo lag sasa, nafikiri utapata picha tunaposema kuwa inafunguka, na imetulia. Hakuna mahala nimesema kuwa eti inakuwa off, nimesema inakuwa with no effect! Kutokana na maana hio, ndio tunasema turbo haijafunguka inapokuwa kwenye low RPM kwa sababu the spinning of turbo wheel is not enough to make an effect. Nakubaliana na wewe uliposema kuwa inapolia inakuwa katika its peak power, na mostly inakuwa at higher RPMS

Kuhusu hio Turbo boost pressure ndo kama nlivosema kuwa, gari ikikaa on turbo inazunguka kama kawaida, isipokuwa turbo itahitaji ukanyage ndio iwe na effect.

Je unajua Turbo Anti Lag? Hii ni system ambayo imewekwa kueliminate hio turbo lag, kuifanya turbo wheel kuspin hata kama engine haina nguvu ya kutosha ya kuzungusha hio wheel.

Labda kwa kutoa mfano mwengine, wenye Honda Vtec engines wanapokamua wakifika top rpms wanakwambia "Vtec Kick In", haimaanishi kuwa vtec ilikuwa haifanyi kazi kabla haja push it to the limit, vtec ilikuwa wazi lakini effect yake inaonekana unapoipush to the limit.
 
chilubi,

Mkuu ,
Tunapishana padogo Sana , inaonekaka uko deep Sana , ila Kuna baadhi ya dhana umekua miss informed, tuchukulie tu huo mfano wako wa prm to power graph ya subaru, hebu niambie hiyo power ya 240hp inaanza ghafla bin vuu? Si kunakuwa na stages za rpm, mpaka unaipata hiyo maximum power, ? Hizo power stages hufanikishwa na hiyo hiyo turbo japo wewe unakuwa huisikii,!, Inaonekana wewe unadili na turbo za magari ya petroli ambayo kiuhalisia turbo zake ni trick kufahamu ufanisi wake, lkn hata kwenye diesel lugha ya turbo imefunguka haipo sahihi
 
t blj,
bora hata unisaidie jamaa ana stori za mtaani ndo wale wanasemaga gari ikifika. spidi 100 ikifungua turbo huipati.....muulize anavyosema turbo ikifunguka mfano at 4000rpm ina maana kabla ya hizo rpm let say 3000 inakuwa sawa na ingine nyingne kama hiyo ambayo ni natural aspirated?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…