Naomba kujua historia ya Urusi

Naomba kujua historia ya Urusi

Ziroseventytwo;eebwanae,! Umesema vema. Sasa mkuu naomba kuuliza swali linalohusu uchumi.

Mimi si mchumi ila nitakujibu kwa kadri ya uelewa wangu


1. Mbali na mafuta na gesi russia(urusi) wanategemea nini zaidi kiuchumi.

Mrusi anategemea biashara ya Silaha hasa kwa nchi za North Africa(The Maghreb)na south East Asia,pia ni muuzaji mkubwa wa diamond European Union.
Kwa bahati mbaya uchumi wa Urusi uko Vulnerable kwasababu haja diversify uchumi wake hivyo anategemea sana import ya goods kutoka European Union.


2. Yanapokutana mataîfa tajiri duniani utasikia: mataifa tajiri 8 (G8) yanayoongoza kwa viwanda pamoja na urusi/russia yatakutana labda davos. Swali. Russia siyo nchi ya viwanda.

For the record G8 is not a formal International Organisation kwasababu hakuna mkataba wowote ambao wameusaini kutengeneza G8. Hivyo usiringanishe G8 na NATO au European Union.
And Yes my friend Russia is an industrialized country. The main difference is that Russia haven't invested much in Super-Civilian Technology.

3.pesa ya russia inathamani gani ukiilinganisha na dola ya u.s.a au na hata euro ya nchi za ulaya?

Without being prejudiced Russian Ruble haiwezi kushindana na Dollar, Euro and The Pound. At least Not for Now.
Hii ni kwasababu Dollar ndiyo the main Currency inayotumika sana ila kufacilitate international trade and exchange.
The Dollar Diplomacy Started during the 1947 all the way to the 1990's during the collapse of the soviet union.
Kumbuka matajiri wengi wa Urusi hata pesa zao wamewekeza nje katika nchi za ulaya hivyo ni ngumu kuifanya currency yao Ruble ishindane na Dollar.

But in the near future inaweza kushindana kwasababu kuu mbili

  1. The Existance of The BRICS
  2. The Formation of The Asian Development Bank under China.
Mwaka huu huu China-Urusi wamesaini deal la Billions and unfortunately wametumia Rubles and Chinese Yuan.
Vivyo hivyo kwa matifa mengine.

Na la pili Bank hiyo hata muingereza na mataifa mengine wanazungumza kujiunga ambapo kupata mkopo ni lazima utapewa kwa currency za Asia hivyo ni lazima Yuan Diplomacy ita weaken the influence of the dollar in Europe.



CC: Abu mohamed , Mchumba, Globu , Ziroseventytwo , mtoto wa bata , ROBERT MICHAEL , saidi yande , Mahesabu , Bayyo , Tanzanite klm , Vlad , t blj , Walas Ba , majeshi 1981 , JustDoItNow , toto zuli , born again pagan , kireri jr , shabani hassani , Ngongo , Mashy Jim007 2 , utafiti , Dotworld , maziku masunga Jr, Bukyanagandi
 
Walas Ba;Shukran mkuu emporar

Maswali

1.Alievujsha siri za urusi kwa western alaifanya ivo ili kuisliti nchi yke au alipandikizwa?

Huyu aliisaliti nchi yake.
Huwa wanitwa defectors. Alidai kwamba hakuridhika na utawala wa Kikomunisti kipindi kile.

2.Kwan mambo muhimu karibu yote ya Urusi yana herufi ''v" kuna utukugu gani kwenye herufi hii au kuna maana gani hasa kwao.

Hili halina Ukweli wowote. Kwasababu lugha za watu wa Slavic region au Eastern Europe zina baadhi ya alphabets zilizoongezwa.
Kama kipolishi kina alphabets za lugha ya kilatini zilizoongezwa.


3.Jehistoria inasema nn kuhusu kuweza kutokea kwa vita nyingine ya dunia?

Siwezi kusema ndiyo au hapana.
Kwasababu History is a place of reference and not a place of residence
Ila mengi hutokea.

4.Uchumi wa urusi unauwezo wa kumudu vikwazo vya marekan?

Indeed. Kwasababu zifuatazo,

  1. kwasababu Urusi ndiyo soko kubwa la European Union
  2. Marekani anategemea sana ushawishi wa kidipomasia wa Urusi hasa katika nchi za mashariki ya mbali kama Iran and Syria
  3. Urusi ana mbadala ambao ni THE BRICS
  4. Mwisho, Vikwazo vikizidi vitaleta mtafaruku duniani na hata Mataifa ya Ulaya yanajua hilo.
Amani ya duniani inategemea ushawishi wa mataifa makubwa kama China na Urusi.
 
Heshima kwako kaka, URUSI ni moja kati ya nchi zenye historia kubwa saana ya kufurahisha.Kwanza urusi zamani iliitwa Russian Empire haikuwa na eneo kubwa kama unavyoliona sasa.Urusi ilitawaliwa kwa zaidi ya miaka 300 na familia ya RAMANOV ambayo utawala wake ulifikia kikomo mwaka 1917 baada ya mapinduzi makubwa ya wakomunisti...kihistoria mfalme anayekumbukwa kuipanua urusi kuwa kubwa mara mbili anaitwa Czar Peter the great au St.Peter.Urusi ilikuwa na nguvu kwa miaka mingi kijeshi kwasababu ya ukubwa wake,rasilimali nyingi na hali yake ya kijeografia ambapo ni baridi sana utoweza kuruhusu wageni kuvamia kirahisi mfano mzuri ni pale ambapo mfalme Napoleon Bournaparte wa Ufaransa alivyoivamia na jeshi la watu kama laki sita hivi mnamo miaka ya 1800's na kupigwa vibaya na mfalme Alexander wa Urusi ambapo aliiamuru miji yote ichomwe moto na kisiachwe chakula ili wafaransa wakija wapigwe na baridi kali ili wafe na kwa bahati nzuri ilitokea hivyo.kadiri miaka ilivyoendelea Urusi ikaanza kuwa dhaifu kwasababu ya mfumo wa Feudalism ambao uliruhusu rushwa na utawala wa watu wachache juu ya wengi walio maskini,kumbuka urusi ni moja ya rainbow states since ina multiple ethnical groups,kama Caucasian,jews,mongols etc.Urusi ilijiingiza kwenye struggle for power mnamo miaka ya 1800's hadi 1900's na matifa ambayo ni madogo kuliko yeye lakini yalikuwa tayari yamesha fanya mabadiliko ya kiviwanda kuliko yeye hivyo kupelekea kushindwa vita hata na kitaifa kama Japani na Uturuki.Mnamo miaka ya 1914 ilitokea vita ya dunia ambapo mfalme wa Urusi bila kufikiria aliliingiza taifa la Urusi vitani kisa kulinda tu heshima yake,wakati huu Urusi ilikuwa haina silaha za kutosha na za kisasa kama automated rifles,aircrafts,tanks and submarines hivyo alitegemea sana silaha kutoka kwa Muingereza,..Mrusi alijiunga na muingereza na Mfaransa kuwapiga adui na majirani zake Germany Empire,Uturuki kipindi hicho ni Ottoman Empire na Austria.Warusi wengi kama 4million walikufa hivyo kuifanya Urusi kuwa Taifa maskini sana na chovu kuliko yotee ulaya.

Mnamo mwaka 1917 mfalme wa Urusi alianza kuua wanaharakati ambao walitaka asitishe vita na kufanya mabadiliko ya kimfumo,watu kama Vladmir Lenin walikuwa exiled ambapo alirudi mwaka 1917 kuendesha mapinduzi makubwa ya kikomunisti ambayo yalipelekea Civil war hadi mwaka 1919 ambapo mataifa mengi dunian hayakupenda ukomunisti hivyo yakasupport wapinzani wa Lennin ila walishindwa.hii ni historia ndogo tuu.

Urusi chini ya Lenin na ukomnisti iliweza kuunda nchi inayoitwa USSR au The UNION OF THE SOVIET SOCIALIST REPUBLICS au CCCP,ambayo iliweza kuanzisha ujamaa ambao kwanza uliwaunganisha warusi wote kwasababu walikuwa na uchumi sawa na hali sawa,pili iliwekeza sana kwenye elimu na pia mwisho jeshi la Urusi lilikuwa linaanza kufundisha watoto wakiwa na umri wa miaka 6.Lenin aliunda mifumo ya kipelelezi iliyoitwa Cheka,NKVD na GRU hivi ndivyo vyombo vilivyoifanya urusi iwe leo unavyoiona.Mwaka 1924 Lenin alifariki akaingia raisi anayeitwa Stalin ambaye alikuwa ni dikteta mbaya ambaye alivitumia vyombo hivyo kuua maadui wa Urusi na kuiba technolojia ya mataifa ya magharibi na kuiletea urusi.1939 dunia iliingia vitani tena ambapo urusi ilionyesha umahiri mkubwa saana kijeshi baaada kumshinda Hitler alipoivamia hapa napo walifanya tena kama kwa Napoleon walikimbia kuelekea Red Square ili wajerumani wadhani kwamba warusi hawana nguvu kumbe walikuwa wanasubiri winter ianze ili baridi iwasaidie.ndaendele kesho:smile-big:

Now sasa the world war came to an end in 1945 ambapo the then Super power Great Britain alikuwa amechoka vibaya sana kiuchumi hivyo Marekani na USSR wakajikuta ndiyo mataifa yenye nguvu duniani kumbuka mrusi na marekani ndiyo walikuwa wa kwanza kuingia berlin walianza kufanya sabotage na assassinations za Nazi leaders lakinin kikubwa walichokifanya GRU ya Urusi ni kuwateka scientists wa nazi na kurudi nao urusi huku na marekani alikuwa akifanya vivyo hivyo.Marekani aliiba project kubwa sana ya ujerumani na kuipa jina la The Manhattan Project ambapo ilipomalizika we all know what happened to Hiroshima na Nagasaki.Mwaka 1945 raisi Franklin delano Roosevelt alifariki dunia na kumwachia madaraka makamu wake mwendawazimu aliyeitwa Harry S Truman ndiye aliyeruhusu mabomu ya atomic code Name FAT MAN na THE LITTLE BOY kuangushwa pale japan.USSR under Joseph Stalin hawakukupenda kile kitendo provided that Japan aliisha surrender na viongozi wake kama General Hedaki Tojo na Sugiyama walikuwa wamejiua.USSR alitumia mwanya wa vita ya pili kujitanua ambapo nchi kama poland,georgia,kazkhastan,ukraine,east germany na vijitaifa vya Eastern Europe vilimezwa kinguvu kitu ambacho kiliyaogopesha mataifa ya Magharibi kwamba nayo yataja mezwa.USSR ilikuwa ndiyo nchi kubwa sana duniani kuliko zote ambapo kijeografia ilikuwa inastretch almost Eleven time zones.Marekani kwa kuigopa urusi alishauri mataifa ya Ulaya ili kujilinda yatengeneze umoja wa NATO mwaka 1947,formation of Israel naton in the middle East mwaka 1948 kumbuka Israel ilitakiwa iwekwe hapa East Africa kwetu lakini walipima ni jinsi gani watzuia the Soviet advance(russian advance),Warusi walitumia mitandao yao kufinance vikundi vya kikomunisti vya Uchina hadi kupelekea mwaka 1949 kushinda na kuwaumiza Wamarekani kwa kiasi kikubwa saaaana kiuchumi.Mwaka 1949 mrusi aliishangaza dunia baada ya kurusha kombora la nuclear ambapo marekani alijua analo peke yake hivyo kupelekea mahusiano yao kudorora,Mrusi ndiye aliyekuwa anaongoza kuwa na sophisticated Rocket technology kuliko Marakani hivyo kufanya the red army kuogopwa saaana.Mnamo miaka ya 1949 hadi mwaka 1950's kulikuwa na kitu kinaitwa The Molotov Plan ambao ulikuwa mpango wa ku counter The Marshall plan ya Marekani ambao ulikuwa unatoa mikopo kwa mataifa yaliyoumizwa kiuchumi na vita ya pili.Warusi walikuja kufanya maajabu tena baada ya kuanza extensive innovation projects ambapo kalashnikov aligundua bunduki yenye nguvu saana aina ya AK47 au Avtomot Kalashnikov,tena miaka ya 60's mrusi ndiye aliyekuwa wa kwanza kurusha Artificial Sattelite kwenye Orbit na tena pia Mrusi ndiye aliyekuwa kwanza kupeleke mtu(cosmonaut)outer space nadhani alikuwa anaitwa Yiri Gargarian kama sijasahau.Mrusi alitumia mitandao ya upelelezi kama NKVD na GRU ambapo walipenyeza serikali za marekani na mataifa ya Nato ambapo walikuwa wanua viongozi wakubwa kwa poisoning na other tactics mfano mzuri waliweza kuunda kitu kinachoitwa THE RING OF FIVE pale Yale UNIVERSITY ambacho kilikuwa kinaua wanafunzi ambao wanaonekana ni future potential American leaders,umoja huu uliundwa na wnafunzi ambao walikuwa ni wamarekani.Urusi ilikuja kuugopesha dunuai mbapo mwaka 1961 walipeleka makombora ya Nuclear pale Cuba huku wakilenga miji mikubwa ya Marekani kama Chicago,Atlanta na newyork huku raisi wa Urusi wakati huo alikuwa anaitwa Nikita Krushchev alikuwa anawatishia Nato kwamba I WILL BURRY YOU,ilibaki kidogo ianze Nuclear War laikini wakubwa huwa wanaogopana yakamalizwa kwa diplomasia,lakini hata CIA wanakiri kwamba vita ingeanza wangeshindwa vibaya kwasababu wlijiamini na kujua kwamba vita haiji kuingia jirani na USA,they were wrong coz this time the bad omen was at their door step.Mrusi alikuwa na military bombers ambazo zilikuwa na uwezo wa kufanya mashambulizi makubwa saaana USA ukiangalia ujirani kati ya Cuba na USA.Mrusi alikuja kushikwa pabaya na USA kwenye the Six Days War ambapo mmoja wa mjasusi wake alikimbia Urusi kama alivyofanya Snowden na kuelekea Uingereza ambapo alitoa secret files za majina ya secret ghost agents wa Urusi ambao walikuwa wanaoperate middle east hivyo kupelekea wauawe na Israel kushinda vita,kushindwa huku kulipelekea Urusi chini ya rais mpya bwana Leonid Brezhnev kutengeneza the lethal weapon ambayo itaweza ku undermine all world intelligence agencies na kuirudisha Urusi katika hali yake,waliunda kitu kinachoitwa KGB.Trust me people even the Mossad feared the KGB,it was notoriuos,efficient killing machine,efficient tool for collecting information,tromendous tool in drafting national policies,masters of infiltration and good suppressors of internal dissidents.KGB itakumbukwa kwa kuifanya Urusi iwe the most feard country in the world hasa chini ya boss wake aliyeitwa Yuri Andropov ambaye alikuja kuwa rais wa Urusi baadae.KGB ilianza kupenyeza majasusi wake hadi kwenye jeshi la Marekani ambapo waliweza kumrecruit US NAVY chief ANthony Walker ambaye alifanya kazi kwa miaka 18 na kgb.Urusi na China walihusika saaana kuwaua Wamarekani kwenye Vietnam war,Urusi ndiyo waliilinda India mwaka 1971 ili USA wsiivamie na kweli USA alishindwa kuvamia India.Ije ikumbukwe Mrusi anakuwa na Nguvu saaana kwasababu huwa habetray allies wake kama USA,ambapo anawalinda NORTH KOREA,VIETNAM,SYRIA,IRAN na mataifa mengine washirika wake wakubwa.Urusi kailinda saaana Syria kwasababu kwanza ni nchi ambayo inavitega uchumi vikubwa saaaana vya mrusi kuna makampuni ya mafuta kama Tatneft,pia kampuni la mafuta la Syria linanua vifaa kama pipes kutoka Russia,pia Syrian Air and Marine companies vessels zake nyingi ni za Mrusi na pia mbali na south Asia soko kubwa la silaha liko Syria sasa.Mrusi hawezi ruhusu mataifa ya magharibi kuvamia kwasababu amewekeza saana Syria kwenye manufacturing industry,Urusi alizubaa libya kuna mikataba ambayo alisiani na Qaddafy ya matrilion ya Pesa ili aimalize mwaka 2011 lakini akazubaa uongozi ulivyoingia mpya dili la silaha akapewa mfaransa Urusi ikaumizwa na ndiyo maana sasa ailitishia vita NATO wakaogopa.Naomba niishie hapo.


CC:
Dotworld , maziku Masunga Jr , Bukyanagandi , MALCOM LUMUMBA

Mkuu nimekukubali
 
Last edited by a moderator:
Bandiko zuri lakini kuna sehem umepotoka..si kweli kwamba Taifa la israel lilitakiwa liundwe east africa...la sivyo km una nondo weka tupite nazo
 
Bandiko zuri lakini kuna sehem umepotoka..si kweli kwamba Taifa la israel lilitakiwa liundwe east africa...la sivyo km una nondo weka tupite nazo

Haya kwa kukusaidia tu hebu soma hiyo nyaraka, uone jinsi Gavana wa makoloni wa Uingereza Lord Chamberlain alivyofanya kikao pamoja na viongozi wa Zionist Congress mwaka 1903.
Akipendekeza wayahudi wanaoishi Urusi wapelekwe Uganda at that time inaitwa British Uganda.
Ilishidikana na haikuwezekana.

Miaka ya 1930's serikali ya Ujerumani chini ya Hitler ilitaka Jewish State iwe Madagascar ila ikashindikana pia kwasababu Muingereza ailikuwa na ajenda zake nyingine.


uganda.jpg

Sources: Encyclopedia of Genocide and Crimes Against Humanity, Encyclopedia of the Age of Emperialism Vol1&2,
Cambridge History of Modern World Vol 1, Cambridge History of the Cold war vol 1&2.
Links:http://www.jewishvirtuallibrary.org/jsource/Zionism/Uganda.html

Nadhani nimekusaidia mkuu

cc: mtoto wa bata , Dotworld , Globu , Mahesabu , born again pagan
 
Last edited by a moderator:
historia ya kupendeza sana kaka..mojawapo ya sifa kubwa sana za warusi ni kutengeneza vitu simpo, rilayabo na vinavyofanya kazi iliyokusudiwa (kwa wale waliopitia jeshini wanaelewa hii makitu sana-bunduki mizinga vifaru na nyambizi NATO walizibatiza "blackholes" manake walikuwa wanshindwa kuzi ditekti mahala zilipo kwenye bahari za pacific na atlantic, midege yao ya MiG ilikuwa inatumia Vacuum tubed radar systems ingawa marubani wa NATO walikuwa wanawabeza hapo mwanzoni lakini walikuja gundua kuwa radar za aina hii z inaathiriw kidogo sana na electronic jamming system, ingawa na zenyewe zilikuwa na ishu zake baadae warusi waliziacha pia---wataalam zaidi wataongezea ama kusahihisha)
 
historia ya kupendeza sana kaka..mojawapo ya sifa kubwa sana za warusi ni kutengeneza vitu simpo, rilayabo na vinavyofanya kazi iliyokusudiwa (kwa wale waliopitia jeshini wanaelewa hii makitu sana-bunduki mizinga vifaru na nyambizi NATO walizibatiza "blackholes" manake walikuwa wanshindwa kuzi ditekti mahala zilipo kwenye bahari za pacific na atlantic, midege yao ya MiG ilikuwa inatumia Vacuum tubed radar systems ingawa marubani wa NATO walikuwa wanawabeza hapo mwanzoni lakini walikuja gundua kuwa radar za aina hii z inaathiriw kidogo sana na electronic jamming system, ingawa na zenyewe zilikuwa na ishu zake baadae warusi waliziacha pia---wataalam zaidi wataongezea ama kusahihisha)

Very simple,
Hasa kwenye Vacuum tubed radar systems.
Hapa ndiyo utakuja kujua umuhimu wa kuwekeza kwenye elimu.
 
Haya kwa kukusaidia tu hebu soma hiyo nyaraka, uone jinsi Gavana wa makoloni wa Uingereza Lord Chamberlain alivyofanya kikao pamoja na viongozi wa Zionist Congress mwaka 1903.
Akipendekeza wayahudi wanaoishi Urusi wapelekwe Uganda at that time inaitwa British Uganda.
Ilishidikana na haikuwezekana.
Miaka ya 1930's serikali ya Ujerumani chini ya Hitler ilitaka Jewish State iwe Madagascar ila ikashindikana pia kwasababu Muingereza ailikuwa na ajenda zake nyingine.


View attachment 282052

Sources: Encyclopedia of Genocide and Crimes Against Humanity, Encyclopedia of the Age of Emperialism Vol1&2,
Cambridge History of Modern World Vol 1, Cambridge History of the Cold war vol 1&2.
Links:http://www.jewishvirtuallibrary.org/jsource/Zionism/Uganda.html

Nadhani nimekusaidia mkuu

cc: mtoto wa bata , Dotworld , Globu , Mahesabu , born again pagan

Kuna kitabu, Khrushchev Remembers,'' kaandika mwenyewe ni kitabu kizuri kwa kuielewa siasa za Urusi kabla na baada ya mapinduzi. Pia kuna movie, ''Nicholas and Alexandria,'' kuna mengi ya kujifunza.
 
Last edited by a moderator:
Kuna kitabu, Khrushchev Remembers,'' kaandika mwenyewe ni kitabu kizuri kwa kuielewa siasa za Urusi kabla na baada ya mapinduzi. Pia kuna movie, ''Nicholas and Alexandria,'' kuna mengi ya kujifunza.

Shukrani sana Mkuu.
 
COLD WAR: PHASE 1- The Bolshevik Revolution and Versailles Treaty

Okay Champs,
Tuanze kuzungumzia vita baridi A.K.A The Cold War.
Kama alivyosema @born again pagan pagan.
Ntajaribu kulelzea kwa kadiri ya uwezo wangu.

Kwanza neno lenyewe Cold War lilitengenezwa na mwandishi mashuhuri mwenye asili ya Uingereza anaitwa George Orwell. Hii ilitokea baada ya Marekani kuangusha mabomu ya atomiki huko japan katika matimbo ya Hiroshima na Nagasaki. Hii ilikuwa ni kumaanisha vita isiyohusisha majeshi ya nchi kubwa kwa moja kwa moja ila tu wanatumia nyanja nyingine kama uchumi na kisiasa (ukomunisti na Ubepari), propaganda na ukusanyaji wa taarifa za kiintelijensia ili kumtishia adui yako.

Hasa kwa ufupi tu, wataalamu wanaanza kusema Cold-War ilianza mara baada ya mapinduzi ya Urusi ya mwaka 1917. Haya mapinduzi kama nilivyoelezea hapo awali katika toleo la kwanza yalileta sera mpya kabisa duniani inayoitwa ukomunisti. Ukomunisti kwa kifupi ni ujamaa uliokamaa; Hii ni sera ya kiuchumi na kisiasa inayofanya mifumo yote ya kimaisha ya nchi kuwa chini ya utawala la kiraia ili kujenga usawa na kuondoa aina yote ya matabaka.

Hii sera ilionekana ni hatari sana kwa mataifa ya Magharibi kwasababu moja kubwa; Hii sera ili iweze kufanikiwa kama aliyeitunga Karl Marx ni lazima dunia yote iwe chini ya ukomunist. Hivyo basi kulikuwa na mpango wa Warusi kupeleka mapinduzi katika nchi za Ulaya, Marekani, Asia na Mwishowe Afrika.
Hili likawa tishio sana kwa mfumo wa kimaisha wa Ubepari hivyo baada ya mapinduzi ya Urusi na vita ya kwanza ya dunia kuisha kulikuwa na Civil War kubwa sana ndani ya Urusi ambapo ule utawala wa watu wachache wanaoijiiita THE WHITES ilipigana na utawala mpya wa Kibolshevik waliojiita THE REDS.
Hawa THE WHITES walisaidiwa na mataifa ya Magharibi kama Marekani chini ya raisi Woodrow Wilson, Ufaransa chini ya George Clemenceau na Uingereza chini ya Waziri mkuu aliyeitwa Lloyd George.
The Bolsheviks wao walisaidiwa sana na Ujerumani amabao walikuwa maadui wa nchi nyingi za Magharibi.

Mwishowe hiyo vita iliishia vibaya baada ya The Whites kushindwa na Mataifa ya Magharibi yakashindwa kuua ukomunisti katika hatua ya kwanza katika miaka ya 1918-1919.
Baada ya hapo ulifanyika Mkutano wa Versailles Ufaransa 1919 ambapo mataifa ya Ulaya yalitoa adhabu kali kwa Mjerumani kwa kusababisha vita ya Kwanza ya dunia.
Katika makubaliano hayo Mjerumani aliumizwa sana kiuchumi na mataifa ya Marekani, Ufaransa na Uingereza kufaidika sana.
Katika mkutano huo walitengeneza Umoja wa mataifa unaitwa The League of Nations ambao uliyatenga mataifa makubwa kama USSR na China.


Ikumbukwe kipindi hichi the world super power alikuwa na Muingereza bado ambapo kitakwimu alikuwa anamiliki asilimia zaidi ya 21% ya Ardhi ya Dunia. Hii ni katika makoloni yake yote ya Asia, Amerika na Mashariki ya kati. Huu ulikuwa ni utajiri mkubwa sana na ulimfanya muingereza ainyonye dunia ipasavyo.
Kipindi hichi Urusi na Marekani walikuwa na influence ndogo ukilinganisha na ya muingereza, ufaransa, Uturuki kipindi hicho ni Ottoman Empire, Japan, Belgium na Spain. Hivyo ikawa ngumu sana kwa mrusi kujitanua ipasavyo.

Huu ndiyo mwisho wa Utangulizi wa Cold War.
Stay tunned for the Second Phase.

BY: MALCOM LUMUMBA a.k.a COBBLEPOTS
 
Last edited by a moderator:
COLD WAR: PHASE 2- Stalin's Russia.

Vladmir Illyich Lenin kiongozi wa kwanza wa USSR alikufa mwaka 1924. Ikumbukwe aliukuwa anaumwa kisukari na alishanusurika na vifo vya risasi mara mbili tofauti hivyo kupelekea afya yake kuzorota hadi kufa.
Lenin alipenda arithiwe na Leon Trotsky ambaye alikuwa ni rafiki yake wa karibu na ndiye aliyetengeneza muundo wa jeshi la Urusi The Red Army pamoja mifumo ya kiintelijensia kipindi hicho ambayo ilikuwa ni The Cheka baadae uliitwa OGPU,NKVD,NKGB,KGB ambao saa hizi inaitwa FSB na SVR. Pia alisaidia sana kutengenezwa kwa chombo cha kijeshi cha upelelezi (Military Intelligence) ambacho mpaka leo hii kipo kinaitwa The GRU.

Leon Trotsky alikuwa ni Myahudi na kipindi hicho wayahudi wengi walikuwa wanatengwa sana Urusi. Hivyo Stalin pamoja na genge lake waliwawahi wakina Trotsky na kundi lake hivyo Joseph Dhughashvili A.K.A Comrade Joseph Stalin akawa kiongozi wa Urusi.
Stalin alitofautiana na Lenin na Trotsky katika kusema Ukomunisti ni lazima uimarike kwanza USSR kisha Upelekwe katika mataifa mengine.
Katika hili Stalin alikuwa sahihi kwasababu bila kufanya hivyo Urusi isingeweza kushinda vita ya pili ya Dunia na umoja ungekuwa umesambaratika mapema.

Stalin alianza FIVE YEARS PROGRAM ambapo alianza kuimarisha Uchumi wa Urusi kwa ajili ya kutawala dunia. Aliongeza kasi ya watu kupata elimu hasa aliwekeza sana katika Upelelezi wa Kiviwanda unaoitwa CORPORATE ESPIONAGE na Military Intelligence. Katika haya majaribio ya kipelelezi Moscow iliweza kupandikiza Majasusi wengi Ulaya, Asia na Marekani.
Ikumbukwe baada ya mapinduzi ya Urusi kulikuwa na wimbi kubwa la wakimbizi kutoka Urusi kuelekea mataifa mbalimbali ya Ulaya. Hivyo walipokelewa vizuri na kupewa Uraia wa Marekani, Uingereza, Ufaransa, Hispania, Ujerumani, China na mataifa mengi.

Moscow ilitimia mwanya huu kupenyeza majasusi katika nchi za Magharibi hasa katika Viwanda, majeshi na serikali. Hawa wanaitwa SLEEPER AGENTS ambao wao kazi yao ilikuja kuonekana wakati wa vita ya pili ya dunia na baada yake.
Mataifa ya Magharibi yaliupuuzia umoja wa nchi za Kisovieti kwasababu ulikuwa ni maskini sana kiuchumi na mbaya zaidi mwaka 1919 Urusi walishindwa vita na Nchi ya Finland hivyo ikawa ni aibu.

Huku nyumbani Stalin alitengeneza kitu kinachoitwa A Closed Society, ambapo mfumo wa kijasusi wa Urusi ulikuwa katika kila kona na kila kitongoji. Kuanzia walimu, wanafunzi, wanajeshi, airport, walinzi wa mipaka,raia wa kawaida na nk.
Stalin alisaini mkataba unaoitwa THE CONCORDE AGREEMENT ambao uliwazuia vijana wa Urusi chini ya miaka ya 40 wasitoke nje ya URUSI; hii ilisaidia sana kuzuia influence ya magharibi nchini Urusi lakini pia ilikuwa inapunguza maendeleo ya kasi nchini humo kwasababu haukuwa unasaidia innovation na biashara.

End of Phase two; stay tuned for phase 3

BY: MALCOM LUMUMBA a.k.a COBBLEPOTS
 
Back
Top Bottom