kenstar
JF-Expert Member
- Aug 24, 2015
- 2,276
- 1,443
Napata shida kujua nani wanapanga ushuru wa magari yanayoagizwa toka nje huwa wanatumia vigezo vipo. Mfano unaweza ukanunua kwa bei mliopatana ukifika nchini wanaikataa bei ulionunulia wanakukadiria kwa bei elekezi kulingana na mifumo ya bei zao. Kitu kingine napenda kujua kwann magari yanayokuja kuinua uchumi na kutoa ajira nchini mfano magari ya mizigo na abiria ushuru wake uwe juu zaid ya gharama ya cif. Nilikuwa napenda kushauri kuhusu magari hasa haya ya mizigo na abiria kuliko kukaa mda mrefu bandarini sababu ya mtu kushindwa kulipia ushuru yangeruhusiwa yaingie yawe na namba maalumu zenye kuonyesha kuwa bado linadaiwa ili kumsaidia mjasiliamali aweze Kuzungushia ili apate pesa ya kulipia kodi au adhaminiwe na bank