Naomba kujua mchango wa Wamisionari katika maendeleo ya elimu Afrika

Hiyo shule iko wapo kwa sasa? Au ilikuwa eneo gani?
Kinyungu,
Shule ya Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika ilijengwa kuanzia mwaka wa 1933 ilipoasisiwa taasisi yenyenyewe.

Waasisi wakiwa Mzee bin Sudi President, Kleist Sykes Secretary pamoja Ali Jumbe Kiro na wazee wengine wa Dar es Salaam.

Hawa wote walikuwa viongozi pia katika African Association.

Mwaka wa 1936 Aga Khan alitembelea Tanganyika na akakaribishwa kuitembelea shule hii.

Mwanafunzi aliyesoma risala ya kumkaribisha Aga Khan alikuwa Abdul Sykes.

Baba yangu na watoto wengi wa miaka ile walisoma shule hii.

Aga Khan akachangia fedha shule ikamilishwe na likajengwa jengo ambalo lipo hadi leo Mtaa wa Makisi Mbwana na Lumumba Avenue.

Serikali ilipovunja EAMWS na kuunda BAKWATA mwaka wa 1968 shule hii ikaangukia mikononi kwa BAKWATA na hivi ndivyo ilivyokuwa kwa mali zote za Waislam.

Hii shule imebadilishwa jina inaitwa Lumumba.
Waislam wameomba warudishiwe jengo lao na shule lakini hadi leo hawajafanikiwa.

Naingia Maktaba kukutafutia picha.
 
Tutajie jina la hilo jengo.

Mnataka kurudishiwa shule yenu na Wakristo wakitaka kurudishiwa shule zao mtasoma wapi? Au vibarazani na mikekani?
 
Sorry sijaelewa ni wapi? Au unamanaisha hii hapa kwenye makutano ya Mkunguni na Lumumba ave? Mbele yake kidogo penye Shopping Mall kubwa ambayo nasikia majengo ni ya Bakwata?
 
Sorry sijaelewa ni wapi? Au unamanaisha hii hapa kwenye makutano ya Mkunguni na Lumumba ave? Mbele yake kidogo penye Shopping Mall kubwa ambayo nasikia majengo ni ya Bakwata?
Kinyungu,
Jengo lipo kona ya Mtaa wa Makisi Mbwana na Lumumba Avenue.



Katika miaka ya 1930s Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika walikuwa wanajenga shule ambayo sote tunaijua lakini hela zilikuwa tatizo jengo likawa linachukua muda mrefu kukamilika.

Sababu ya kujenga shule hii ni kuwa wazee wetu na wao walitaka wawe na mahali pa kuwasomesha watoto wao kuepuka vijana wao kubatizwa katika shule ambazo serikali ya kikoloni iliziweka mikononi kwa Kanisa.

Kleist akiwa kiongozi wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika alitambua mapema sana kuwa tatizo kubwa lililokuwa likiwakabili Waislam ilikuwa ni kukosa elimu ambayo serikali ya kikoloni iliwaachia wamishionari waisimamie.

Si kama Waislam hawakuwa wanatambua faida ya elimu kwa watoto wao.

Wazazi wengi walichelea kuwapeleka watoto wao shule kwa sababu wamishionari walichukua fursa hiyo kuwabatiza.

Kuliko kwa watoto wao kutolewa katika Uislam na kuwa murtad, wazazi wengi waliamua kuisamehe elimu yenyewe kabisa.

Kleist aliona kuwa ufunguo wa tatizo hilo kwa Waislam ilikuwa ni kuanzisha shule zao wenyewe ambazo zitasomesha Qur’an pamoja na masomo mengine.

Wakati ule, na hata hivi sasa, Qur’an ilikuwa ikisomeshwa kwa mtindo wa asili ambapo mwanafunzi anakaa chini sakafuni mbele ya maalim akiwa na ubao wake na juzuu.

Kleist hakuona sababu kwa nini Qur’an nayo isisomeshwe kama elimu nyingine, wanafunzi wakiwa madarasani wakikaa katika madawati.

Alilitoa wazo hili kwa rafiki zake akashauri madrasa ipanuliwe ili masomo mengine yasomeshwe pamoja na Uislam.

Ushauri huu ulijadiliwa kati ya Kleist, Ali Kiro, Maalim Popa Saleh na Shariff Salim.

Wakitambua kazi kubwa iliyokuwa ikiwakabili, waliamua waanze hiyo shule kwa kidogo kidogo kwa awamu.

Nyumba itakayokuwa shule ya muda ilitafutwa na wanafunzi wakaanza kusoma.

Kati ya walimu wa mwanzo wa shule hiyo walikuwa Mzee Ali Comorian na Sheikh Abdallah Iddi Chaurembo ambao walikuwa kati ya wasomi wa Kiislam waliokuwa wakiheshimika.

Wazazi wa Kiislam waliombwa wachange fedha ili jengo la kudumu lijengwe.

Al Jamiatul Islamiyya ikawa inapita nyumba hadi nyumba ikikusanya michango kutoka kwa Waislam.

Bahati nzuri mwaka wa 1936 Aga Khan alitembelea Tanganyika na akafahamishwa kuhusu ujenzi wa shule ile.

Katika hafla ile mtoto aliyesoma risala kwa Aga Khan alikuwa Abdul Sykes akiwa na umri wa miaka 12.

Marehemu Kanyama Chiume amenihadithia kuwa wakati huu alipofika Aga Khan Tanganyika yeye alikuwa anasoma Shule ya Kitchwele na alikuwa katika bendi ya shule iliyompokea yeye akipiga, ‘’triangle,’’ na alinieleza kuwa picha yake yeye akipiga, ‘’triangle,’’ ilitokea katika gazeti.

Aga Khan alitoa fedha na shule ikajengwa New Street si mbali sana na ilipokuwa ofisi ya African Association.

Kleist akawa katika kamati ya ujenzi akikagua kazi hadi ujenzi ulipokamilika.

Hii ni moja kati ya shule za mwanzo kujengwa na Waislam wa Tanganyika.

Jengo la Al Jamiatul Islamiyya lipo limesimama hadi leo kama ushahidi na kumbukumbu za juhudi za Waislam katika kujiletea maendeleo yao.

Serikali katika kuthamini mchango wa Kleist katika kupeleka mbele elimu kwa ajili ya watoto wa Kiislam ikamchagua kuwa katika Provincial Education Committee of Tanganyika Education.

Mwanae Abdulwahid na yeye vilevile akaja kuwa katika Aga Khan Education Committee.
 

Mkuu unayejibizana nae ndio Mohamed Said,mwanahistohisia wa Tanganyika.
 
Mkuu,
Asante sana kwa elimu endelevu kwangu na kwa wale wote wenye "imani" hiyo.
Hakika, bandiko langu na maswali yamejaa upungufu wa " imani" na elimu...walakin. Mtu yeyote asiyejua kitu anapaswa kujua kama itampatia umuhimu katika maisha yake, na hii ni maoni yangu. Hivyo basi, nakutangulizia asante, kwani, nina faraja. Naelimika.

Mkuu, kwa vile suala hili la "mchango wa wamishionari katika maendeleo ya elimu Afrika"ni pana na nina uhakika bado wapo watu kama wewe na wengine ambao wanajua na kuona umuhimu wa "elimu" huu wa "mchango"
Basi mie ninatakujua hivi vitu...au tukubaliane
"Wamishionary" walikuwa na "mission" na moja ni kuleta na kutangaza dini wanazoamini.
Na katika mlolongo huo walileta "elimu" ya kutuwezesha kuelewa hayo? au?
Mkuu, kutoka vyombo husika na masuala ya definition...Elimu ni mchakato wa kujifunza vitu?Naomba nielemishwe.


Mkuu, kutoka mission hizo tukubaliane tulielimika, tulijuwa then na bado tunaendelea kuelimika now kuwa walikuwa na mission tofauti ya maendeleo ya elimu then na hata sasa kwa vile makusudi yao ya kale na labda hata ya sasa yamejaa uhaini.

Sasa nirudi hapa na kuhusu marginalization of islamic teachings and or instututions.


Wapo wengi wenye ujuvi wa haya na wewe mmoja wapo. Tukiweka historia mbele mimi kama muafrika -I really have nothing to do with the ongoing scramble for dominance by either party for control of mind and soul of African peoples." And these parties divinely so, holy and sacred are being handled by the grand and sanctity of the you know who!
That aside, mimi naona mpasuko wa dini ya kikristo uliukiritimba dini ya kiislamu, ilikuwa siasa ni wa kisiasa-neno lenye asili ya uislamu- na bado ni kisiasa, walakin wakristo na waislamu wanaishi bega kwa bega na kuonana ana kwa ana, nafikiri kama wahumini aidha wa kikristo, uislaam n.k kama watu, wanaweza kuungana na kukemea maovu ya wachache katika dhuluma na kujaribu kutenganisha dini katika mandhari za kisiasa Duniani, Ni ndoto zangu hizi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…