Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nchi za European Union zimepiga marufuku karanga kutoka Tanzania kuingizwa kwenye mataifa yao, baada ya kugunduliwa zikiwa na kiwango kikubwa cha sumu. Inadaiwa kuwa wakulima wengi huvuna karanga changa ambayo haijakomaa vizuri, na wanapoianika juani karanga changa huota utando ndani ya gamba ngumu. Utando huo baadaye unakuwa sumu.
Mwezi wa sita serikali iliwakusanya wakulima wakubwa wa karanga, pamoja na viongozi wa vijiji vinavyolima karanga kwa wingi kwenye kituo cha utafiti wa mazao ya nafaka na korosho cha Naliendele Mtwara, wakifundishwa ukulima bora wa zao la karanga na utunzaji wake.