Naomba kujuzwa kuhusu biashara ya mchele

Umewahi kuifanya biashara ya mchele kwa upana? Mimi kitambo nilikuwa na usafiri nimewabebea sana mchele wafanyabiashara wa masasi,newala ,mtwara nk kwahiyo ninachokuambia nakijua
 
Yaani kwa hiyo bei ya 3000 kwa kilo uzia huko huko mbeya maana hata dar bei imeshuka...

Au weka stock mpaka mwez wa 12
Unajua kuna mahala nimeona kaandika kuwa biashara yake inakosa wateja nikamuuliza bei anataja 3000 namuambia mchele umeshuka mno bei huu ni wakati wa mavuno halafu anaanza kuniambia mara umenyooka upo vizuri sio chenga nikaona bora niachane nae amekuwa mjuaji sana
 
Ni sahihi mkuu.
 
Achana naye,kwani wengine wanauza mchele uliopinda? au anajiona yeye ndo wakwanza kuuza mchele.
 
Mkuu huo mchele unao au unasubr wateja uwe mtu kati? Na hata kama umenyooka kama basmart kipind hchi cha mavuno unauza 300k tena upo hukooooo shamba huko unatarajia me mtu wa nanguruwe nije kuuza bei gani? Sijasafirisha, uchukuzi,ushuru, n.k hebu kuwa sirias na hyo bei.
 
Hiyo bei mimi nakufikishia kwako, namaanisha gharama zote ni juu yangu wewe unapokea mchele wako na kuanza kuuza au kuutumia utakavyo wewe mkuu.
Ahsante
 
Weka stock uuze baadaye. Mpanda unavunwa mwingi...Majimoto unavunwa mwingi hatari..kwa bei hiyo na Mbeya utapata hasara tunza uuze ukipanda. Pia nunua na mahindi inaonekana yatapanda hatari
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…