Naomba kujuzwa utagaji wa kuku aina ya Kuroiler na SASSO

Naomba kujuzwa utagaji wa kuku aina ya Kuroiler na SASSO

Mwasapile

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2020
Posts
214
Reaction score
448
Habari wadau!! Kuna ukweli gani kuhusu utagaji wa hawa kuku chotara aina ya SASSO na Kuroiler!

Inavyosemekana kuwa wanachelewa sana kutaga na hawatagi mayai mengi, kama ukitaka kufuga hawa chotara kwa biashara ya mayai hawafai.

Kuna ukweli wowote kuhusu hilo[emoji1489][emoji1489][emoji1489]
 
Hata mimi nahitaji kujua hili jambo.

Kuna rafiki yangu mmoja aliniambia anafuga kuku hawa kwa ajili ya kutaga mayai.

Kauli yake hiyo iliniachia maswali kuhusu maslahi yake wakifugwa kwa ajili ya mayai.
 
Hawa kuku chotara sasso na Kuroiler wametengenezwa kwa minajili ya kutumika kama kuku wa nyama. Ndiyo sababu wanakula sana chakula na huwa na miili mikubwa ndani ya muda mfupi.

Bahati mbaya sana ni kuwa wasambazaji wa kuku hawa hupotosha au kutowaambia ukweli wafugaji. Matokeo yake ni kuwa wafugaji wengi zaidi wa kuku hapa nchini bila kujua hufuga kuku hao wa nyama huku wakiwa na matarajio ya kupata biashara ya mayai.

Kuna training ilifundishwa kuwa kuku hawa hutaga mayai kati ya 85 - 95 hivi kwa mwaka. Hapo usitegemee kupata faida hata kidogo.
 
Hawa kuku wanataga vizuri sana kama utaweza kucontrol chakula, ukiwapa chakula kingi kutaga itakuwa kwa mbinde tena mayai makuubwa yenye viini hadi vitatu.
 
Hawa kuku chotara sasso na Kuroiler wametengenezwa kwa minajili ya kutumika kama kuku wa nyama. Ndiyo sababu wanakula sana chakula na huwa na miili mikubwa ndani ya muda mfupi.

Bahati mbaya sana ni kuwa wasambazaji wa kuku hawa hupotosha au kutowaambia ukweli wafugaji. Matokeo yake ni kuwa wafugaji wengi zaidi wa kuku hapa nchini bila kujua hufuga kuku hao wa nyama huku wakiwa na matarajio ya kupata biashara ya mayai.

Kuna training ilifundishwa kuwa kuku hawa hutaga mayai kati ya 85 - 95 hivi kwa mwaka. Hapo usitegemee kupata faida hata kidogo.
Sijajua kama unayaongea haya kwa uzoefu au ushabiki.

Ili useme juu ya utagaji wao inapaswa tuwe na mfano wa kulinganisha nao. Je unaposema hawana utagaji mzuri, utagaji wao ni mbaya kulinganisha na aina ipi?

Hao waliokwambia kuku anataga mayai 95 tu kwa mwaka, wanazungumzia mwaka wa utagaji au mwaka wa maisha ya kuku? Maana zitakuwa ni akili za ajabu kabisa kumhesabia kuku kataga mayai tisini kwa mwaka bila kuzingatia kuwa anaanza kutaga akifikisha miezi mitano.

Mimi acha nikupe uzoefu, maana Kuroiler ninawafuga. Hawa kuku kwa kuwalinganisha na kuku wa kienyeji wao wanataga zaidi, il ukiwalinganisha na kuku wa mayai hawafikii uwezo wao wa kutaga. Lakini kuna jambo la kujifunza kuwa, hawa kuku wa mayai wanapewa suppliments nyingi sana kufikia huo utagaji, kitu ambacho hatufanyi kwa Kuroiler na kienyeji.

Jambo la pili nikupe maarifa na uzoefu, Kuroiler wanataga kati ya mwezi wa nne na nusu kuelekea wa tano, jambo ambalo halitokei kwa kienyeji na kuku wa mayai. Layers hutaga miezi 6 na kienyeji ni mwezi wa 6 kuelekea 7 na pengine 8 kabisa kama chakula ni haba.

Kuhusu ukubwa wa mayai, kuroiler anataga mayai makubwa kuliko kuku wa mayai. Lakini labda swali la kujiuliza ikiwa unaamini vinginevyo au una experience tofauti ni JE, HAO KUKU ULIONAO NI KUROILER AU ALIYEKUUZIA NDIO KAKWAMBIA NI KUROILER?

Shida moja ni kuwa, Kuroiler wana rangi sawa tu na kuku wa kienyeji, hivyo kuwatambua uhalisia wao si rahisi kwa hiyo watu wengi huuuziwa kuku wasiowajua na huishia kupata famba.
 
Sijajua kama unayaongea haya kwa uzoefu au ushabiki.

Ili useme juu ya utagaji wao inapaswa tuwe na mfano wa kulinganisha nao. Je unaposema hawana utagaji mzuri, utagaji wao ni mbaya kulinganisha na aina ipi?

Hao waliokwambia kuku anataga mayai 95 tu kwa mwaka, wanazungumzia mwaka wa utagaji au mwaka wa maisha ya kuku? Maana zitakuwa ni akili za ajabu kabisa kumhesabia kuku kataga mayai tisini kwa mwaka bila kuzingatia kuwa anaanza kutaga akifikisha miezi mitano.

Mimi acha nikupe uzoefu, maana Kuroiler ninawafuga. Hawa kuku kwa kuwalinganisha na kuku wa kienyeji wao wanataga zaidi, il ukiwalinganisha na kuku wa mayai hawafikii uwezo wao wa kutaga. Lakini kuna jambo la kujifunza kuwa, hawa kuku wa mayai wanapewa suppliments nyingi sana kufikia huo utagaji, kitu ambacho hatufanyi kwa Kuroiler na kienyeji.

Jambo la pili nikupe maarifa na uzoefu, Kuroiler wanataga kati ya mwezi wa nne na nusu kuelekea wa tano, jambo ambalo halitokei kwa kienyeji na kuku wa mayai. Layers hutaga miezi 6 na kienyeji ni mwezi wa 6 kuelekea 7 na pengine 8 kabisa kama chakula ni haba.

Kuhusu ukubwa wa mayai, kuroiler anataga mayai makubwa kuliko kuku wa mayai. Lakini labda swali la kujiuliza ikiwa unaamini vinginevyo au una experience tofauti ni JE, HAO KUKU ULIONAO NI KUROILER AU ALIYEKUUZIA NDIO KAKWAMBIA NI KUROILER?

Shida moja ni kuwa, Kuroiler wana rangi sawa tu na kuku wa kienyeji, hivyo kuwatambua uhalisia wao si rahisi kwa hiyo watu wengi huuuziwa kuku wasiowajua na huishia kupata famba.
Kweli kabisa hata mimi nafuga kroiler wanaangusha mayai ni balaa
Kuku aina ya saso/sasu wanakuwa na maumbo makubwa utagaji wa mayai kwao ni hafifu sana wana uzito na hivyo wanafaa kwa biashara ya nyama unaweza uza Sasu mmoja hadi kwa 40,000tsh na mtu akakubali tu maana wana uzito mkubwa.
 
Kweli kabisa hata mimi nafuga kroiler wanaangusha mayai ni balaa
Kuku aina ya saso/sasu wanakuwa na maumbo makubwa utagaji wa mayai kwao ni hafifu sana wana uzito na hivyo wanafaa kwa biashara ya nyama unaweza uza Sasu mmoja hadi kwa 40,000tsh na mtu akakubali tu maana wana uzito mkubwa.
Asee. Hawa sasso mi nawasikia tu. Nyama yao ni tamu? Kuroiler ndio ninawafuga, wanashawishi kuongeza stock kwa kweli. Tatizo watu wengi wamejiita wauzaji wa Kuroiler, ni shida sokoni.
 
Hawa kuku chotara sasso na Kuroiler wametengenezwa kwa minajili ya kutumika kama kuku wa nyama. Ndiyo sababu wanakula sana chakula na huwa na miili mikubwa ndani ya muda mfupi.

Bahati mbaya sana ni kuwa wasambazaji wa kuku hawa hupotosha au kutowaambia ukweli wafugaji. Matokeo yake ni kuwa wafugaji wengi zaidi wa kuku hapa nchini bila kujua hufuga kuku hao wa nyama huku wakiwa na matarajio ya kupata biashara ya mayai.

Kuna training ilifundishwa kuwa kuku hawa hutaga mayai kati ya 85 - 95 hivi kwa mwaka. Hapo usitegemee kupata faida hata kidogo.
Swali nje ya mada.
Nikiwapa vyakula hivyo kuku wa kienyeji je wanaweza pata miiili mikubwa ndan ya muda mfupi?
 
Sijajua kama unayaongea haya kwa uzoefu au ushabiki.

Ili useme juu ya utagaji wao inapaswa tuwe na mfano wa kulinganisha nao. Je unaposema hawana utagaji mzuri, utagaji wao ni mbaya kulinganisha na aina ipi?

Hao waliokwambia kuku anataga mayai 95 tu kwa mwaka, wanazungumzia mwaka wa utagaji au mwaka wa maisha ya kuku? Maana zitakuwa ni akili za ajabu kabisa kumhesabia kuku kataga mayai tisini kwa mwaka bila kuzingatia kuwa anaanza kutaga akifikisha miezi mitano.

Mimi acha nikupe uzoefu, maana Kuroiler ninawafuga. Hawa kuku kwa kuwalinganisha na kuku wa kienyeji wao wanataga zaidi, il ukiwalinganisha na kuku wa mayai hawafikii uwezo wao wa kutaga. Lakini kuna jambo la kujifunza kuwa, hawa kuku wa mayai wanapewa suppliments nyingi sana kufikia huo utagaji, kitu ambacho hatufanyi kwa Kuroiler na kienyeji.

Jambo la pili nikupe maarifa na uzoefu, Kuroiler wanataga kati ya mwezi wa nne na nusu kuelekea wa tano, jambo ambalo halitokei kwa kienyeji na kuku wa mayai. Layers hutaga miezi 6 na kienyeji ni mwezi wa 6 kuelekea 7 na pengine 8 kabisa kama chakula ni haba.

Kuhusu ukubwa wa mayai, kuroiler anataga mayai makubwa kuliko kuku wa mayai. Lakini labda swali la kujiuliza ikiwa unaamini vinginevyo au una experience tofauti ni JE, HAO KUKU ULIONAO NI KUROILER AU ALIYEKUUZIA NDIO KAKWAMBIA NI KUROILER?

Shida moja ni kuwa, Kuroiler wana rangi sawa tu na kuku wa kienyeji, hivyo kuwatambua uhalisia wao si rahisi kwa hiyo watu wengi huuuziwa kuku wasiowajua na huishia kupata famba.
Interest yangu iko kwa kuku wa kienyeji.
Swali,
Niwafanye nn wawe na miili mikubwa ndan ya muda mfupi na watage sana?
 
Kweli kabisa hata mimi nafuga kroiler wanaangusha mayai ni balaa
Kuku aina ya saso/sasu wanakuwa na maumbo makubwa utagaji wa mayai kwao ni hafifu sana wana uzito na hivyo wanafaa kwa biashara ya nyama unaweza uza Sasu mmoja hadi kwa 40,000tsh na mtu akakubali tu maana wana uzito mkubwa.
40000/= amekuwa mbuzi acha kupotosha
 
Interest yangu iko kwa kuku wa kienyeji.
Swali,
Niwafanye nn wawe na miili mikubwa ndan ya muda mfupi na watage sana?

Ukubwa na uzito wa kuku unategemeana sana na mbegu ya kuku, kuna baadhi ya mbegu za kuku hata uwalishe vipi hawawi wakubwa, ili upate matokeo bora lazma upate mbegu inayoeleweka ndio maana wengi wanakimbilia kufuga hizi breed chotara kama sasso na kuroiler ili wafikie malengo yao ya kuwafanya kuku wawe wakubwa na wazito.

Otherwise unachoweza kufanya ni kutafuta vifaranga ambao wazazi wao wana miili mikubwa na uzito mkubwa ndio utaweza kufikia malengo yako
 
Ukubwa na uzito wa kuku unategemeana sana na mbegu ya kuku, kuna baadhi ya mbegu za kuku hata uwalishe vipi hawawi wakubwa, ili upate matokeo bora lazma upate mbegu inayoeleweka ndio maana wengi wanakimbilia kufuga hizi breed chotara kama sasso na kuroiler ili wafikie malengo yao ya kuwafanya kuku wawe wakubwa na wazito.

Otherwise unachoweza kufanya ni kutafuta vifaranga ambao wazazi wao wana miili mikubwa na uzito mkubwa ndio utaweza kufikia malengo yako
Nimekuelewa
 
Hawa kuku wanataga vizuri sana kama utaweza kucontrol chakula, ukiwapa chakula kingi kutaga itakuwa kwa mbinde tena mayai makuubwa yenye viini hadi vitatu.
Kweli hata wangu wanataga mayai makubwa
 
Sijajua kama unayaongea haya kwa uzoefu au ushabiki.

Ili useme juu ya utagaji wao inapaswa tuwe na mfano wa kulinganisha nao. Je unaposema hawana utagaji mzuri, utagaji wao ni mbaya kulinganisha na aina ipi?

Hao waliokwambia kuku anataga mayai 95 tu kwa mwaka, wanazungumzia mwaka wa utagaji au mwaka wa maisha ya kuku? Maana zitakuwa ni akili za ajabu kabisa kumhesabia kuku kataga mayai tisini kwa mwaka bila kuzingatia kuwa anaanza kutaga akifikisha miezi mitano.

Mimi acha nikupe uzoefu, maana Kuroiler ninawafuga. Hawa kuku kwa kuwalinganisha na kuku wa kienyeji wao wanataga zaidi, il ukiwalinganisha na kuku wa mayai hawafikii uwezo wao wa kutaga. Lakini kuna jambo la kujifunza kuwa, hawa kuku wa mayai wanapewa suppliments nyingi sana kufikia huo utagaji, kitu ambacho hatufanyi kwa Kuroiler na kienyeji.

Jambo la pili nikupe maarifa na uzoefu, Kuroiler wanataga kati ya mwezi wa nne na nusu kuelekea wa tano, jambo ambalo halitokei kwa kienyeji na kuku wa mayai. Layers hutaga miezi 6 na kienyeji ni mwezi wa 6 kuelekea 7 na pengine 8 kabisa kama chakula ni haba.

Kuhusu ukubwa wa mayai, kuroiler anataga mayai makubwa kuliko kuku wa mayai. Lakini labda swali la kujiuliza ikiwa unaamini vinginevyo au una experience tofauti ni JE, HAO KUKU ULIONAO NI KUROILER AU ALIYEKUUZIA NDIO KAKWAMBIA NI KUROILER?

Shida moja ni kuwa, Kuroiler wana rangi sawa tu na kuku wa kienyeji, hivyo kuwatambua uhalisia wao si rahisi kwa hiyo watu wengi huuuziwa kuku wasiowajua na huishia kupata famba.
Mkuu, umafafanua vzr.. Ukiweza em tupia picha, maana nahisi kuna watu washauziwa 'mbuzi kwny junia'🙄
 
Kweli kabisa hata mimi nafuga kroiler wanaangusha mayai ni balaa
Kuku aina ya saso/sasu wanakuwa na maumbo makubwa utagaji wa mayai kwao ni hafifu sana wana uzito na hivyo wanafaa kwa biashara ya nyama unaweza uza Sasu mmoja hadi kwa 40,000tsh na mtu akakubali tu maana wana uzito mkubwa.
Mkuu, kama mi nahataji kufuga shambani kwangu kwa ajili ya kula (nyama), unashauri sasso badala ya kroiler, au?
 
Asee. Hawa sasso mi nawasikia tu. Nyama yao ni tamu? Kuroiler ndio ninawafuga, wanashawishi kuongeza stock kwa kweli. Tatizo watu wengi wamejiita wauzaji wa Kuroiler, ni shida sokoni.
Mkuu, wastani wa uzito wa hao kroiler ukoje?
 
Ha ha ha.. Mkuu, unajua bei g ya kuchi pure?

Achana na kuchi sasa , kuna huyu kuku anaitwa Brahma wanauzwa mmoja kwa 1.5m
IMG_3115.jpg
 
Back
Top Bottom