Naomba majibu kwa anaejua kuhusu mambo haya kwenye mchezo was soka

Rekondoboshiki

JF-Expert Member
Joined
Nov 24, 2017
Posts
228
Reaction score
280
Salaam,

Naomba kujua iwapo mpira wa kurushwa ukirushwa na kuingia moja kwa moja wavuni kwa timu pinzani bila ya kuguswa na mchezaji yeyote, Je hilo litakuwa ni bao halali?

Na je, ni idadi gani ya wachezaji ambao wakipewa kadi nyekundu inam'bidi refa aahirishe pambano.

Ni hayo tu kwa sasa.
 
LAW 15 INASEMA
mpira wa kurushwa ni njia ya kuanzisha tena mpira baada ya kutoka pembeni ya uwanja.
mpira wa kurushwa unakuwa unatolewa kwa timu pinzani ikiwa mchezaji wa mwisho kuugusa mpira huo ni kutoka timu nyingine wakati mpira huo utakapokuwa umetoka wote kupita mstari kupitia ardhini au juu hewani.

hakuna goli litafungwa kwa mpira wa kurusha moja kwa moja bila kuguswa na mchezaji mwingine tofauti na mrushaji. na ikitokea mrushaji amerusha mpira kuelekea golini kwake mwenyewe na ukaingia golini pasipo kuguswa na mchezaji mwingine yoyote utahesabika kuwa ni pigo la kona


hakuna limit ya refa kutoa red card kwa timu moja lakini ikitokea kuwa wachezaji wa timu moja wamepewa red cards wakapungua chini ya saba uwanjani lazima referee ahairishe pambano bila kuangalia muda uliokwishachezwa
 
Hilo haliwezi kuwa goli...
Ili mchezo uweze kuwa valid inabidi idadi ya wachezaji isiwe chini ya saba pamoja na goalkeeper kwa upande wa timu moja!
 
TATIZO SIO KURUSHA AKISHARUSHA LAZIMA MPIRA UGUSWE NA MCHEZAJI MWINGINE NDIO UHESABIWE GOLI USITUNGE SHERIA ZA MPIRA ZISOME ZILIZOPO

Swali lako gumu sana. Labda wamfufue Albert Enstein atupatie jibu la swali lako.
 
SIO GOLI halali!
Mpira wa kurushwa lzm uwe hai kwa kuguswa na yyt kwa njia yyt isipokuwa mikono kabla haujaingia wavuni
Rule # 15
Watu hawajui kwamba kuna sheria 17 za mpira wa miguu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…