Naomba mnijuze kuhusu wapangaji wangu.

Naomba mnijuze kuhusu wapangaji wangu.

Lipijema

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2015
Posts
830
Reaction score
1,223
Wanajamvi wenzangu naomba msaada wenu mnishauli/ munieleweshe kisheria kuhusu mimi na wapangaji wangu. Hawa wapangaji wapo kwangu sasa ni miaka mitatu tangu nimewapangisha ndani ya nyumba yangu hii, kwa ujumla ninaishi nao kwa amani tu, tatizo lao kubwa kati yao na mimi ni ulipaji wao wa kodi kwa kila mwezi. Mkataba wetu ilikuwa ni kutanguliza kodi ya miezi mitatu mitatu kwa kila muhula, kwa hali ya ubinadamu tu wakati mwingine huwa nawavumilia ili wapatapo wanilipe, sasa basi katika kuvumiliana huku nimejikuta wamelaza kodi ya pango ya miezi saba ndani ya hii miaka mitatu bila ya kunilipa! Nimewataka wahame kwangu kwa vile hii ni dalili ya kutonilipa kwani malimbikizo yamesababisha deni kuwa kubwa, swali ni je, hapa sheria inasemaje kuhusu haki yao na yangu pia? wanayo haki ya kuwapa muda!? Nami kuhusu pesa ninayo wadai je?Msaada wenu wana jukwaa.
 
ngoja nisubiri michango ya wananzengo huku nikiwa siti ya kwanza na popcorn
 
Wape notice ya miezi 3 ya kutaka kuchukua nyumba yako kwa ajili ya ukarabati mkubwa. Kwenye notice wakumbushe na deni Lao.

Nifanye mjinga uwatimue.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama mliandikishana kwa mkataba, basi fuata utaratibu

Sent from my SM-G570F using Tapatalk
 
Nenda kwa mwenyekiti wako au balozi mkuu

Sichenji buku kwa njaa ya siku moja
 
Jf ilivyo ya ajabu nowadays unaweza kuta mleta mada anaishi kwenye sebule ya Shemeji yake na hajawahi kuwa na kiwanja.

I'm sorry to be out of the topic

Sent from my TECNO CA6 using Tapatalk
Aliwazalo mjinga....!
 
Back
Top Bottom