naomba msaada kwa wale wanaofahamu.

naomba msaada kwa wale wanaofahamu.

Daddo

JF-Expert Member
Joined
Jan 17, 2013
Posts
1,435
Reaction score
1,025
jamani mimi nina ndugu yangu wa kike alimaliza shule miaka ya nyuma ila si sana. alipomaliza alkuwa na bahati kweli maana alikuwa na div 4 ya 26 lakini kwa kuwa combination ilibalance basi alipata shule na akaendelea na masomo.baadaye kidogo kwenye mwezi wa kumi na moja alifukuzwa shule kwa ujauzito. basi akaja home kajifungua na sasa mwanaye ana mwaka mmoja.
Sasa tukaona si vyema tumuache hivihivi basi tukamshauri aombe chuo cha ualimu na kweli aliomba lakini bahati mbaya hakuchaguliwa. kwa sasa amesubiri kuona kama atapata nafasi kwenye second selection japo ni ngumu. mie kama uncle wake nimeona nije hapa niulize waungwana kama kuna mwenye information yoyote kuhusu hizi nafasi au mwenye kujua chuo cha private ambacho gharama zake si kubwa sana aniambie maana naona maji yalishamfika shingoni.
Natamguliza shukurani kwenu wanajamii ila kama unaona unamsaada wa mawazo mengine pia unaweza kuchangia.

NB:Matokeo yake ni
kisw C
Eng C
Hist C
Geo D
Commerce F
Maths F
B/keeping D
civic D
 
inabid ujipange tu maana vyuo ving vya private vinacheza kwe mmoja na kuendelea kama greenbird kipo mosh ada m1 na laki4
 
Back
Top Bottom