Naomba msaada wa kiasi chochote cha fedha niweze kujikimu kwa muda nitafutao ajira

Naomba msaada wa kiasi chochote cha fedha niweze kujikimu kwa muda nitafutao ajira

Za leo ndugu zangu,

Naitwa Thandiwe, ni mkazi wa Dar lakini kwa sasa nipo mkoani. Kiukweli hali ya maisha imekuwa ngumu hatukatai ndugu zangu hasa sisi tuliopo mikoani kwa sasa ila kiukweli, kuna wengine tunashindwa jihusisha na mambo yasiyo na maadili ili kujipatia kipato, kwani ninaamini kheri kuomba msaada unapokwama kuliko kujificha na kufa na njaa.

Ombi langu kwenu wenzangu, msaada wa kiasi chochote cha pesa ili kusukuma siku wakati nikiendelea kufuatilia ajira. Kwa yeyote atakaeguswa nipo tayari kuweka mawasiliano yangu PM ili kujieleza zaidi.

Mungu awabariki wote watafutaji.


Tafadhali weka picha yako bila kudanganya kama mdau yeyote atafika bei.
 
mimi nadhani ungeomba kazi dada angu ata mtu akikupa ela ya kula siku mbili baada ya izo siku tatizo litabaki lilelile pole kwa ayo majaribu dadaake
Nashukuru kwa ushauri,ila nimekuwa nafanya sehemu,ila kwa sasa office imefungwa kwa muda sio moja kwa moja
 
Back
Top Bottom