Naomba msaada wa kisheria!

Naomba msaada wa kisheria!

NO NEM

New Member
Joined
Dec 28, 2011
Posts
3
Reaction score
0
Mimi ni mpangaji ambaye mwenye nyumba wangu hakunipa mkataba wowote wakati naingia kwenye nyumba yake, mwanzoni mwa mwezi huu wa kwanza aliniletea notisi inayoeleza kuwa mwisho wa mwezi huu inatakiwa nihame kwa sababu anataka kuhamia kwenye nyumba yake, hata hivyo kodi yangu imeisha trh 6/1/2013. tatizo ni kwamba mwenye nyumba analazimisha kuleta mafundi wa kufanya matengenezo ndani kwangu wakati mimi na vitu vyangu nikiwa bado naishi kwenye hii nyumba yake. Jamani hii ni sahihi? kama si sahihi nifanyeje?....msaada tafadhali
 
Mwenye nyumba anatakiwa kukupa notisi ya Siku 30 kama anahitaji uhame. Uwe na mkataba wa maandishi au la. Baada ya siku 30 unatakiwa uhame vinginevyo ana haki ya kumleta Dalali wa Mahakama kukuondoa kwa gharama zako. Kabla ya siku 30 kuisha mwenye nyumba hana haki ya kukubughudhi kwa namna yoyote ile kama kwa kuleta mafundi, kukufungia nje n.k. Akifanya hivyo una haki ya kumshitaki kwenye Baraza la Kata au Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya.
 
Mwenye nyumba anatakiwa kukupa notisi ya Siku 30 kama anahitaji uhame. Uwe na mkataba wa maandishi au la. Baada ya siku 30 unatakiwa uhame vinginevyo ana haki ya kumleta Dalali wa Mahakama kukuondoa kwa gharama zako. Kabla ya siku 30 kuisha mwenye nyumba hana haki ya kukubughudhi kwa namna yoyote ile kama kwa kuleta mafundi, kukufungia nje n.k. Akifanya hivyo una haki ya kumshitaki kwenye Baraza la Kata au Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya.

Nashukuru sana kwa msaada wako wenye manufaa!
 
Back
Top Bottom