naomba msaada wa wazo la biashara HALALI ya kufanya

mutisya mutambu

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2010
Posts
208
Reaction score
82
msaada wa mawazo jamani,nahitaji kufanya biashara itakayo nsaidia kuyaweza maisha haya magumu yanayonikabili.mtaji nilionao ni 300000.tu nifanye biashara gani?
 
Fungua GENGE; kama upo DAR nenda asubuhi kariakoo nunua vitu kwa jumla halafu unakuja kuuza mtaani kwako. Tengeneza mazingira mazuri ya biashara, ikiwezekana weka huduma ya kupeleka bidhaa nyumbani kwa mteja. Tafuta wateja wa kudumu hapo mtaani kwako kwa kuwatembelea na kuwaeleza adhima yako ya kuwaletea bidha za jikoni kama nyanya, vitunguu n.k. kisha tafuta kijana ambae utampatia baiskeli halafu asubuhi anapita kwa wateja wako kuchukua order ya mahitaji yao na baadae kuwasambazia.
 
Ushauri mzuri,nami nakuunga mkono.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…